Mkuu wa utumishi jeshini aongea na waandishi wa habari kuhusu upotoshaji wa ajira JKT na JWTZ

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287


Jeshi la ulinzi wa wananchi Tanzania limefanya mkutano na waandishi na kutoa tahadhari juu ya matangazo yanayodai kuna nafasi za kujiunga JKT au JWTZ.

Amesema kuanzia leo mtu akimfuata nakumuambia kuna mafunzo ya kujiunga na JKT au jeshi la ulinzi wa wananchi mtu huyo atakuwa ni tapeli,

Amesema jeshi haliwezi kuchukua watu mtaani kiholela na sasa utaratibu wa majeshi yote ni ikiwemo Zimamoto, Tanapa, Uhamiaji, ,Magereza, Polisi, na Jeshi la Ulinzi kunakuwa na kikao cha utumishi jeshini kwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, na vyombo vyote huleta idadi ya watu wanaowahitaji kuwaajiri kisha majina kuchukuliwa na mkuu wa utumishi jeshini na kuyapeleka kwa mkuu wa jeshi la kujenga taifa.

Mkuu wa jeshi la kujenga taifa anaratibu utaratibu wa vyombo vya ulinzi na usalama kwenda kwenye makambi ya JKT vyombo hivyo kwenda kuchukua vijana wanaohitajika na mkuu wa jeshi la kujenge taifa upotoshaji

Utaratibu wa kujiunga na JKT ni mpaka mkuu wa JKT atoe taarifa kupitia vyombo vya habari na kutoa utaratibu unaotakiwa kufuatwa.

Utaratibu wa kujiunga na JKT huanzia kwenye vijiji, kata tarafa kisha kufikia ngazi ya wilaya na majina kuchujwa na kupelekwa baadae kwenda mkoani kisha kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huwachuja na watakaofaulu hupewa fomu ya kujaza.
 
Wamefanya vizuri,lakini pia jkt wawe wawazi zaidi wanapotangaza nafasi za kujiunga huko,Kwan uhaba WA matangazo hayo ndio unaosababisha baadhi ya wajanja kubuni utapeli sababu hakuna taharifa za kutosha za kuwepo kwa usahili WA kujiunga jkt
 
Wamefanya vizuri,lakini pia jkt wawe wawazi zaidi wanapotangaza nafasi za kujiunga huko,Kwan uhaba WA matangazo hayo ndio unaosababisha baadhi ya wajanja kubuni utapeli sababu hakuna taharifa za kutosha za kuwepo kwa usahili WA kujiunga jkt
Amedai mchakato huanzia vijijini, kata, tarafa hata uliyekosa kupata habari utajua tu kamani mfuatiliaji
 
Kumbe siku hizi kupata nafasi JKT ni dili, sisi miaka yetu tulikuwa tunakimbia JKT
 
Jeshi la Wananchi wa Tanzania, wametoa tahadhari kwa vijana na walezi, juu ya uwepo wa vikundi vya matapeli wanaodanganya umma kuwa wanao uwezo wa kuwatafutia nafasi za kuingia katika vyombo hivyo vya ulinzi na usalama.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Utumishi JWTZ, Meja Harison Meja Joseph Masebo amesema, utaratibu wa kuajiri kwa vyombo hivyo uko wazi na kuwashauri wenye uhitaji kufuata taratibu hizo.

18953530_852363591596550_3573754841310365234_o.jpg


Amewataka watanzania kufahamu kuwa vyombo hivyo vya usalama, akimaanisha Uhamiaji, Zimamoto, JKT, Magereza na vinginevyo hutumia taratibu zinazofanana katika kuajiri zikiwemo vikao vya pamoja, uwasilishaji majina na kuyapitia, sanjari na kuitwa katika usaili ambao huangaliwa vigezo muhimu kulingana na taasisi husika inavyohitaji.

Hayo yamejiri kufuatia hivi karibuni kuibuka makundi ya matapeli wanaojiita maofisa wa jeshi wanaodaiwa kuwatapeli wazazi na vijana kwa lengo la kuwapatia kazi jeshini.


ice_screenshot_20170607-123542.png
 
Daaa ngoja tuu subir mana kama mm napenda sana kwenda jkt mungu bariki watoe tangazo mapema
 
Amedai mchakato huanzia vijijini, kata, tarafa hata uliyekosa kupata habari utajua tu kamani mfuatiliaji
Mkuu ili ujue ni mpaka uwe mfatiliaji kwelikweli Yan Ile ya mtu mwenye shida hasa,ni vizur hii kitu ikafahamika kwa uwazi zaidi maana usiri uliopo husababisha wengi kukosa fulsa na wapiga dili kutumia nafasi hiyo.
 
Kwahiyo hakuna kujiunga na jeshi lolote bila kupita JKT? Hii safi sana ...maana yake kila askari wa majeshi yote atakuwa na basic military training ...
 
Back
Top Bottom