Duduwasha
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 5,703
- 3,653
Kauri ya Mustapha Mkulo Waziri wa Fedha, Katika Serikali ya Ajabu Kutokea Duniani Iliyojaa Vilaza Wasio Na Idadi, Isiyo na maadili ya uongozi, ufisadi isiyofuata sheria za nchi, ubabaishaji uliopitiliza. Nchi haina msemaji wake kila waziri akiamka na lake ndotoni analitamka liwe hivyo tumeona kuanzia mkuu hadi vijana wa chama cha mapinduzi sijui tunasubiri nini. Tunaongozwa na watu walioshindwa kutuletea maisha bora kama walivyotuahidi, hii inamaana tumedanganywa. CCM achieni madaraka huu sio uungwana, kubalini yaishe tunajua mlichakachua na imedhihilishwa na raia wengi hawakuwaunga mkono kwenye uchaguzi hampendwi kila kona ya nchi sio hadi fujo zianze kutokea mnyooshewe mkono na jumuia ya kitaifa kama gaddafi kuwa mmekosa imani na wananchi wenu. Jiondoweni mapema au mrekebishe nchi muwaondowe wanaoifanya nchi iende ovyo mnawajua ila mnawaogopa. siku hazigandi Na Kauri ya Mkulo akinukuu maneno ya laana aliyopewa adam ale kwa jasho lake litakuwa imewaudhi wengi kwani sie tunalipa kodi ambazo ni jasho letu inamaana tuache kulipa. naomba uombe radhi kwa watanzania. msivyo na iana Mtakuja sema ile sio kauri ya Serikali. nani haswa msemaji wa serikali.