Ushauri wangu kwa vijana wanaotaka kufanya kazi za majeshi kupitia JKT

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Oct 6, 2016
10,206
12,747
Kichwa Cha habari kipo wazi sana Kama kinavyojieleza NALIA NGWENA nimeamua kutoa ushauri/ronja kwa vijana wenye ndoto yakufanya kazi za majeshi kupitia JKT/Nini Cha kufanya ukiwa mtaani kipindi unafukuzia nafasi za jkt.

Fanya hivi/chunga hivi /usifanye haya unapokua mtaani na una ndoto za majeshi I'll isilete usumbufu katika usajili.

Mosi, usichore tatoo katika mwili wako, Kuna kasumba vijana wengi wanapata nafasi ya kujiunga na jeshi lakini kwenye usahili anangushwa na tatoo alizozichora mwilini mwake.

Usithubutu kuchora tatoo ya Aina yoyote katika mwili wako.

Pili, usishiriki Mapenzi ya jinsia moja(mtoto wa kiume Linda Malinda Kama Mali) kazi za majeshi mtoto wa kiume lazima ugangamale Sasa ukiwa mtepeto (huna Malinda ) huwezi kufanya kazi za majeshi

Kuna upimaji maalumu utabainika tu Kama hiyo ni michezo yako.

Tatu,Linda damu yako ya mwili isipatwe na maambukizi ya virusi Kama virusi vya ukimwi,
Damu ni silaha kubwa sana kwa kijana mwenye ndoto na kazi za majeshi, jeshi linataka watu fiti tofauti na hapo ni unfit.

Nne, uaijiingize kwenye matumizi ya madawa ya kulevya
Kijana pigania ndoto zako ufike unapopataka achana na madawa ya kulevya ni adui mkubwa wa ndoa.

Tano, fanya mazoezi ya nyumbani/pasha mwili wako ili utakapofika huko mwili usishangae kabisa uendeleze pale ulipo ishia

Ya mwisho andaa documents zako mapema weka kabatini ukisikia milio ni kuamka nakutembea faster.

Kijana mpambanaji, I wish you all the best and high spirits of hard fighting.

NB: NIMETOA USHAURI TU KWA VIJANA USIJE INBOX KUNIOMBA CONNECTION.



Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kutunza afya ni muhimu sana mzee.

Inauma sana unapiganisha then unapata nafasi afu kwa bahati mbaya unakua UNFIT.
 
Back
Top Bottom