Mnaoshea siri zenu na marafiki

Mnaoshea siri zenu na marafiki

Mimi sijui niwaweke kundi gani?
Mnajitengenezea silaha za kuwaangamiza wenyewe
Ushindwe kusea na ndugu yako iloishi nae miaka zaidi ya ishirini.. Ila unaweza kushea na mskaji au shoga yako mlokutana njiani serious?
Labda sababu sio mtu qa famjlia yako.. Ni mtu wa mbali huko
Lakini jua huyo ni binadamu kama binadamu wengine.. Siku akikuamulia umekwisha.. Na kama ndo aale wenye siri nzito umekwisha
Kiliwahi tokea kisa kikanifunza.. Nlikua na ndugu yangu huyo.. Ye alikua na shoga ake waloshibana.shoga mke wa mtu.. Basi ikawa haipiti siku bila kupigiana simu.. Mmoja akipata shida anakimbilia kwa mwingine.. Familia zinajuana.. Walidumu karibu miaka nane.. Walisaidiana mengi sana
Ila siku ya siku ikafika kwa kisa kidogo sana wakashindwa kuelewana wakatibuana
Basi ndo ikawa michambano kila siku
Ndugu akamwambia "unajua nna siri zako nzito? Unakumbuka? Sasa endelea nitibue nami naachia kwa watu hadi mumeo Uone
Bibie tangu dakika hiyo kaufyata kimya...aongee hajipendi
Siri zilitumika zana ya kummaliza.
Hata angesema achia zangu sababu nna zako bado angepata hasara kubwa sana..

Huyo unaeshea nae siri zako na mambo yako siku mkikosana umefikiria itakuaje?
Ujumbe mzuri na ni funzo pia,asante mtoa mada
 
Nashukuru Mungu kuzaliwa mkimya na mpole na mtaratibu na si muongeaji na mwenye uwezo wa kuhifadhi mambo / kuvumilia...

Nampenda sana Dadii sababu.... ananipa akili ya Maisha.... he is a life saver.

Kitu kikinizingua sana ambacho ni changu binafsi siwezi mwambia mama, ntamsimulia ndugu au shosti ila jinsi ntavoisimulia namvika uhusuka mtu mwingine mie nakaa pembeni halafu nasikiliza mawazo atayotoa.

Kukaa na vitu bila kuvitoa moyoni ndo ile mnaona mtu kadondoka ghafla, akafa ghafla n.k. Pia tangu niingie JF huku kumekuwa sehemu kubwa na kusema siri zangu kwa jinsi ambayo mtu akija kwenye uhalisia wa maisha hawezi jua huyu ndo Kasie.

Huo ndo mtindo wangu wa maisha na yote ya yote siri nyingine huwa nazissema hotelini, naenda hotelini mwenyewe nafungua maji kwenye shower navua nguo zote nawasha TV channel ya mziki. Naanza kuimba na kucheza kisha ion abetween nasema siri in a way kama namsimulia mtu, kisha naoga deep shower nikitoka hapo nakuwa relieved.

K' Matata.
 
Wnawake ndio tunaongoza kwa kupenda kushare na marafiki
Unakuta mtu hadi za wapenzi mtu anashare na her friend
Daaah ndio maana marafiki wengi wanajikuta wanashare hadi wapenzi kwa style hizi maana mtu anajikuta anajua raha na karaha za huyo mtu.
Sipendi kabisa habari za kushare story za ndani na mtu niliyekutana nae kimjinijini
 
Write your reply...sasa unataka niwaambie ndugu mi ni pusha navuta bangi niwaambie na machimbo wanichome ? siri hii namwambia pusha mwezangu ambaye ni rafiki
 
Ni vizuri kujifunza kufunga domo lako, pia mara mia kumuamini adui yako kuliko rafiki, urafiki kwenye social issues tuu siyo mambo yangu serious kama biashara, familia na mahusiano

Natengeneza marafiki wengi lakini siwapi nafasi ya kunifahamu sana/kutumia mda mwingi pamoja

Marafiki wengi wanafanya vitu kwa ajili ya kukuridhisha, na siyo uhalisia wao, but deep down wamejaa wivu, kijicho na chuki, hawapendi kuona umeendelea zaidi yao na hayo yote anayamezea utakuja kujua siku mmekorofishana au kuingia 18 zake
 
Umesema ukweli mkuu
Ni vizuri kujifunza kufunga domo lako, pia mara mia kumuamini adui yako kuliko rafiki, urafiki kwenye social issues tuu siyo mambo yangu serious kama biashara, familia na mahusiano

Natengeneza marafiki wengi lakini siwapi nafasi ya kunifahamu sana/kutumia mda mwingi pamoja

Marafiki wengi wanafanya vitu kwa ajili ya kukuridhisha, na siyo uhalisia wao, but deep down wamejaa wivu, kijicho na chuki, hawapendi kuona umeendelea zaidi yao na hayo yote anayamezea utakuja kujua siku mmekorofishana au kuingia 18 zake
 
Back
Top Bottom