macho_mdiliko
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 21,804
- 39,621
Nani aliwadanganya watu mafukara hawafi kwa korona? Matajiri ni maarufu ndiyo maana watu wana-share habari zao. Hivi unadhani muuza mchicha au dagaa anayekaa Yombo Vituka akifa kwa korona watu wa sehemu nyingine za nchi watafahamu? Sana watu wa karibu na mtaa anaoishi, ndugu, jamaa na marafiki ndiyo watapashana habari. Korona ipo na maskini wanakufa tena kushinda matajiri ila habari zao zinaishia huko huko wanakokaa. Hivi huyu anayejadiliwa hapa unadhani kama angekuwa dereva wa daladala tungejua?Aisee inawezekana kabisa mkuu