Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 303
SERIKALI imesema kuwa ukuaji wa pato la taifa katika unakadiriwa kuongezeka na kwamba pato halisi litakua kwa asilimia 7 katika mwaka 2010.
Akiwasilisha taarifa ya mwelekeo wa uchumi kwa mwaka 2009 na mwelekeo katika kipindi cha kuanzia 2010 hadi 2013 mbele ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo alisema kuna matarajio makubwa uchumi kuendelea kukua.
Huku akiwaomba radhi wabunge kwa kuchelewa kuwapa nakala ya taarifa hiyo, Mkulo alisema maelezo hayo yalipitishwa juzi asubuhi na Baraza la Mawaziri.
"Naomba radhi waheshimiwa kwa kuchelewa kuwapatia nakala ya taarifa hii kwa kuwa imepitishwa jana asubuhi (juzi) na Baraza la Mawaziri hivyo imechelewa kuchapwa," Mkulo alisema.
Mkulo alisema kuwa katika mwaka 2011, pato halisi la uchumi litakuwa kwa asilimia 7.1, mwaka 2012 asilimia 7.4 na hadi kufikia mwaka 2013 pato halisi la taifa litafikia asilimia 7.8.
My take:
Labda hoja yangu niiweke katika msingi wa swali 'nini maana ya uchumi wa nchi kukua Vs hali halisi ya wananchi wake' inawezekana labda mimi ndiye huwa siielewi serikali inaposema uchumi wetu umeongezeka ukilinganisha na mwaka uliopita wakati mfumko wa bei unazidi kupaa huku pato la wananchi walio wengi likizidi kuwa chini ya dola moja kwa siku.
Naomba msaada tafadhali.
Akiwasilisha taarifa ya mwelekeo wa uchumi kwa mwaka 2009 na mwelekeo katika kipindi cha kuanzia 2010 hadi 2013 mbele ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo alisema kuna matarajio makubwa uchumi kuendelea kukua.
Huku akiwaomba radhi wabunge kwa kuchelewa kuwapa nakala ya taarifa hiyo, Mkulo alisema maelezo hayo yalipitishwa juzi asubuhi na Baraza la Mawaziri.
"Naomba radhi waheshimiwa kwa kuchelewa kuwapatia nakala ya taarifa hii kwa kuwa imepitishwa jana asubuhi (juzi) na Baraza la Mawaziri hivyo imechelewa kuchapwa," Mkulo alisema.
Mkulo alisema kuwa katika mwaka 2011, pato halisi la uchumi litakuwa kwa asilimia 7.1, mwaka 2012 asilimia 7.4 na hadi kufikia mwaka 2013 pato halisi la taifa litafikia asilimia 7.8.
My take:
Labda hoja yangu niiweke katika msingi wa swali 'nini maana ya uchumi wa nchi kukua Vs hali halisi ya wananchi wake' inawezekana labda mimi ndiye huwa siielewi serikali inaposema uchumi wetu umeongezeka ukilinganisha na mwaka uliopita wakati mfumko wa bei unazidi kupaa huku pato la wananchi walio wengi likizidi kuwa chini ya dola moja kwa siku.
Naomba msaada tafadhali.