Mkutano wa CCM kuzuiwa na Polisi?

Mkutano wa CCM kuzuiwa na Polisi?

CCM hawaishi sarakasi na vituko.
Watakuambia siasa ziishe watu wafanye Kazi.
Hivi siasa ni dhambi?

Wanajua wanaongea na vilaza. Sijui ni Watanzania wangapi wanajua maana halisi ya siasa? Utakuta watu ikiwa ni pamoja na viongozi wakuu wanadai maendeleo hayahitaji siasa!
 
Tunalipenda Jeshi letu sikivu, Jeshi lenye Nidhamu na hivyo tunaliomba liendelee na msimamo wake ule ule wa kuzuia mikutano ya vyama vya Siasa kama ilivyofanya kwa Chadema na ACT Wazalendo.

Tarehe 23 Julai 2016 CCM nao wametangaza Mkutano wao wa kumkabidhi Mwenyekiti chama, huu ni Mkutano wa kisiasa, ni Mkutano ambao hauna tofauti na ule wa ACT wa ndani ya Ukumbi au ule wa Sherehe za CHASO huko Dodoma Leo. Tunaamini Jeshi letu pendwa litapeleka Magari ya Washa Washa kwenda kuzuia Mkutano ule. Naam ni Mkutano wa Siasa!

Asante Jeshi letu pendwa....
kwani tanazania kuna polisi mm naona ni tawi la ccm tu
 
Sidhani kama mikutano chaguzi ndani ya chama imekatazwa, ni kiasi cha kwenda kuomba kibali unaulizwa ni mkutano wa aina gani?! Simple as that
 
Kama juzi ccm mwanza waliandama kisa diwani wao kawekewa sumu ofisini na rpc akasema hakuwa anafahamu kama ccm waliandamana, hata hiyo ya mkutano wao utafanyika salama tu na maisha yatasonga tu
Polisi watasema intelejensia yao imethibitisha kuwa hakutakuwa na uvunjifu wa amani katika mkutano wa CCM kwa kuwa hakuna chama kingine ambacho nacho kimeonyesha kitafanya kile ambacho CCM wanafanya. Aidha, watasema intelejensia yao imeonyesha hapatakuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani nchini kote siku CCM wanafanya mkutano wao......
 
Polisi watasema intelejensia yao imethibitisha kuwa hakutakuwa na uvunjifu wa amani katika mkutano wa CCM kwa kuwa hakuna chama kingine ambacho nacho kimeonyesha kitafanya kile ambacho CCM wanafanya. Aidha, watasema intelejensia yao imeonyesha hapatakuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani nchini kote siku CCM wanafanya mkutano wao......
Na kwa kuwa wale vibaka wa amboni wamesha dhibitiwa
 
Sidhani kama mikutano chaguzi ndani ya chama imekatazwa, ni kiasi cha kwenda kuomba kibali unaulizwa ni mkutano wa aina gani?! Simple as that
Kwahiyo kwenye mikutano ya chaguzi midomo ya watu itawekwa gundi? Maana kinachohofiwa ni maneno yanayotoka vinywani mwa wanasiasa, sio ile mikusanyiko!
 
Mazingira ya mkutano wa CCM huko Dodoma yakoje, na mazingira ya mkurano wa ACT Wazalendo na CHASO yakoje? Lengo la mkutano wa CCM ni lipi? na lengo la mkutano wa CHASO na ACT Wazalendo lilikuwa lipi?
Kwahio tunaangalia Mazingira? Au tunaangalia ajenda? Au tunaangalia nani atakuepo wapi??
 
Sidhani kama mikutano chaguzi ndani ya chama imekatazwa, ni kiasi cha kwenda kuomba kibali unaulizwa ni mkutano wa aina gani?! Simple as that
Mkuu Mkutano wa Zito ulikua wa Ndani au wa nje?? Mahafali Ya CHASO yalikua Ya ndani au ya nje? Maandamano Ya CCM kule Mwanza yalikua Ya ndani au ya nje? Hahahaaha Hahahahaha
 
Mkuu Mkutano wa Zito ulikua wa Ndani au wa nje?? Mahafali Ya CHASO yalikua Ya ndani au ya nje? Maandamano Ya CCM kule Mwanza yalikua Ya ndani au ya nje? Hahahaaha Hahahahaha

swala ni kibali! mkutano wowote wa kisiasa omba kibali...

mbona chaso dar wamefanya!? si wamefata taratibu
 
swala ni kibali! mkutano wowote wa kisiasa omba kibali...

mbona chaso dar wamefanya!? si wamefata taratibu
Hivi yale Mahafali Ya CHASO pale Dodoma yalihitaji kibali? Oooghh Sikujua Mkuu, asante
 
Back
Top Bottom