- Source #1
- View Source #1
Inadaiwa baada ya kupoa kwa muda mrefu, Volkano ya Mlima Ol Doinyo Lengai imeanza tena kulipuka. Suala hili linaweza kuwa hatari kwa afya ya umma hivyo wananchi wachukue tahadhari.
- Tunachokijua
- Mlima Ol Doinyo Lengai una maana ya kuwa "Mlima wa Mungu" na mlima unaochukuliwa kama mlima mtakatifu miongoni mwa Wamasai. Mlima huu una asili ya kulipuka na umeshawahi kulipuka katika vipindi tofauti.
Madai
Kumekuwa na Taarifa kuanzia Januari 08, 2026 kuwa mlima Oldonyo Lengai umeanza kulipuka na kwa mara ya mwisho ilikuwa ni mwaka 2008.
Uhalisia wa Taarifa hiyo ni upi?
JamiiCheck imefuatilia taarifa hiyo kuhusu kuliuka kwa mlima Oldonyo na kubaini kuwa Taarifa hizo si za kweli.
Ufuatiliaji umebaini kuwa hakukua na chanzo chochote cha kuaminika kilichochapisha taarifa hizo na kufanya JamiiCheck ifuatilie zaidi.
Kupitia kwa mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Brigedia Jenerali Wilson Sakulo ameeleza kuwa
Taarifa hizo za Mlima Ol Doinyo Lengai kulipuka sio za kweli