Wakuu nina ndugu yangu wa karibu ambaye ni mwanajeshi anasema taarifa za kulipuka kwa hayo mabomu zilijulikana tangu siku ya j'tatu . askari wa wadogo ambao ndiyo hasa walinzi wa hayo maghala waliona dalili za milipuko na wakatoa taarifa kwa wakubwa wao ,ambao nao wakatoa taarifa ngazi zinazofuata. akasema mpaka jumanne walikuwa bado hawajaambiwa ni nini cha kufanya na juma tano ikawa sikukuu hivyo walikuwa wanasubiri mpaka siku ya alhamisi ndipo waambiwe nini cha kufanya .
na pia kaniambia baada ya milipuko wanajeshi wengi wamekufa sababu waliambiwa waingie kwenye hayo maghara na wachukue hayo baadhi ya mabomu na wayaelekeze upande wa juu ili kuepusha madhara ya kulipua kambi nzima. japo hajaniambia ni idadi gani ya hao wapiganaji wetu waliopoteza maisha yao.
jamani urasimu huu mpaka lini ona unavyotugharimu mtu anapelekewa taarifa muhimu mara hayopo ofisini na taarifa zinabaki mezani kwake. kama habari hizi zinaukweli kazi tulionayo ni kubwa sana
na pia kaniambia baada ya milipuko wanajeshi wengi wamekufa sababu waliambiwa waingie kwenye hayo maghara na wachukue hayo baadhi ya mabomu na wayaelekeze upande wa juu ili kuepusha madhara ya kulipua kambi nzima. japo hajaniambia ni idadi gani ya hao wapiganaji wetu waliopoteza maisha yao.
jamani urasimu huu mpaka lini ona unavyotugharimu mtu anapelekewa taarifa muhimu mara hayopo ofisini na taarifa zinabaki mezani kwake. kama habari hizi zinaukweli kazi tulionayo ni kubwa sana