Mkurugenzi MORUWASA unatesa wananchi Morogoro

Patriot

JF-Expert Member
Feb 11, 2008
5,698
4,693
Niko hapa morogoro ktk moja ya hotel zinazosifika. Ninachokiona bado rais Magufuli hajapata watu wanaostahili kumsaidia ktk uongozi. Kuna watu hawa wanaojiita ni wakurugenzi, mainjinia wa maji. Watu hawa wanatia aibu takribani miji yote isipokuwa Tanga.

Hapa morogoro hakuna maji. Kisingizio cha mkurugenzi wa MORUWASA eti maji hayatoshi kwa wakazi wa mji huu lakini ajabu ni kwamba kuna magari yanasomba maji toka huko huko MORUWASA na kuyaleta mahotelini na majumbani. Hali hii haikubaliki na ni aibu kuendelea kuwa na wakurugenzi wa aina hii. yasemekana magari haya ni miradi yao waajiliwa wa MORUWASA!

Nasikitika sana kuona suti ninayovaa na kujiita mgeni ndani ya hotel, naishia kuoga maji ya ndoo na vikopo. Kule kwangu Dar, tunaoga maji ya chumvi yaliyochimbwa na mahoteli, labda huko idadi ni kubwa, iweje kamji kama haka nako ni tatizo?
 
Pole sana next time usifikie guest za bei poa hukk vichochoroni. Guest hata Tank na pump ya kupandisha maji haina? Vp mbu nao?
 
hilo ni tatizo sugu kwa Morogoro mjini....

inasikitisha kuona wawakilishi wa kisiasa wapo kimya kuhusu hili na waziri mwenye dhamana ajachukua hatua yoyote....
 
Pole sana next time usifikie guest za bei poa hukk vichochoroni. Guest hata Tank na pump ya kupandisha maji haina? Vp mbu nao?
Hahaaaa! Kumbe waganga wa kienyeji wana kazi rahisi sana. Kuna watu badala ya kwenda hospitali, munajitafutia tiba wenyewe! Tumia vyombo husika kwa viwango husika. Achana na mambo ya visima, matenki, bhla-bhla! Unanishauri nilale kwenye hoteli zenye matenki! Uzuri nina ka elimu kakutosha kukupa hata ushauri. Siku nyingine ukiwa safarini sikiliza harufu ya maji unayooga. Kama una uelewa kama wangu utaisikia harufu ya humic acid. Ukiisikia tu, hiyo ina maana unaoga uchafu wa udongo na kwa hapa Dar, hicho ni kinyesi.

Baadaye angalia matenki ya maji yako hapo nje, ukiona ukoko wa blue, hiyo ni ishara nyingine ya maji machafu ya chumvi ya baharini. Unaijua sababu? Pole. Maji siyo mahitaji ya kujitafutia. Ni hitaji linalotolewa na vyombo maalumu kwa viwango!
 
Hahaaaa! Kumbe wanganga wa kienyeji wana kazi rahisi sana. Kuna watu badala ya kwenda hospitali, munajitafutia tiba wenyewe! Tumia vyombo husika kwa viwango husika. Achana na mambo ya visima, matenki, bhla-bhla! Unanishauri nilale kwenye hoteli zenye matenki! Uzuri nina ka elimu kakutosha kukupa hata ushauri. Siku nyingine ukiwa safarini sikiliza harufu ya maji unayooga. Kama una uelewa kama wangu utaisikia harufu ya humic acid. Ukiisikia tu, hiyo ina maana unaoga uchafu wa udongo na kwa hapa Dar, hicho ni kinyesi.

Baadaye angalia matenki ya maji yako hapo nje, ukiona ukoko wa blue, hiyo ni ishara nyingine ya maji machafu ya chumvi ya baharini. Unaijua sababu? Pole. Maji siyo mahitaji ya kujitafutia. Ni hitaji linalotolewa na vyombo maalumu kwa viwango!
Dogo umebobea guest za uchochoroni(@ cheap)
Hujui Tank za maji ni nini? Au hujui km zinakuwa installed kwenye majengo kupokea maji kutoka bombani? Gv me a break! Wewe ni msomi? Kweli umezoea hayo ambayo ni chooni km ulivyosema.

Nakushauri tena usafiripo jali afya yako na usalama wako, fikia mahali sahihi acha Upare wako
 
Morogoro ni mkoa wa CCM . Na CCM ndio maisha waliyozoea. Kuishi bila maji hawalalamiki wanasubiri Tshirts na Kofia 2020. Na bado maji wataambiwa hakuna ili wanunue . Wanaishi kama mashetani ya kijani
 
Niko hapa morogoro ktk moja ya hotel zinazosifika. Ninachokiona bado rais Magufuli hajapata watu wanaostahili kumsaidia ktk uongozi. Kuna watu hawa wanaojiita ni wakurugenzi, mainjinia wa maji. Watu hawa wanatia aibu takribani miji yote isipokuwa Tang
a.

Hapa morogoro hakuna maji. Kisingizio cha mkurugenzi wa MORUWASA eti maji hayatoshi kwa wakazi wa mji huu lakini ajabu ni kwamba kuna magari yanasomba maji toka huko huko MORUWASA na kuyaleta mahotelini na majumbani. Hali hii haikubaliki na ni aibu kuendelea kuwa na wakurugenzi wa aina hii. yasemekana magari haya ni miradi yao waajiliwa wa MORUWASA!

Nasikitika sana kuona suti ninayovaa na kujiita mgeni ndani ya hotel, naishia kuoga maji ya ndoo na vikopo. Kule kwangu Dar, tunaoga maji ya chumvi yaliyochimbwa na mahoteli, labda huko idadi ni kubwa, iweje kamji kama haka nako ni tatizo?
MOROWASA ni takataka
 
Mkuu umenitubua hasira zangu zilizolala yaani idara ya maji morogoro imeoza kishenzi sijui kwanini viongozi wanalea hawa watu hawana ubunifu wanajali matumbo yao wananchi wanapitisha wiki nzima hawana maji

Visingizio vya kijinga jinga sana mafisadi sana kujifanya wanajua kufuatilia bili .

Maji yenyewe yakitoka machafuuu

Naweza kusema idara ya maji morogoro ndo idara mbovu kuliko zote Tanzania.

Kitila mkumbo na watendaji wemgine moruwasa ni bonge LA assignment kwenu .

Watoeni hao watu muwasaidie wakazi wa Moro
 
HI I THREAD NAPENDA SANA IMFIKIE MKUU , UKWELI NI KWAMBA MORUWASA WANALETA MZAHA SANA KATIKA KAZI, HAPA MOROGORO KWANZA MAJI HAWAYA TREAT VZR ILA ZAIDI NI KUNA UKOSEFU WA MAJI MUDA MWINGI KIASI CH KWAMBA HAMNA KAZI ZINAZOONEKANA ZA MUHIMU WAZIFANYAZO MORUWASA .. NAJUA MKURUGENZI WA MORUWASA NA MAINJIA UCHWARA WAKO MNAONA HAYA MALALAMIKO , NI KHERI MKATUMBULIWA MKAE PEMBENI NA SIO KUISHIA KUTESA WANANCHI TU
 
MORUWASA wamezoea, iwe mvua au jua kama mwezi huu lakini mgao kama kawa. Kama hapa maeneo yangu, ukipata leo maji, kesho ujue hamna. Wenyewe wanachukulia poa, maji yenyewe yanaleta mba kishenzi.
Haajitambui hawa jamaa.
 
ukiona mkoa kama Morogoro wana shida ya maji safi... hii ni kwamba viongozi wao hawana umuhimu wala faida kuwepo ktk uongozi....

mkoa wa Morogoro una vyanzo vingi vya Maji kuliko Shinyanga au Singida....
 
Haingii akilini mkoa kama morogoro pawepo na ukosefu wa maji kiasi hiki.maji yenyewe kuna baadhi ya sehemu kama kola b yanatoka mara moja kwa wiki siku ya ijumaa tu!na maji yenyewe yakitoka ni uchafu mtupu...kuna haja kubwa ya kuutizama upya uongozi wa mamlaka husika
 
Niko hapa morogoro ktk moja ya hotel zinazosifika. Ninachokiona bado rais Magufuli hajapata watu wanaostahili kumsaidia ktk uongozi. Kuna watu hawa wanaojiita ni wakurugenzi, mainjinia wa maji. Watu hawa wanatia aibu takribani miji yote isipokuwa Tanga.

Hapa morogoro hakuna maji. Kisingizio cha mkurugenzi wa MORUWASA eti maji hayatoshi kwa wakazi wa mji huu lakini ajabu ni kwamba kuna magari yanasomba maji toka huko huko MORUWASA na kuyaleta mahotelini na majumbani. Hali hii haikubaliki na ni aibu kuendelea kuwa na wakurugenzi wa aina hii. yasemekana magari haya ni miradi yao waajiliwa wa MORUWASA!

Nasikitika sana kuona suti ninayovaa na kujiita mgeni ndani ya hotel, naishia kuoga maji ya ndoo na vikopo. Kule kwangu Dar, tunaoga maji ya chumvi yaliyochimbwa na mahoteli, labda huko idadi ni kubwa, iweje kamji kama haka nako ni tatizo?
Morogoro Mtaa was Mlimani kata ya mkundi, maji watu wananunua ndoo tsh 400 had 500/= umeme hakuna Barbara hazijachongwa, nk viwanja vimepimwa nyumba ziko nyingi, wananchi wengi. Tabu ya maji utafikiri Jangwani. Diwani hakai ktk kata take ndiyo tatizo. Mbunge hajawahi tembelea mtaa huu.
 
Morogoro Viongozi Wako Wapi
Yaani Tafori Imejengwa Miaka Ya Karibu Ila Eneo Kongwe Kama Kingolwira Hakuna Maji Zaidi Ya Story

Rais Alisema Kiongozi Akishindwa Kutatua Kero Za Wananchi Akija Kutatua Rais Anamtatua Kiongozi Naye
Yaani
Mkuu Wa Mkoa, Wilaya, Mainjia, Wakurugenzi
Kazi Hakuna
 
Zamani Morogoro maji yalikuwa yanatiririka kila kona ya mlima. Mito ilikuwa ina flow all over the town. Tatizo la wananchi kuharibu mazingira sasa athari zake ndio hizo... Kuna kazi sana kushughulikia changamoto za maji going foward...
 
Zamani Morogoro maji yalikuwa yanatiririka kila kona ya mlima. Mito ilikuwa ina flow all over the town. Tatizo la wananchi kuharibu mazingira sasa athari zake ndio hizo... Kuna kazi sana kushughulikia changamoto za maji going foward...
Hili la mazingira ni ziada ya uzembe kwa viongozi wa mkoa. Kumbe ndo maana Makonda anatolewa kama mfano wa kuigwa maana Mkuu wa mkoa wa Morogoro ana ubunifu gani?? Kila mwaka miezi hii milima yote inawashwa moto. Mgeni yeyote ukifika moro, usiku ni kizaa zaa! Baada ya muda wake huu, nini anachoweza kuonyesha kwamba hili ni matokeo ya fikra zake?
 
Back
Top Bottom