Mauaji yanatokea, watu wanapotea, wengine wanashambuliwa, wengine wanaokotwa baharini, shutuma zimetokea kuelekezwa upande wa CCM.
Hivi vyama vya upinzani mnaweza kuweka ushahidi unaokubalika kuwa CCM na serikali yake wanahusika?
Vyama ambayo mpaka imebakiza siku moja ndio wanaanze kupiga makelele kuhusu Tume huru ya Uchaguzi mlishindwa nini ndani ya miaka mitano kulianzisha na kulivalia njuga, wacheni kubabaisha raia.
Imebakia siku tatu mnabana pua Tume sio huru, miaka minne mmeufyata, wapiga kura wawaelewe vipi, hata kulizungumzia hamkusikika, siku zote hizo hamkulijua, au mtasema mlizuiwa mikutano.
Nikirudi na mada shinikizi kuhusu ushahidi,kama mna ushahidi na mahakama imetupilia mbali basi mnaweza kulipiza kisasi kisasi kinaruhusiwa kidini ila kusamehe ni bora zaidi.
Hata wakiengua wagombea wenu wa Urais mnaweza kulipiza kisasi, kama mmethibitisha haki haikutendeka, hivi akienguliwa Magufuli mtapinga au mtakesha kwa furaha?
Ili iwe fundisho kama mmethibitisha CCM ndio mambo yao na nyinyi lipizeni kisasi cha uhakika na ijulikane kuwa hapa kisasi kimelipizwa.
Kama mtaishia kupiga makelele bila kutoa funzo ili mheshimiane mtabakia, vyombo vya dola havitendi haki, polisi wanaipendelea CCM, usalama wapo na chama tawala, kama mna ushahidi pambaneni kwa kulipiza kisasi dhidi ya CCM, basi hata hivyo vyombo vikiona mambo yanageuka watawapendeni kama wanavyowapenda CCM.
.
[/QUOTE
ushahidi kamuulize NAPE kwanza