Mkullo: Maisha yangu yako hatarini!

Hayawani huyu!

Usemi kama huo ni kutaka kujikuza kwamba yeye ni mtu mkubwa sana, muhimu sana ambaye safari zake ni siri, ndo maana ni hatari kuzitaja.

Half-brain person at the tresury control.
 
Lakini ebu tuangali upeo wa elimu ya Mkullo ktk historia ya ofisi ambazo amewahi kufanya kazi huyu jamaa cv yake haijulikani kabisa ki-elimu amesoma mpaka kiwango gani kwani mpaka leo hata ukienda kwenye mtandao wa wabunge mkullo cv yake iko nyeupe kabisa hakuna kitu sasa mtu kama huyu angekuwa na elimu iliyo nyooka angefahamu zuri na baya hata athari za kuliingiza taifa ktk unexpected loss ya us dollar 5,000 bila ya maelezo.

Unajua nina mashaka sana na huyu jamaa kwani upande wa maadili ni zero kwani historia inaonyesha kuwa uzinzi na ufujaji wa mali za umma ni kama vile anakunywa supu ya asubuhi kazi yake kubwa ni kulimbikiza mademu kwenye mashirika ambayo yana ripoti hazina moja kwa moja.

Hata JK nae namshangaa sana kumpa wizara nyeti huyu jamaa kwa mara mbili mfululizo. Sasa angalia katishiwa nyau kidogo kwenye gazeti anaanza kumtafuta mchawi yaani hata kivuli chake akiongopa hii kali mno usiongope kufa wewe huna integrity kwa sasa Tanzania inanuuka kwa rushwa na tunaipeleka nchi kwenye civil wars, ukiona kwa mwenzio kuna teketekea au ukiona mwenzio ananyoolewa basi we tia maji. Sasa umati utakufika pale tu kuiendelea kufuja mali za walala hoi kwani sala zao Mungu anazipokea. Ndipo majanga kama haya hutaweza kuyakwepa dingi wa totoz.
 
hiyo ni ya mkulo tu,ukichanganya na mawaziri wengine je!! hakika watz tumekalia ncha ya mkuki
 
Solution simple tu, BADILIKA full stop. Btw mara 8 tu?????
 
No wonder almost 70% ya mapato ya serikali yanaishia kwenye operation and only 30% inaenda kwenye development project
 
Amekuwa waziri kwa miaka mitatu na nusu. Haya tuna Mawaziri 30 asuming kila mmoja amekodi mara nane tu @ 8 zidisha mara $5000 (wastani) = $ 1,200,000 (Tsh Billion 18)! kukodi ndege tu!! Kama siyo ubadhirifu ni nini?? Halafu anakomaa komaa

Mkuu hesabu yako nzuri, lakini hujawapigia hesabu ya posho ya hao madereva wao na mafuta ya bure ya kwenda Dodoma
 
Wakati mwingine ni vema kukaa kimya....watu watashindwa kukujaji kama una busara au huna.
 
mkulo ni fisadi tu kama walivyo akina mkwere, na wala asizingizie kua maisha yake yapo hatarini hakuna anaetaka kumuua. tunawashukuru wazalendo walitupatia habari hii dhidi ya matumizi mabaya ya rasilimali zetu
 
Hivi karibuni gazeti moja (Tanzania Daima Jumatano), likaamua kufuatilia safari ya waziri na dereva wake toka Dar es Salaam kwenda Dodoma baada ya kukodiwa ndege kwa gharama ya dola 5,000 bila kufanya uchunguzi kwa sababu gani ilifanyika hivyo...lakini ilikuwa imesukwa na baadhi ya watendaji wetu, tena wamo humu ili wamchafue Mkulo,” alisema.

Katika hotuba hiyo iliyokuwa fupi lakini iliyorefushwa na ufafanuzi wa taarifa hiyo iliyoonyesha kumkera sana Waziri Mkulo hivyo kumlazimu kutumia zaidi ya dakika 30 kutoa ufafanuzi juu ya mazingira ya kukodiwa ndege hiyo, Mkulo alisema hana mamlaka ya kujiamulia kukodi ndege na kuongeza kuwa tangu awe waziri, amekodiwa ndege mara nane tu.

Mkulo ambaye alionyesha kukerwa sana na taarifa hiyo, alisema wizara iliamua kumkodia ndege hiyo yeye na dereva wake kwenda Dodoma kutokana na majukumu yaliyokuwa yakimkabili likiwemo la kulazimika kukutana na baadhi ya mabalozi na mawaziri wa fedha toka nje ya nchi ambao walikuwa wanaliingizia taifa takriban dola za Kimarekani milioni 100.

“Akaandaliwa mwandishi uwanja wa ndege Dar es Salaam apige picha ndege anayopanda waziri na kule Dodoma akaandaliwa mwandishi kupiga picha ndege atakayoshuka waziri...ni hatari sana; hebu fikiria kama wangekuwa maharamia mimi si nigeuawa kwa dola 5,000 zinazodaiwa nimefuja!?” aliongeza.



Hiyo RED: Kwani Bw. Mkullo ana faida gani hasa kwa Tz? Ni mfujaji na fisadi kama aliyemteua tu. Nionavyo mimi hofu aliyonayo si hasa kuhusu Uwaziri bali ni kutokana na madudu mengine tu ambayo yanamwandama.
 
Sku zote tukiambiwa ukweli tunakuwa wakali, ila kama ni habari za ushuzi wala mtu hajali. Udhaifu mwingine ni wa kujitetea kwa watu, ooh mimi hivi ooh mimi vile, ukikaa kimya inasaidia sana!
Hata hivyo hao viongozi waliopewa dhamana wajue kuwa muda wao umefika!!!
 
..kwanini anataka akodi ndege kisirisiri?

..kwanini kuwe na usiri ktk matumizi ya fedha za walipa kodi?

..kwanini anafikiri maisha yake yako hatarini ikiwa anatekeleza majukumu yake kwa haki na uadilifu?
 
Ni kweli, mahafali na huo mkutano vyote vilipangwa, hakuna dharula hata moja hapo. Hoja kubwa kwa nini gari limfuate dodoma wakati kule magari yapo?

Well said mkuu. Ndio maana ni lazima tuwe na priorities. Hata kama alikuwa busy kwani kwenye mahafali ni lazima aende? Si angemtuma muwakilishi tuu. Inasikitisha jinsi viongozi wetu akili zao zinavyofikiria. Yaani ameshajiona victim. Kuna wakati watu walikuwa wanasema ni wakati wa kufanya kazi kwa uwazi na ukweli, naona hiyo imekua replaced na ari zaidi kasi zaidi.
 
..kwanini anataka akodi ndege kisirisiri?

..kwanini kuwe na usiri ktk matumizi ya fedha za walipa kodi?

..kwanini anafikiri maisha yake yako hatarini ikiwa anatekeleza majukumu yake kwa haki na uadilifu?

You said it all!!!!
 
Hata inashangaza zaidi kuona kua hajui kua jukumu la kufundisha usiri ofisini kwake lipo chini yake. Kashindwa kufundisha usiri ofisini yeye mwenyewe badala yake anatulaumu sisi wa kariakoo sokoni. Wakubwa wake walimpa cheo ili awafichie siri zao ama la sivyo wanamfutia uraia ama wanamuumbua na vyeti vyake - hii ndio CCM's office culture.
Wala haishangazi sana maana Mkuu wake wa kazi kaongelea swala la udini kufungua bunge, hajui kuwa ni jukumu lake kuhakikisha analikemea kwa uwazi mara moja pale linapojitokeza. Badala yake anangoja kuyumba kisiasa ndiyo abatize kuporomoka kwa sifa yake kitaifa kuwa ilitokana na udini. Kiongozi asiyeweza ku-delagate authority ili wakati hayupo kazi ziendelee kama kawaida siyo kiongozi mzuri hata kidogo. Angeweza kuondoka jana yake na kumwachia Waziri mdogo hiyo Wizara hata Katibu Mkuu angeliweza kuifanya. Siku hizi njia za mawasiliano ni nyingi sana akiwa kwenye V8 anaweza kuchapa kazi sana tu ila ni ule ule ujinga wa viongozi kujiona miungu watu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom