Mnaotafuta ajira kuweni makini na matapeli

Mnaotafuta ajira kuweni makini na matapeli

Syston

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2017
Posts
243
Reaction score
354
Habari wadau,

kumeibuka utapeli unaowalenga wahitimu wa vyuo, hasa ukizingatia kipindi hiki kila mtu anatafuta ajira na zimekuwa ngumu kwelikweli, hivyo matapeli hawa wamekuja na njia ya kutangazia watu kuna nafasi za kazi mahali fulani na kutoa mawasiliano yao.

Ukishawatafuta wanakuomba pesa kwa ajili ya fomu na na vitu vingine vya ajabu ajabu, kuna mtu ameombwa atume pesa ya fomu ya fire extinguisher, teh teh teh.

Kuweni makini na mtu anayeitwa ERNEST, ndivyo anavyojitambulisha na anatangaza nafasi za kazi Migodini hasa GGM, huyu ni tapeli anaanza kwa kuomba hela ya medical checkup form, na pesa zake ni zile ambazo huwezi enda polisi, 5000, 6500 akienda sana 10000.

anatumia email ya yahoo kuweni maikini.

Nawasilisha.
 
Kuna tapeli mwingine pale Makumbusho, ana kiofisi chake kinaitwa Job junction.
Kila ikipita wiki 2 anatoa tangazo hilo hilo la customer care, ukituma maombi anakuita na anakuambia ulipe elfu 25 akutafutie kazi kwenye makampun.
Ila ndio nitolee hiyo


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kuna tapeli mwingine pale Makumbusho, ana kiofisi chake kinaitwa Job junction.
Kila ikipita wiki 2 anatoa tangazo hilo hilo la customer care, ukituma maombi anakuita na anakuambia ulipe elfu 25 akutafutie kazi kwenye makampun.
Ila ndio nitolee hiyo


Sent from my iPhone using JamiiForums
Makumbusho stend! Ukiingia utamkuta mdada 1 hivi atakukaribisha then atakja huyo jamaaa hahahhaaa wanakamata wengi wasiojua mchezo!
Nilienda pale 2018 , December baada ya kuambiwa lipia 20,000/= ili tukusambazie cv yako nikaona hapa n kusepaaaaaa
 
Waambie matapeli wote wanipigie niwape pesa ya kula bure ila sharti pekee waje wakiwa hawajavaa chupi/boksa.!
 
Makumbusho stend! Ukiingia utamkuta mdada 1 hivi atakukaribisha then atakja huyo jamaaa hahahhaaa wanakamata wengi wasiojua mchezo!
Nilienda pale 2018 , December baada ya kuambiwa lipia 20,000/= ili tukusambazie cv yako nikaona hapa n kusepaaaaaa
Kama ni kweli wanazisambaza hizo CV yaweza kuwa hakuna utapeli, maana kupata au kukosa ni matokeo tu.
 
Poleni sana watapeliwa siku zote changamoto za maisha hufanya watu wawe wabunifu wa kutafuta riziki no matter kama ni legal au illegal cha muhimu ni kuwa makini kufanya reasoning ya kila jambo kabla ya uamuzi. Utapeli upo na hauwezi kuisha na wewe kwa nafasi yako ukipata nafasi itumie kujikwamua kimaisha
 
Ndyoo, nilipigwa buku 4 jero mkuu, nilitumiwa hiyo interview invitation ya maana full of details, mpaka nikahisi nishapata kazi hata kabla, nikaona inabidi kuchangia gharama kidogo for refreshment after interview, nikasita refreshment ya nini mi nataka kazi, ila nikaona si mbaya ni amount ndogo tu nikatuma, kumbe nishapigwa na interview hamna aisee, mitapeli naichukia mimii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu wa GGM alishataka kunitapeli na mie, 2years back Yani kila kitu alikua anataka papo kwa hapo.
Aliponiomba elf 5 anijazie medical details nikaanza kumtilia shaka, alafu alikia na namba Kama tatu nikamrudia my aloniunganisha nae, akasema nisimpe Basi alivomrudia hata sikuona simu ya msisitizo.
Hawa matapeli heri wakukute kwenye msoto huwez toa kitu hata uwe desperate vipi na ajira.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom