Mlioko mbeya tusaidieni ufafanuzi juu ya Mtoto alielawitiwa huko na taarifa zikamfikia mkuu je ni igizo au ni taarifa za kweli?

stella1975

JF-Expert Member
Nov 25, 2018
870
1,249
Moja ya mikutano ya mkuu wa nchi huko mbeya alijitokeza mama mmoja akidai kuwa Mtoto wake alilawitiwa na mtu mmoja huko, Halafu mtu huyo hajachukuliwa hatua yoyote, kitu ambacho kimemfanya mama huyo kuomba msaaada kwenye taasisi zinazohusika pasipo kupata msaaada na kuomba mkuu wa nchi kusaidia ili mama apate haki, suala ambalo mkuu wa nchi aliamua kulifuatilia, Lakini baada ya mkuu kufuatilia inasemekana kuwa wamepewa majibu kuwa mtuhumiwa alishafungwa kifungo cha maisha, sasa je hili ni IGIZO au ni suala la kweli? Na Kama ni kweli ilikuwaje huyo mama akashindwa kujua kuwa mtuhumiwa alishafungwa? Na huyo mtuhumiwa ni Nani na anafanya shughuli gani?
 
Moja ya mikutano ya mkuu wa nchi huko mbeya alijitokeza mama mmoja akidai kuwa Mtoto wake alilawitiwa na mtu mmoja huko, Halafu mtu huyo hajachukuliwa hatua yoyote, kitu ambacho kimemfanya mama huyo kuomba msaaada kwenye taasisi zinazohusika pasipo kupata msaaada na kuomba mkuu wa nchi kusaidia ili mama apate haki, suala ambalo mkuu wa nchi aliamua kulifuatilia, Lakini baada ya mkuu kufuatilia inasemekana kuwa wamepewa majibu kuwa mtuhumiwa alishafungwa kifungo cha maisha, sasa je hili ni IGIZO au ni suala la kweli? Na Kama ni kweli ilikuwaje huyo mama akashindwa kujua kuwa mtuhumiwa alishafungwa? Na huyo mtuhumiwa ni Nani na anafanya shughuli gani?
Wenyeji wanasema anacholalamikia yule mama ni haki za mtoto ikiwa ni pamoja na matibabu,kwenda shule na mahitaji mengine muhimu! Inaonekana ni Kama mama huyo hakujua sehem anayotakiwa kwenda kwa ajili ya kupata msaada huo ndio maana anasema alienda kwa jaji mkuu,IGP na vituo vya polisi ambavyo sometimes huwa wanamuweka ndani kwa kuona amekuwa msumbufu!
 
Back
Top Bottom