Mlimani Tv na Tambwe Hizza

Mzito Kabwela

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
18,857
7,618
Leo asubuhi nilibahatika kuyaona mahojiano live kati ya Mlimani TV na Mzee wa Propaganda Tambwe Hizza. Pamoja na kukosoa uendeshaji mbovu wa kipindi kile kilichoongozwa na kijana niliyemtafsiri kama inexperienced person in that particular field bado pia Stesheni hii ya wasomi ina safari ndefu hasa kwenye oganaizesheni yake.

Maudhui ya kipindi yalikuwa ni Miaka 48 ya Uhuru wa Tanzania bara. Nilitegemea wangewaita watu ambao wako politically neutrally biased ili wachambue mustakabali wa Taifa hili bila kuegemea upande wowote mf TAMWA,TGNP na wengineo, au kama ni wanasiasa basi wangewaleta wa CCM na wanaoipinga CCM ili kuballance story. Wao kwa busara zao wakamleta Tambwe.Jamaa akaanza kupiga siasa...Hakika ni mzee wa propaganda na jukwaa alilitumiavizuri sana. Sasa haya ni baadhi tu ya yale aliyoyasema na nawaomba ndugu zangu tuyajadili aliyoyazungumza Tambwe.

1.Wanaoikosoa Serikali ya awamu ya nne ni WALEVI

2.Kuna maendeleo sana Tanzania tangu JK aingie madarakani kwa kuwa kina mama sasa hivi wanaendesha magari (akatoa statistics) kwenye magari miamoja yanayopita barabarani, 40 yanaendeshwa na kina mama.

3.Yapo maendeleo vijijini mfano alienda Busanda akakuta nyumba nzuri sana ya Block juu ina ungo... ni CCM hiyo sio wapinzani

4. Tangu aingie JK vyuo vimeongezeka sasa hivi ni 33 na enrollment imeshoot sana, almost wanafunzi 93,000 wanasomea digrii

4. Kuna lami nchi nzima, lami hadi ifakara na nachingwea

5.Watanzania wamewezeshwa, ukiona basi linatembea au duka ujue ni la mtanzania mweusi tofauti na zamani ambapo raslimali hizo zilikuwa za waarabu au wahindi

6. Hakuna kama CCM

Nawasilisha.
 
huyo jamaa hana upeo kabisa, ni kibuyu cha maana tu, anaongea vitu vya kufikirika
 
....

.........Sasa haya ni baadhi tu ya yale aliyoyasema na nawaomba ndugu zangu tuyajadili aliyoyazungumza Tambwe.

1.Wanaoikosoa Serikali ya awamu ya nne ni WALEVI


Nawasilisha.

Siyo WEHU (kama alivyosema Makamba)?

Hapo labda CCM walinunua/lipia kipindi. Ila nadhani wengi wetu hatuwezi kupoteza muda wake kuangalia mharo kama huo
 
siyo wehu (kama alivyosema makamba)?

Hapo labda ccm walinunua/lipia kipindi. Ila nadhani wengi wetu hatuwezi kupoteza muda wake kuangalia mharo kama huo


tena ni uharo wa makande yaliyochacha
 
wana JF naomba kama kuna mwenye CV ya Tambwe Hizza atuwekee humu ndani yawezekana kaungonjwa ni kale kale.......
 
huyu jamaa anajitahidi kupropaganda!duh,yaani bila jk wanawake wasingeendesha magari.inakera sana!hasa ukiwa umeona maendeleo wanayofanya wenzetu kama wachina!kuna wachina walikuja hapa home tz wakagoma kuamini kuwa nchi hii ina serikali,maana kila kitu tambarare hapa ila akina tambwe hawaoni wanatamba tu...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom