Responded Mkuu wa Mkoa Mwanza asema anafuatilia madai ya ukiukwaji wa udahili katika Shule ya Nyanza

Responded Mkuu wa Mkoa Mwanza asema anafuatilia madai ya ukiukwaji wa udahili katika Shule ya Nyanza

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda amesema anafuatilia madai kuwa kuna taarifa za Shule ya Msingi Nyanga English Medium kukiuka taratibu za udahili na kwamba kuna mazingira ya kupeana nafasi ya Mwanafunzi kusoma hapo kwa njia ya “kujuana”.

Kusoma hoja ya awali, bofya hapa ~ Kuna mazingira ya ukiukwaji wa taratibu za udahili kwa Shule ya Nyanza English Medium (Mwanza)

RC Mtanda amesema hayo katika taarifa ya Mwanachama wa JamiiForums.com iliyochapishwa kwenye Ukurasa wa Instagram ambapo amesema “Nitafuatilia ukweli wa suala hili, tutatoa taarifa” wakati akimjibu Mwananchi mwingine ambaye alihoji kuhusu suala hilo kwenye sehemu ya maoni.

Wakati huohuo, Mwananchi mwingine naye akatoa maoni yake katika ukurasa huo kwa kuandika:

“Hili halina ubishi mimi mwenyewe nilienda ilikuwa siku ya Alhamis nikaambiwa muda wa kuchukua form umeisha jana yake, cha kushangaza baada kama ya wiki mbili jirani yangu akaniuliza nikamwambia walisema nilichelewa lakini kwake ikawa tofauti.

“Akasema yeye alienda akaambiwa aende Jumatatu ya wiki inayofuata, kilichofuata mwanaye anasoma hapo hadi leo licha ya kuwa alichelewa wiki mbili ila mimi nilipishana siku moja tu nikaambiwa nafasi zimejaa.”
 
Hii inaonyesha fursa ya kuanzisha na kupiga pesa kwenye hii biashara ipo juu sana Mwanza , hawana competition ndio maana wanafanya mambo ya kipuuzi
 
Back
Top Bottom