ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,026
- 49,670
Mkuu wa Mkoa wa DSM Albert Chalamila amesema ni aibu Kumsumbua Waziri Mkuu kuja kutatua Changamoto wakati yeye Mkuu wa Mkoa Yupo.
Chalamila ameahidi kwamba Hilo halitajitokeza tena
=====
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila amesema ni aibu kumsumbua Waziri Mkuu kuja kusikiliza kero za wafanyabiashara wakati yeye Mkuu wa mkoa yupo huku akiahidi sasa itakuwa ni mwisho kutokea jambo hilo
Akizungumza na wafanyabiashara wa Kariakoo wakati akimkaribisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, RC Chalamila amesema ofisi yake itakuwa wazi muda wote huku akisema anafahamu wazi kuwa kuna mahalui wafanyabiashara wanakanyagwa kiatu na atafanyia kazi suala hilo
“Nawathibitishia Ofisi ya RC itakuwa wazi, nafahamu Wafanyabiashara kuna mahali mnakanyagwa kiatu na Mimi kama RC itakuwa mara ya mwisho kuja kikao ambacho kina Waziri Mkuu wangu maana itakuwa aibu RC kumsumbua Waziri Mkuu afike na Mimi nipo maana yake nitakuwa sitaki kazi ya Ukuu wa Mkoa wa Dar es salaam” amesema RC Chalamila
Chalamila ameahidi kwamba Hilo halitajitokeza tena
=====
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila amesema ni aibu kumsumbua Waziri Mkuu kuja kusikiliza kero za wafanyabiashara wakati yeye Mkuu wa mkoa yupo huku akiahidi sasa itakuwa ni mwisho kutokea jambo hilo
Akizungumza na wafanyabiashara wa Kariakoo wakati akimkaribisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, RC Chalamila amesema ofisi yake itakuwa wazi muda wote huku akisema anafahamu wazi kuwa kuna mahalui wafanyabiashara wanakanyagwa kiatu na atafanyia kazi suala hilo
“Nawathibitishia Ofisi ya RC itakuwa wazi, nafahamu Wafanyabiashara kuna mahali mnakanyagwa kiatu na Mimi kama RC itakuwa mara ya mwisho kuja kikao ambacho kina Waziri Mkuu wangu maana itakuwa aibu RC kumsumbua Waziri Mkuu afike na Mimi nipo maana yake nitakuwa sitaki kazi ya Ukuu wa Mkoa wa Dar es salaam” amesema RC Chalamila