Mkulo: Msilipe Kodi Ruksa

Duduwasha

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
5,703
3,653
Kauri ya Mustapha Mkulo Waziri wa Fedha, Katika Serikali ya Ajabu Kutokea Duniani Iliyojaa Vilaza Wasio Na Idadi, Isiyo na maadili ya uongozi, ufisadi isiyofuata sheria za nchi, ubabaishaji uliopitiliza. Nchi haina msemaji wake kila waziri akiamka na lake ndotoni analitamka liwe hivyo tumeona kuanzia mkuu hadi vijana wa chama cha mapinduzi sijui tunasubiri nini. Tunaongozwa na watu walioshindwa kutuletea maisha bora kama walivyotuahidi, hii inamaana tumedanganywa. CCM achieni madaraka huu sio uungwana, kubalini yaishe tunajua mlichakachua na imedhihilishwa na raia wengi hawakuwaunga mkono kwenye uchaguzi hampendwi kila kona ya nchi sio hadi fujo zianze kutokea mnyooshewe mkono na jumuia ya kitaifa kama gaddafi kuwa mmekosa imani na wananchi wenu. Jiondoweni mapema au mrekebishe nchi muwaondowe wanaoifanya nchi iende ovyo mnawajua ila mnawaogopa. siku hazigandi Na Kauri ya Mkulo akinukuu maneno ya laana aliyopewa adam ale kwa jasho lake litakuwa imewaudhi wengi kwani sie tunalipa kodi ambazo ni jasho letu inamaana tuache kulipa. naomba uombe radhi kwa watanzania. msivyo na iana Mtakuja sema ile sio kauri ya Serikali. nani haswa msemaji wa serikali.
 
yale yale ya waziri wa fedha wa zamani mheshimiwa Basil Pesambili Mramba.

tulikula majani rada na ndege ya raisi ikanunuliwa

amekuja kilaza mwingine anatuambia tule jasho letu

wamesahau wao ndio wanaokula jasho letu
 
Kwani Tanzania tuna serikali? Mbona kila kiongozi anajifanyia mambo yake bila hata wakumzuia? Mbona kuna watu ambao wako juu ya sheria? Mbona kuna watu wanaonyanyasika na kudhulumiwa kila kukicha lakini hakuna wa kuwaokoa au kuwalinda? Mbona wananchi walichagua CHEDEMA halafu kikundi fulani (NEC) kikasema wananchi wamechagua CCM na hakukuwa na wa kuhoji kwa nini kikundi hicho kilipindisha matokeo? Hivi kama Tanzania ina serikali makini, haya yote na mengine yangekuwa yanatokea bila hatua yoyote kuchukuliwa?
 
Mmekosa hoja, mmebaki kungoja Rais na maWaziri wake wanasema muanza kupiga vuvuzela.

Hivi huwa hamna ubunifu?
 
Kauri ya Mustapha Mkulo Waziri wa Fedha, Katika Serikali ya Ajabu Kutokea Duniani Iliyojaa Vilaza Wasio Na Idadi, Isiyo na maadili ya uongozi, ufisadi isiyofuata sheria za nchi, ubabaishaji uliopitiliza. Nchi haina msemaji wake kila waziri akiamka na lake ndotoni analitamka liwe hivyo tumeona kuanzia mkuu hadi vijana wa chama cha mapinduzi sijui tunasubiri nini. Tunaongozwa na watu walioshindwa kutuletea maisha bora kama walivyotuahidi, hii inamaana tumedanganywa. CCM achieni madaraka huu sio uungwana, kubalini yaishe tunajua mlichakachua na imedhihilishwa na raia wengi hawakuwaunga mkono kwenye uchaguzi hampendwi kila kona ya nchi sio hadi fujo zianze kutokea mnyooshewe mkono na jumuia ya kitaifa kama gaddafi kuwa mmekosa imani na wananchi wenu. Jiondoweni mapema au mrekebishe nchi muwaondowe wanaoifanya nchi iende ovyo mnawajua ila mnawaogopa. siku hazigandi Na Kauri ya Mkulo akinukuu maneno ya laana aliyopewa adam ale kwa jasho lake litakuwa imewaudhi wengi kwani sie tunalipa kodi ambazo ni jasho letu inamaana tuache kulipa. naomba uombe radhi kwa watanzania. msivyo na iana Mtakuja sema ile sio kauri ya Serikali. nani haswa msemaji wa serikali.

Hivi wewe ni mTanzania kweli? Hata kiswahili hujui? Halafu unajidai una uchungu na Tanzania? Mtanzania wa kweli lazima ajuwe tofauti ya "kauri" na kauli.
 
Mmekosa hoja, mmebaki kungoja Rais na maWaziri wake wanasema muanza kupiga vuvuzela.

Hivi huwa hamna ubunifu?

Mwambie Kikwete na serikali yake sio wabunifu kama wangekuwa wabunifu nchi isingeingizwa kwenye Mikataba feki, Matatizo ya Umeme, Mfummo wa bei au wewe ndio umetumwa na Mafisadi kujibu hoja hapa? wanakulipa Shs ngapi au ndio umepachikwa sehemu ili utafune kodi za Watanzania?
Nenda kapate Kikombe kwa babu akili zitulie na ufunguke macho, unahitaji msaada sio bure wewe
 
Hivi wewe ni mTanzania kweli? Hata kiswahili hujui? Halafu unajidai una uchungu na Tanzania? Mtanzania wa kweli lazima ajuwe tofauti ya "kauri" na kauli.

Kwani nyie wanyonyaji wewe na mkwere mwatuona sie ni Watanzania?hata sishangai kwa taarifa yako, Mtanzania ni Rostam Azizi Ngeleja, Majimshindo Tendwa na wengine wengi nitasaidiwa kutajiwa nyie ndio mnaonesha mna uchungu na Tanzania sababu ni tamu kwenu.. sababu ni MBU wanyonyaji mkistuliwa mwalia nzzzzzzzz!!!
 
Mmekosa hoja, mmebaki kungoja Rais na maWaziri wake wanasema muanza kupiga vuvuzela.

Hivi huwa hamna ubunifu?

Hapo kwenye Nyekundu je wewe ni Mtanzania huweki neno lieleweke au kila kitu mwapotosha tu. CCM mnatoa mapovu hiyo ni laana ya kuchakachua kura Kama chama chenu ni cha mapinduzi basi mapinduzi mwajifanyia nyie wenyewe mwisho wenu umekaribia siku zenu zinahesabika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom