happiness win
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 2,461
- 1,384
Nimewasikia Akinamama waliokuja kumfariji shangazi yangu baada ya mume wake kutafuta nyumba ndogo na kuelekeza nguvu zote huko wakimfariji na kumwambia kila jaribu lina mlango wake wa kutokea, jipe moyo Mungu atakusaidia Sasa najiuliza, vipi kuhusu mlango wa kuingilia? Wamama hawa wanazijua fika tabia za ugonvi, uvivu, umbeya na nyingine nyingi alizonazo Shangazi yangu. Sasa iweje leo wanapoteza nguvu kwa kukesha, kulia na kuomba kutafuta mlango wa kumtoa Shangazi kwenye majaribu! Kwa nini hawakumtahadharisha Shangazi kufunga mlango wa kuingilia kwenye hayo majaribu?
Wewe unaonaje kuhusu hili?
Wewe unaonaje kuhusu hili?