Mnaoenda kwenye vituo vya watoto Yatima ili kuombewa dua, mnawafanyia ukatili na unyanyasaji hao watoto

Mnaoenda kwenye vituo vya watoto Yatima ili kuombewa dua, mnawafanyia ukatili na unyanyasaji hao watoto

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
19,349
Reaction score
36,300
" Aisee ndugu yangu ukitaka jambo Lako liende wewe nenda kafanyiwe Dua na watoto yatima. Yani majibu ni papo kwa papo. Dua zao Mungu anazipokea hapo hapo "

Hayo si maneno yangu, bali ni maneno ya MTU mmoja mvivu wa kufikiri na mkwepa majukumu.

Uliongea na Mungu Lini akakwambia huwa anapokea na kujibu dua za watoto yatima papo hapo?

Kama ingekuwa kweli basi si ingefaa tuwaue walau wazazi millioni moja kila nchi halafu tujenge vituo vya kulelea watoto yatima viwe ndio makanisa au misikiti watu wawe wa naenda kuomba Dua.

Maelfu ya watu wana amini katika uzushi huu na hawa ndio huenda kwenye vituo vya kulelea watoto yatima na viroba vya mchele kilo tatu na shilingi elfu 20 ili wakeshe na watoto yatima wakiomba Dua.

Mnyanyasaji mkubwa wewe wa watoto. Hivi kweli watoto wako ulio wazaa mwenyewe unaweza kuwatesa kiasi hicho?

Mtoto wa miaka mitano, Saba au Tisa unakesha nae kuanzia saa moja usiku hadi saa 11 asubuhi mnaomba Dua? Unataka mpige Yasin Mia 4 ndani ya usiku mmoja.

Yote hiyo unataka eti biashara yako ipate wateja. Hiyo ni sadaka umetoa ama ni unyanyasaji una fanya?

Kwa akili yako mbovu, unadhani huyo Mungu atajibu Dua yako wewe unae watesa na kuwanyanyasa watoto kiasi hicho?

Kama Mungu atajibu dua hiyo basi atafunga biashara yako kabisa na kukunyima rizki ili siku nyingine usipate muda wa kwenda kuwasumbua viumbe wake. Maana akijibu dua yako kwa kukuletea wateja kwenye biashara yako utaamini ujinga wako na kitakacho fata utaenda kukesha nao siku tatu ufunge nao siku tatu mpige Yasin Mia 4 ili wateja waongezeke ndani ya hizo siku tatu. Mafi yako.

Na nyie wamiliki wa vituo vya kulelea watoto yatima acheni kuwatesa na kuwanyanyasa watoto wa watu.

Mnawafanya kitega uchumi. Mnawatesa na kuwafanyia ukatili wa Hali ya juu.

......

Jana ilikuwa birthday yangu. One day before nilienda kwenye kituo cha kulelea watoto yatima kuongea na mwenye kituo aaandae watoto Mia plus waje wale na kunywa pamoja nami.

Nilikuta mmiliki niliemzoea hayupo , yupo binti yake. So nikamwambia kesho Nina birthday yangu. Akaniwahi duh umefanya la maana kweli. Tena inabidi ufanye dua kubwa sio vidua vya elfu thelathini au 50. Ufanye dua kubwa ili Mambo yako yanyooke.

I was not even surprised.

"NINA TOA SADAKA KWA SABABU NIMEBARIKIWA NA SIO KWA SABABU NINATAKA KUBARIKIWA"

Anyways Nika muenjoy " Dua kubwa ndio inakuwaje hiyo"?

Majibu yake sasa 👇👇👇👇

Tunachinja mbuzi, cow au kondoo. Chakula kinapikwa then watoto wanakusomea Dua kuanzia asubuhi saa kumi na mbili hadi saa sita usiku"

I was like Jesus! This amount to child abuse.

I told her don't worry about the Dua. I just want to enjoy with these children. I don't want to stress them.

Ifike muda sasa jamii ianze kupaza Sauti dhidi ya unyanyasaji huu dhidi ya watoto yatima kwenye vituo vya kulelea watoto yatima.

Kama wanakuja watu wa aina hii kila siku maana yake ni kwamba hao watoto wanapewa kazi hii ya dua kila siku. Can u imagine.


Kuna mijitu mingine ya hovyo inachukulia vituo vya kulelea watoto yatima kama vilinge vya waganga wa kienyeji.

Mtu anaenda kwenye kituo cha watoto yatima na kuku mweusi, kuku mweupe, nazi zilizo andikwa herufi za kishirikina etc.

Hizo nazi hutakiwa kuvunjwa na hao watoto yatima kulingana na maelekezo ya mganga. Kama mganga kaagiza nazi zivunjwe na watoto wa kiume au wa kike au both basi itakuwa hivyo.

Wengine wanaenda na dawa kapewa na mganga kwamba dawa inatakiwa kutwangwa na mtoto bikira. Anapewa binti wa miaka 12 kutwanga hiyo dawa.

Hili hata serikali mkitaka kulithibitisha ni kazi rahisi sana. Wewe nenda kwenye kituo cha kulelea watoto yatima ongea na mmiliki jifanyeunataka dawa yako itwangwe na mabinti let's say 7 wenye age 12 hadi 13, mtangazie dau hela kidogo, atakwambia kama unataka hata nywele zao utapewa..


Binafsi namchukia sana mtu anaetesa na kunyanyasa watoto.


Binadamu anatakiwa kuishi maisha yake to the fullest na nyakati pekee inayo weza Ku guarantee hili ni childhood.

Children need to live their child hood to the fullest.
 
Mtoa mada umekuja na tatizo hujaja na solution.
Kwanza nikupongeze kwa kulisemea hili, ni jambo baya kuwatumikisha mayatima na ni kuwaonea.
Kuombewa dua si jambo baya. Ila kuomba kwa style hiyo ya dua ndefu ni mateso kwa watoto.
Mtu kama ana cha kuwapelekea mayatima na awapelekee, wafurahi waenjoy, wale na kuvaa ikibidi. Kama una shida zako binafsi unahitaji kuombea basi ombea sadaka yako. Hili lina ruhusiwa, yaani unamuambia Mungu wako kuwa kwa matoleo haya kwa mayatima eeh Mungu nakuomba unitatulie hili na lile kabla hata hujafika huko kwa mayatima.
Na ukifika kule, waombe hao watoto wakuombee kwa Mungu wakati unaaga kuondoka ufanye nao maombi ya pamoja wao waishi vizuri nawe pia mambi yako yanyooke. Hii ni dua ya dakika 5.

Kuna imani kuwa dua za watoto hazikataliwi na Mungu na Mungu hachelewi kujibu. Kwa sababu watoto hawana makando kando ya dhambi, dhuluma n.k. So, the idea here is to pray through the children.....swali linakuja, ni wapi unawapata watoto wengi pamoja?
Ndio wengi hukimbilia huko vituoni.
Lakini kama unahitaji visomo virefu kama Yaasin 400, au Kursiyyu 1,000 ni heri ukaenda Madrassa, mwombe mwalimu wao na atafute wale wakubwa kidogo 10 yrs plus ukae nao chini wakusaidie na uwalipe. Zingatia neno kuwalipa. Hiyo sadaka yako ya pesa wape wao waile. Na mbuzi wale nyama pia.
Ahsante.
 
Back
Top Bottom