Mtemikwila
JF-Expert Member
- Aug 29, 2013
- 1,389
- 1,065
Epuka fujo, kimbia vurugu, acha choko choko, kubali kuwa mjinga mwenye faida, kuliko kuwa mjanja mwenye hasara. Kwa mwoga huenda kicheko, lkn kwa shujaa huja kilio.
Baadhi ya watu wamo gerezani, pasipo kutarajia, kwa sababu tu, walisukumana na mtu mgonjwa, akafa kwa kuanguka.
Idadi kubwa ya watu ambao hawajasoma, si kwamba walikua hawana akili shuleni, lkn chanzo ni wazazi wao, walifanyiana vurugu, wakatengana, na watoto wakaambulia hasara.
Angola ni nchi tajiri sana, lkn haina wataalamu wengi, kwa ajili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, iliyo dumu kwa miaka 35, pia vilema ni wengi, kwa ajili ya land mines, mabomu ya ardhini, yaliyo achwa wakati wa vita hivyo, na serikali inatumia fedha nyingi sana kuyaondosha, maana wakulima wanashindwa kuzalisha, ingawa ardhi ina rutuba.
Hayo ni baadhi tu ya athari za vurugu, choko choko na fujo. Tanzania ni nchi nzuri mno, watu wake ni waungwana pia serikali haina dini, raia wana uhuru wa kuabudu, katika dini yoyote, mradi tu ufuate sheria na kanuni zilizopo, oa na olewa na yeyote umpendaye, kwa dini yoyote, siku na saa yoyote, la endapo huko kwenye dini hawakutaki, lkn ukienda kwa mkuu wa wilaya atakufungishia ndoa yako.
Tanzania mnataka nini? waTanzania nyie, Mungu awape nn? Kila mtu, kila kiumbe kina mapungufu yake, ndiyo maana, tunakula samaki lkn miiba yake, tunaitoa, samaki ana shombo, tunamtia ndimu, lkn je si tunamla? Basi na maisha, na watu, wapo ivyo ivyo, tuangalie mazuri yao, na mapungufu yao, ni kawaida hiyo, Mungu mwenyewe, ameumba viumbe vyote vipo hivyo hivyo.
Je, hili nalo linahitaji mahubiri ya padre, shehe na mchungaji? Hebu fikicha ubongo, Mtanzania, ili ujifikirie, kama wakimbizi wa DRC, Burundi, wanakimbilia Tanzania, je ww mTanzania ukifanya fujo utakimbilia wapi?
Nawakilisha nikiwa mpakani kabisa na msumbuji huku,[HASHTAG]#Mtajijua[/HASHTAG] wenyewe..
Baadhi ya watu wamo gerezani, pasipo kutarajia, kwa sababu tu, walisukumana na mtu mgonjwa, akafa kwa kuanguka.
Idadi kubwa ya watu ambao hawajasoma, si kwamba walikua hawana akili shuleni, lkn chanzo ni wazazi wao, walifanyiana vurugu, wakatengana, na watoto wakaambulia hasara.
Angola ni nchi tajiri sana, lkn haina wataalamu wengi, kwa ajili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, iliyo dumu kwa miaka 35, pia vilema ni wengi, kwa ajili ya land mines, mabomu ya ardhini, yaliyo achwa wakati wa vita hivyo, na serikali inatumia fedha nyingi sana kuyaondosha, maana wakulima wanashindwa kuzalisha, ingawa ardhi ina rutuba.
Hayo ni baadhi tu ya athari za vurugu, choko choko na fujo. Tanzania ni nchi nzuri mno, watu wake ni waungwana pia serikali haina dini, raia wana uhuru wa kuabudu, katika dini yoyote, mradi tu ufuate sheria na kanuni zilizopo, oa na olewa na yeyote umpendaye, kwa dini yoyote, siku na saa yoyote, la endapo huko kwenye dini hawakutaki, lkn ukienda kwa mkuu wa wilaya atakufungishia ndoa yako.
Tanzania mnataka nini? waTanzania nyie, Mungu awape nn? Kila mtu, kila kiumbe kina mapungufu yake, ndiyo maana, tunakula samaki lkn miiba yake, tunaitoa, samaki ana shombo, tunamtia ndimu, lkn je si tunamla? Basi na maisha, na watu, wapo ivyo ivyo, tuangalie mazuri yao, na mapungufu yao, ni kawaida hiyo, Mungu mwenyewe, ameumba viumbe vyote vipo hivyo hivyo.
Je, hili nalo linahitaji mahubiri ya padre, shehe na mchungaji? Hebu fikicha ubongo, Mtanzania, ili ujifikirie, kama wakimbizi wa DRC, Burundi, wanakimbilia Tanzania, je ww mTanzania ukifanya fujo utakimbilia wapi?
Nawakilisha nikiwa mpakani kabisa na msumbuji huku,[HASHTAG]#Mtajijua[/HASHTAG] wenyewe..