Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Mkurugenzi wanyamapori ang'olewa
Imeandikwa na Hellen Mlacky; Tarehe: 4th March 2011
WIZARA ya Maliasili na Utalii, imefanya mabadiliko kwa kumuondoa katika wadhifa wake, Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Erasmus Tarimo.
Kwa mujibu wa taarifa za uhakika kutoka katika Wizara hiyo, nafasi ya Tarimo aliyeishikilia tangu Desemba 2007, imechukuliwa na Obeid Mbangwa aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Matumizi ya Wanyamapori.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alipoulizwa kuhusu mabadiliko hayo, alielekeza aulizwe Katibu Mkuu, lakini anayekaimu nafasi hiyo kwa sasa, Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Kale hakupatikana kuzungumzia hilo. Huenda taarifa rasmi ya mabadiliko hayo ikatolewa leo.
Kuondolewa kwa Tarimo katika Idara ya Wanyamapori kumekuja siku nne tangu Rais Jakaya Kikwete abadilishe makatibu wakuu ambapo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Ladislaus Komba, amepelekwa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambako kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, atapangiwa kazi maalumu.
Katibu Mkuu mpya ni Maimuna Tarishi. Wakati huo huo, Serikali imeanza makubaliano na India kwa lengo la kuweka kichocheo kwa watalii kutoka nchini humo kuwekeza katika utalii nchini kwa lengo la kukuza pato la taifa kupitia utalii hususan kwa kufungua mawasiliano ya ndege katika nchi hizo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kutokana na ziara waliyoifanya India kwa lengo la kuhimiza utalii.
Alisema katika ziara hiyo alizungumza na wamiliki wa shirika kubwa la ndege la India la ‘Jet Airways' ambalo lilikubali kuanzisha mchakato wa kuomba kibali cha kutua Dar es Salaam na katika kufanikisha azma hiyo, ameiagiza Bodi ya Utalii kufuatilia suala hilo ili shirika hilo lipate kibali.
Aidha, alisema alihimiza utalii wa mikutano ambapo alizungumza na wakala wa Kampuni ya Sun Pharmaceutical Ltd ambayo ina watumishi 12,000 duniani kote kufanya mkutano na watumishi wake nchini Tanzania mwaka huu ambapo aliridhia katika juma la tatu la Julai.
Alisema kampuni hiyo huwa inawapa watumishi wake motisha kwa kuwasafirisha kwenda nje ya India kwa ajili ya utalii na kufanya mkutano na kupongezana na watakaokuja ni 1,000 hivyo kutokana na maridhiano hayo, kamati maalumu itaundwa chini ya TTB ili kufanikisha maandalizi ya ujio huo.
Imeandikwa na Hellen Mlacky; Tarehe: 4th March 2011
WIZARA ya Maliasili na Utalii, imefanya mabadiliko kwa kumuondoa katika wadhifa wake, Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Erasmus Tarimo.
Kwa mujibu wa taarifa za uhakika kutoka katika Wizara hiyo, nafasi ya Tarimo aliyeishikilia tangu Desemba 2007, imechukuliwa na Obeid Mbangwa aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Matumizi ya Wanyamapori.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alipoulizwa kuhusu mabadiliko hayo, alielekeza aulizwe Katibu Mkuu, lakini anayekaimu nafasi hiyo kwa sasa, Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Kale hakupatikana kuzungumzia hilo. Huenda taarifa rasmi ya mabadiliko hayo ikatolewa leo.
Kuondolewa kwa Tarimo katika Idara ya Wanyamapori kumekuja siku nne tangu Rais Jakaya Kikwete abadilishe makatibu wakuu ambapo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Ladislaus Komba, amepelekwa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambako kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, atapangiwa kazi maalumu.
Katibu Mkuu mpya ni Maimuna Tarishi. Wakati huo huo, Serikali imeanza makubaliano na India kwa lengo la kuweka kichocheo kwa watalii kutoka nchini humo kuwekeza katika utalii nchini kwa lengo la kukuza pato la taifa kupitia utalii hususan kwa kufungua mawasiliano ya ndege katika nchi hizo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kutokana na ziara waliyoifanya India kwa lengo la kuhimiza utalii.
Alisema katika ziara hiyo alizungumza na wamiliki wa shirika kubwa la ndege la India la ‘Jet Airways' ambalo lilikubali kuanzisha mchakato wa kuomba kibali cha kutua Dar es Salaam na katika kufanikisha azma hiyo, ameiagiza Bodi ya Utalii kufuatilia suala hilo ili shirika hilo lipate kibali.
Aidha, alisema alihimiza utalii wa mikutano ambapo alizungumza na wakala wa Kampuni ya Sun Pharmaceutical Ltd ambayo ina watumishi 12,000 duniani kote kufanya mkutano na watumishi wake nchini Tanzania mwaka huu ambapo aliridhia katika juma la tatu la Julai.
Alisema kampuni hiyo huwa inawapa watumishi wake motisha kwa kuwasafirisha kwenda nje ya India kwa ajili ya utalii na kufanya mkutano na kupongezana na watakaokuja ni 1,000 hivyo kutokana na maridhiano hayo, kamati maalumu itaundwa chini ya TTB ili kufanikisha maandalizi ya ujio huo.