southernboy
JF-Expert Member
- Sep 27, 2015
- 826
- 1,017
Habari wakuu. Yaani kuna muda unaweza kysikia habari mbaya lakini kutokana hali yako ya maisha unatamani hiyo habari iwe heri kwako,Mimi binafsi nilipitia jkt kujitolea miaka mitatu 2019 hadi 2022 ,Lakini mazingira niliyo pitia ya kuona wenzetu njia walizopitia kuajiriwa na mimi sikuwa na konection yoyote ile ,Sahizi nipo napambana mtaani Dodoma Siwazii sana Majeshi lakini hata kazi za kubeba zege tuu nazo huku mtaani bila connection hipati, Siku ile mkuu wa majeshi alivyosema kuwa kuna vijana wanasafirishwa kwenda kujiunga na vikundi nilitamani sana kama na mimi ningepata hiyo connection niachane na haya maisha.