dada faizafoxy umenena, hayo wachina wanayafanya kweli, na wahujumu uchumi wote wanaangamizwa, lakini hapa, sijui. Wakati tukitafakari kama wahujumu uchumi kama ekelege wanaweza kuangamizwa, ebu tujikumbushe kidogo sakata hili: Makamu mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za mashirika ya umma (pac), deo filikunjombe amemshutumu mkurugenzi mkuu wa shirika la viwango tanzania (tbs) charles ekelege kwa utendaji wake mbovu, uliojaa utapeli ambao kamati hiyo iliugundua katika ziara nje ya nchi ya kukagua kampuni za ukaguzi wa magari yanayoingizwa nchini. Filikunjombe alikuwa anazungumza hayo katika kikao cha kamati za bunge za hesabu za serikali (poac) na pac cha kujadili utendaji wa wizara ya viwanda na biashara, dar es salaam. Naye mbunge lugora akielezea kikao hicho jinsi alivyoakasirishwa na ubabaishaji wa ekelega, na kuamua kumrushia konde ambalo ( kwa bahati mbaya) lilidakwa na filikunjombe wakiwa ughaibuni baada kamati kupewa sumu feki ya kampuni ya nje inayokagua magari yanayoingizwa nchini. Picha hapa chini ni muonekano wa ekelege kama vile anataka kulia au kuigiza ze komedi katika kikao hicho (picha ya 1 na 2) na mbunge lugora (picha ya 2) na makamu mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za mashirika ya umma (pac), deo filikunjombe (picha ya 4).
View attachment 46278View attachment 46279View attachment 46280View attachment 46281 source:
http://kingkif.blogspot.com/2012/01