Mlegezo/kata k.

Mbangubangu

Senior Member
Joined
May 6, 2013
Posts
188
Reaction score
70
kuna tabia naona inakuwa kwa kasi kubwa sana na hii ni uvaaji wa suruali katikati ya makalio kwa vijana wa kiume.hii ni fashion za kuonyesha boxer? au ni tabia za kuiga?coz sio kwa wanamuziki na vijana wa mitaani tuu, hata vijana kwenye maofisi siku hizi suruali zafungiwa kati ya makalio.
 
Barack Obama, akizungumza na
kituo cha MTV kabla ya uchaguzi wa
mwaka 2008, alisema sheria zinazopiga
marufuku uvaaji wa suruali za mlegezo
zilikuwa sawa na kupoteza muda, lakini
alifuatisha matamshi hayo na: "Baada ya
kusema hayo, kina kaka laazima
wapandishe suruali zao. Unatembea
sambamba na mama yako, na bibi yako,
chupi yako inaonekana, tatizo ni nini?
Baadhi ya watu hawapendi kuona chupi
yako.
 
Fashen tu na sifa za kijinga....itakuja itapita itakuja nyingine pia itapita! kama vile wanaume walivyoanza kusuka,kuvaa eleni...kata k, na sasa kata k ya mtindo wa kuacha boxer nje.. basi mbwembwe tu za kidunia japo zinamadhara yake kimaadili
 
Fanya mambo yako.. Mafisadi mmewashindwa wahindi wanaketwa kila siku kuja kuajiriwa hapa nchini mmenyamaza ila unafuatilia mlegezo.. Unakuhusu?
 
Ni noumer! tutajuaje kama wanavaa chupi na boxer jamani? Huu ni ulimbukeni haswa maana tunafahamu wazi kwamba mvulana amevaa suruali lakini ndani kuna chochote (ndo maana zinaitwa nguo za ndani) aliyewaambia tunahitaji kuona michupi na miboxer yao nani??? hebu waache hizo bana wanakera. Utakuta konda wa daladala nae kashusha mlege bab kubwa ukicheki bukta / boxer alovaa utaomba amani! chafuuu hadi sura yake halisi imepotea... usiseme tena muharufu unaotoka duh.....

Lakini kuna tetezi eti kizazi cha digitali ukivaa vile ndo unavutia sijui wadau mtasemaje. Ladies wakiona men kapiga mlege basi wanaanza kutengeneza mazingira. Ni kama mbadala wa kutongozea nowdays....
 
Tuende mbele zaid mlegezo ni kero na si kwa wanaume tu kuonyesha boxer zao, saivi wanawake ndo wanaongoza kwa hii style..utakuta mdada kavaa jeans mlegezo ma.t.a.k.o waz kama nyan unaona ka kamba tu cha bikin kinapotelea mtaron. Inakera sana.
 
kuna wakati kata k ni stage tu! na kuna wakati ni fixation kwa wale ambao hawakukata k' enzi za ujana(esp.foolish age).
 
Its high level of imaturity...sema sisi vijana wakitanzania tunaiga tu hauelewi...mtu anaevaa mlegezo ukiangalia hatua zake za ukuaji(developmental milestone) utakuta kuna kasoro flan hivi...
 
Ni fasheni tu wakikua wataacha
ilikuwepo zama zetu na lazima bega moja liwe juu kuipita shingo na liguse shavu la kushoto, halafu lazima uvute mguu wa kulia yaani uwe nyuma kila hatua kuliko wa kushoto TUMEACHA
bado hamjavaa Bugaloo, Tina Bull Raizon (raise on)
hizo ni mipito tu ya wakati na itaisha
 
ya Ngoswe hayo...but katabia ako hakajaanza leo mbn!!!
 

tatizo mmezidi kutuandama vijana,hiyo ni style tu,itafika siku itapotea.Mbona mtu akivalia suruali tumboni(maarufu kama bag)hamumsemi?,kwan nyie mnawaona wanaume tu,je hao wasichana na mi mama mijitu mizima inayova nusu uchi hamuwaoni?
 
aliyeleta hilo balaa ni tupac shakur RIP.

Alafu hii tabia ilikuwepo miaka ya 80 mwishoni kabisa enzi tupo watoto mzazi akikununulia chupi, unatembea kifua wazi alafu suruali inashuka chini kiaina kuonyesha umepiga kitu kipya (but ilikuwa kwa watoto enzi za kombolela lakini siku hizi kila mtu anapiga kata K)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…