ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bw. Alberic Kacou akisoma hotuba katika ufunguzi wa Semina ya Siku ya Wahariri wakuu wa vyombo vya habari nchini ambapo alisisitiza ushirikiano katika ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa Tanzania ikiwa ni nchi moja wapo kusimamia, kusaidia na kuhamasisha utetezi wa haki za Binadamu chini ya Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa UN. Semina hiyo imefanyika kwa ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa nchini na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.Kulia ni Mkurugenzi wa Masuala ya mahusiano ya Katiba na Haki za Binadamu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Mathew Mwamu.
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. George Masaju akifungua semina ya Wahariri wa Vyombo vya habari nchini iliyolenga kuwafahamisha kuhusu kusaidia kuandika habari juu ya haki za binadamu. Semina hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Masuala ya mahusiano ya Katiba na Haki za Binadamu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Mathew Mwamu.
(Pich kwa hisani ya Moblog