Mkuu wangu wa Idara, ananikosesha amani kazini

Mkuu wangu wa Idara, ananikosesha amani kazini

Latoya

JF-Expert Member
Joined
Apr 18, 2013
Posts
660
Reaction score
457
Habari wanabodi,

Mimi ni mtumishi wa umma, idarani kwetu tumebahatika kupata mkuu mpya yapata mwaka sasa.Tatizo la boss huyu anasikiliza maneno ya majungu ya watumishi wenzangu, yani akisikia shutuma kukuhusu hafanyi uchunguzi,anaziamini direct na kuanza kukuongelea vibaya kwenye vikao na kwa wafanyakazi wengine.

Binafsi nimekuwa muhanga wake baada ya wanoko kumpelekea maneno kunihusu,basi sina amani kazini,anaishia kunizungumzia vibaya kwa watendaji wenzangu.

Tabia hii nimeipuuzia kwa muda ila naona kadri siku zinavyosonga naanza kuichukia ofisi na kutotamani hata kufika kazini.Suala la bajeti ya idara ameliacha kwa watumishi wachache wanao jiandikia posho afu watumishi wengine tunawekwa kando.

Niliwahi kumuomba kiasi fulani cha matumizi ya internet kwaajili ya mfumo wa idara akanitoa resi ofisini kwake,ila kwa fungu hilohilo nililoomba nipewe kiasi cha mtandao walikomba watu wengine tena bila kufanya lolote ila iliporudi hoja ya matumizi ya pesa hizo akaning'ang'aniza mie nijibu.

Kuna mengi ambayo siwezi yaanika hapa, naomba ushauri wenu nifanyeje??kwani nafikiria kuhama kituo cha kazi.
 
Duh,ni shida!Ni halmashauri ya wilaya?Au shirika la Umma?
 
Woga wako ndio kuonewa kwako.

Mkalishe chini mpe ukweli.

Hii sii karne ya kuendekeza ujinga..haswa kwa hela ambazo ni kodi ya wananchi
 
acha kazi..ndo suluhu pekee!! kwanini watu mnapenda sana utumwa??
 
Hii hali hata mimi inanitokea ofisini , ikitokea semina inayoniusu anapewa mwingine, kwenye kikao ukitoa wazo linakataliwa lakin hilo wazo likitolewa na mtu mwingine linakubaliwa, tatizo langu mimi huwa mamwambia ukweli, sasa najiandaa kujiajili siwezi fanya kazi katika mazingira haya
 
Umeipata Nafasi Hy Kwa Fadhila? Unavyeti Vya Mashaka? Kama Jibu Ndiyo Kwa Mojawapo Ya Maswali Hayo Basi Huna Haki We Kubali Kuonewa. Lakini Kama Jibu Hapana Kwa Maswali Hayo Basi Tambua Kuwa Mkuu Wako Wa Idara Siyo Bosi Wako Wa Mwisho. Kwanini Usimshitaki Kwa Mkurugenzi Mtendaji?
 
Mabosi kama hao wapo wengi tu, cha muhimu mlie-timing akijilengesha tu...............
 
Muachie Mungu, na endelea kuvumilia mpaka mwisho

Huyo boss siyo pepo wa kuachiwa Mungu, mtumishi anatakiwa ajue haki zake na azidai. Km kweli huhusiki na hizo tuhuma basi ongea na mtu wa rasilimali watu au utawala ili mmalize huko kutoelewana.
 
Muokozi magufuli kaja ngoja aapishwe

Tutakuwa tunajidanganya sana, saa ngapi wewe kapuku lofa mkubwa uje ukutane na Magufuli? Naye tutamshangaa kama atakuwa anashughulika na watu wa chini kabisa huku utafikri hana majukumu mengine!
 
Dawa yake huyo ni ndoogo mno

kila kitu tumia email
akikujibu vibaya unazi forward kwa wakubwa wake
shutuma zote muulize kwa email ili akujibu ajiingize mkenge
we kazi yako ni kuzi cc emails kwa wakubwa wake au unazi forward
anapokujibu hovyo....

ukifanya mara mbili tu hatarudia
 
Back
Top Bottom