Nakapanya
JF-Expert Member
- May 22, 2012
- 2,096
- 708
Mwanzoni nilikuwa najiuliza kwanini asilimia kubwa ya Mabibi harusi huvaa gauni jeupe na si vinginevyo?katika kutaka kujua hilo;nikawauliza baadhi ya watu na majibu yao yalifanana,walisema hivi;NGUO NYEUPE HUMMANISHA KWAMBA BI HARUSI BADO NI MSAFI/HANA DOA NABADO ANAO USICHANA WAKE (BIKIRA) AMBAYO NI ZAWADI KWA BWANA".Sasa hali ilivyo siku hizi watu hufunga ndoa wakishakuwa wamechakachuana na usichana unakuwa umeondoka,tena wengine hufunga ndoa wakati tayari wakiwa na watoo au wajawazito.Je kuna maana yeyote ya kuendelea kutumia gauni jeupe kwa tafsiri hiyo hapo juu?