ISMAIL MKIMBIZI
Senior Member
- Jan 13, 2013
- 192
- 23
Wakuu,taarifa za kusikitisha ni kwamba Mkutano wa Dr.slaa umevunjika Kasulu,amepigwa mawee na vijana wasiojulikana akiwa Jukwaani,Polisi wanapiga mabomu ya Machozi Muda huu kutawanya watu,haijulikani Slaa ameumizwa kiasi gani lakini polisi wamewahi kumuokoa na kumtorosha kusikojulikana.
hali ni tete wakuu,naomba Munipe muda wa kuwawekea Picha hapa.
Pia awali Mkutano ukiwa unaendelea,Waitara ambaye ni Mkurugenzi wa CHADEMA alitangaza kuwa Matamko na mambo mengine yote ya kumtibulia Dr.slaa yanaratibiwa na Kijana Habib Mchange na Diwani mmoja wa Mwanza(Hakutaja jina).
MODS naamini mnawatu KASULU,wapigieni simu MUDA huu,Mpigieni Tumaini Makene mjue Ukweli huu.naomba muiache Post watu wachangie
Moja ya bango Mkutano wa slaa kasulu kabla haujavunjika
Umati wa wananchi waliokusanyika kumsikiliza Katibu Mkuu, Dkt. Slaa leo mjini Kasulu Uwanja wa Kiganamo. Hapa ilikuwa kabla ya vijana wapatao 10-15 hivi kurusha mawe, baada ya wananchi kuwafukuza wakitaka kuwapiga, wakipinga kitendo cha vijana hao kupiga kelele ili mkutano usiendelee.
Mbinu ya kuhakikisha mkutano hauendelei kisha itokee vurugu, ambayo ingefuatiwa na mabomu ya machozi ili kujustify headlines ambazo tayari zimeshaandaliwa kuwa ''Dkt. Slaa aokolewa kwa mabomu...Dkt. Slaa ashindwa kuhutubia, Polisi wamwokoa Dkt. Slaa n.k', ilipangwa kutumika leo baada ya Dkt. Slaa kufanikiwa sana ku-counter issue ya vijana na mabango kwa kuwapatia fursa ya kukaa mbele katika mikutano iliyopita.
Tutawaletea maelezo ya kutosha juu ya mpango huo na mwingine unaoendelea kupangwa kwa ajili ya kufanyika Kigoma mjini na maeneo mengine. Tutajibu maswali na hoja za watu kuhusu tukio la leo.
kime stink mbaya
mtei baba mwenye nyumba
mbowe mtoto wa mwenye nyumba
slaa mpangaji
lissu mchumia tumbo ha ha ha
lema ni nani??
Khali ni mbaya kwa doctor Slaa baada ya wananchi wa Kasulu kumshusha kwa mawe jukwaani
viongozi mbalimbali wa CHADEMA wakiwamo Shaban Mambo Mwenyekiti wa chadema Kanda ya magharibi na Rajabu Bujoro Mwenyekiti wa Kasulu wamefungua mkutano hali ikiwa shwari watu wa Kasulu wakionesha ustaarabu wa hali ya juu. Lakini kufumba na kufumbua alipopanda jukwaani Dr Slaa Katibu mkuu wa CHADEMA Taifa kikundi cha watu kiliibuka na mabango mbalimbali huku wakitamka kwa jazba maneno mbalimbali ya kumtaka Zitto na kukejeli upngozi wa juu wa CHADEMA.
Katibu Mkuu ameonesha ustaarabu na demokrasia iliyokomaa alipo ruhusu mabango yasogezwe mbele na kuwataka askari polisi wasiwachukulie hatua wenye mabango. Pia aliwauliza wanakasulu ni wangapi wanataka mkutano uendelee wengi wamenyoosha mikono kutaka mkutano uendelee. Hali si salama sana na nimeacha mpaka naingia mitamboni polisi wanatafuta mbinu mbadala za kuimarisha ulinzi na kuongeza kikosi.
tupe ushahidi wa picha
Sisapoti vurugu. Nampa pole Slaa kwa kupigwa mawe. Nawaomba wananchi wa kasulu mutumie njia za amani kudai haki zenu
Na vidole 007