Mangaline
JF-Expert Member
- May 19, 2012
- 1,045
- 221
Katika hali isiyo ya kawaida, madaktari wameamua wao wenyewe, kuwa walinzi wa kamanda wao dr. uli. Hali hii inamaanisha kuwa madaktari hawa, hawana imani na jeshi la polisi, kwani hawaamini kuwa ulinzi wa polisi, waweza kuwa salama kwa kamanda wao. Kukosekana kwa imani ya madaktari kwa chombo halali cha usalama wa raia, kinazidi kujenga chuki kati ya makundi haya mawili. wakati huo huo, jeshi la polisi, linaendelea kuwa chombo cha dola cha kupiga, kunyanyasa, na kutesa raia.
Hali hii, inaweza kupelekea madaktari kutumia taaluma yao katika vita hii chafu. Hali ikifikia hapo, nchi inakosa uhalali wa kuwa dola.
WAZO LANGU:-
Mheshimiwa mkuu wa kaya, katika hali hii, iko haja ya kuvunja ukimya, utoe sauti angalau ya kupoza machungu ya jamii, la sivyo, magumu yakitokea, mimi na wewe, hatucheka wala kufurahia matokeo yake. Tafadhali mkuu, funguka.
"MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBARI, RIP TANZANIA"
Hali hii, inaweza kupelekea madaktari kutumia taaluma yao katika vita hii chafu. Hali ikifikia hapo, nchi inakosa uhalali wa kuwa dola.
WAZO LANGU:-
Mheshimiwa mkuu wa kaya, katika hali hii, iko haja ya kuvunja ukimya, utoe sauti angalau ya kupoza machungu ya jamii, la sivyo, magumu yakitokea, mimi na wewe, hatucheka wala kufurahia matokeo yake. Tafadhali mkuu, funguka.
"MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBARI, RIP TANZANIA"