Mliooa mlipata wapi wake zenu?


vigezo vipo mkuu, ktk muda kiukweli ipo wazi, akipata afaae, maandaliz yanaanza
 

Dah! Sijui nikupe nini mtoto wee mweeeee umeongea point mpaka nimesisimka.
 
Ikifika siku Mungu atatuma malaika uitaona anakuonyesha huyu ndo mke wako.

Lakini wewe hutamuona malaika.





inawezekana anakupa wa kufanana na wewe, badilika uone.

Leo hii ukiniuliza nilimpataje mama Ngina hata sikumbuki...................... haya mambo huwa yanatokea Automatikale.

Ila kweli mkuu wanawake wengi nimcharuko lakini siyo wote wewe jitaidi kutafuta kanisani kwako na pia umuombe mungu
Nimesoma hizi comments hakika nimeona busara zenu, i hope kwa wale wote wanaosaka ndoa watanufaika na mashauri haya. Kila la kheri waJF
 
Nimefarijika sana na ushauri wenu.Thanks guys ngoja nami nijipange upya,possibly nilikuwa nakosea.
 
Dah! Sijui nikupe nini mtoto wee mweeeee umeongea point mpaka nimesisimka.

Sidhani kama unanyanyuka from nowhere unamtaka tuu mwanamke awe mkeo bila kuhakikisha kuwa anafikia kiwango kile unachotaka
Inawezekana umeweka elimu, kazi, sura, ucha Mungu wake na ni mwanamke wa aina gani unataka
Sana sana huwa hayo hayazingatiwi sana ila sidhani utanyanyuka tuu na kumvamia mwanamke yeyote utakayomuona na akakuvutia na ukamfanya mke
Mkuu nenda taratibu na kama nilivyokuambia Mke sio nyanya sokoni wala sio nguo dukani ila mke ni mtu wa muhimu sana kwako na ambaye utautumia muda mrefu sana wa maisha yako kuwa nae
Usiende papara wala usivamie kila mwanamke utakayemuona na ukadhania ni mke
Wanawake wako wengi lila mke ni mmoja tuu sasa issue inakuwa hapo kumpata huyo mmoja
Muombe Mungu na utulie katika kufanya chaguo lako
Achana na papara maana utaishia kupata mcharuko
 
Tatizo wanaume micharuko pia mnataka waliotulia. Tuliotulia wenyewe tupo wachache. Hebu oeni micharuko yenu hyo hyo.
 
Tatizo wanaume micharuko pia mnataka waliotulia. Tuliotulia wenyewe tupo wachache. Hebu oeni micharuko yenu hyo hyo.

Husninyo kweli hututakii mema kuoa mcharuko aise noma
Mwanaume mcharuko anaweza kutulia bana
 

Dear!
Kwa nyongeza katika ulochangia ni kwamba mtoa mada inabidi aache tabia zake mbaya.

Ukimu-aproach mwanamke kimzaa mtaishia kwenye mzaa. Ukiwa serious katika kumweleza nia yako naye atakuwa serious tu! Wanawake wana akili sana kuliko sisi wanaume; wanatusoma, wanatujadili - sisi wanaume hatuna mda wa kuwajadili - ndo maana wanatu-handle.

Najibu swali la mtoa mada....
Mlioooa mlipata wapi wake zenu?

Wa kwangu nilimpata siku alipokuja dukani kwa kaka yangu kufanya shoping; nikamjengea ukaribu - hadi akawa rafiki wa familia yetu na mwisho nikamtamkia kuwa nataka kuwa naye maishani - hakusita. Inataka muda kumteka mawazo mtoto wa kike. Vijana wa siku hizi wanakurupuka kuomba tendo la ndoa, wanachokana mapema na kutimuana. Pengine ni malezi mabaya; kwetu sisi tuliolelewa katika mazingira kiroho tunakuwa na woga sana - si kwamba tunawaogopa wanawake; la hasha - tunamwogopa Mungu.
 
Hivi kuna aina ngapi za wanawake?Halafu kumbe kuna vipezo vya kumpata mwanamke!Inawezekana ndo maana wanawake wanashindwa kuolewa!Watu wanatoa vigezo kama vile anaweka oda ya gari kwenye kiwanda!Wanawake kazi mnayo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…