Shehullohi
JF-Expert Member
- Jul 21, 2020
- 3,754
- 3,680
Wakifanya kosa wakaleta jina jipya na wasilete mwana ccm asilia na anaekubalika na Chama ccm mtampa Kaz kuongoza nchi Samia , chondechonde ,leten mtu anaekubalika ndani ya Chama na viongoz wengi wakiwemo wanachama apa nchi itakuwa kama mkeka.
Nao hao amboa mnasema hawakubaliki si CCM asili ndio ambao wameonesha ni viongozi bora tena kwa muda mfupi tu. Mkiwatoa kwenye uongozi kwa fitina ambayo ndio sifa ya wanao jiita CCM asili wawe na plan B.
Wala wasiogope JPM kesha warahisishia kwa kuwafungua macho Watanzania. Jeuri ya Viongozi Mafisadi wa CCM ni vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama ambavyo JPM amevigeuza mitazamo yake sana tu.
Unless kiongozi anafanya mambo ambayo ni mapenzi ya walio wengi hana nafasi tena Tanzania. Hivyo mafisadi na vibaraka wakiwaletea za kuleta ndani ya CCM tafutene kuwa tumikia Watanzania wenzenu nje ya CCM na mtaungwa mkono na walio wengi kwa uwazi na hata kwa kificho.