Mwitongo
JF-Expert Member
- Jan 30, 2009
- 312
- 362
Wana JF, nimekutana na hii katika Gazeti Jamhuri la leo katika website yao. Inaonekana Mkono anajiandaa kuvaa Gwanda!!!! Peopleeeeeeeeees!!!!
Mkono akubali kufukuzwa CCM
*Apata wasiwasi kuwa Nyerere aliuawa wakubwa waharibu mambo
*Filikunjombe asema wabunge ni wanafiki, yuko tayari kufukuzwa
*Nape asema vikao vipo, NEC yawatwisha mzigo wabunge wa CCM
Na Waandishi Wetu
Hali ya mambo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inazidi kuwa mbaya, baada ya mmoja wa makada na wafadhili wake maarufu, Nimrod Mkono, kusema yupo tayari kufukuzwa uanachama.
Hatua hiyo ya Mkono imekuja baada ya kuwapo tetesi kwamba wabunge watatu wa CCM - Mkono (Musoma Vijijini), Deo Filikunjombe (Ludewa) na Alphaxard Lugola (Mwibara), kuweka saini kwenye fomu yenye kusudio la kutaka kumng'oa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Mkono ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, ameiambia JAMHURI kwamba yupo tayari kwa lolote, ikiwa ni pamoja na kuvuliwa gamba kama itaonekana kuwa uamuzi wake wa kusaini ulikiuka misingi.
"Siwezi kubadili msimamo, heri nife kuliko kuunga mkono Serikali inayoiba, maana pale katika Mgodi wa Buhemba iliyoiba ni Serikali… imeondoa kila kitu na kuacha mashimo," alisema kwa hisia kali na kuongeza:
"Kwangu mimi haina faida kuwa mbunge kama kuna mambo ya kuwaumiza wananchi. Mimi ni mbunge wa wananchi wa Musoma Vijijini, natetea masilahi yao, sasa kama wanataka kunifukuza kwa kuwatetea wananchi, wanifukuze, nipo tayari. Chochote waamue, nipo tayari kabisa."
Amesema yeye na wabunge wenzake waliosaini fomu ya kumng'oa Waziri Mkuu walifanya hivyo kwa nia njema ya kuleta uwajibikaji serikalini, na kwamba huo ndiyo uliokuwa msimamo wa wabunge wengi kwenye kikao cha Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (party caucus).
"Watuvue magamba, mimi nipo tayari kuvuliwa gamba, hatuwezi kwenda hivyo. Katika party caucus tulikubaliana tuiwajibishe serikali. Mimi kila mahali naongea Buhemba, Buhemba, Buhemba. Kwenye vikao vya chama nazungumzia Buhemba, Kyarano, lakini hawasikii. Sasa kama hawanisaidii kumaliza hizi kero za wananchi, nikae kwenye chama kinisaidie nini?" Amehoji.
Kyarano ni bwawa lililochimbwa kwa maelekezo ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwanzoni mwa miaka ya 1980 kwa ajili ya shughuli za kilimo cha umwagiliaji. Lipo katika mpaka wa vijiji vya Butiama, Bisarye na Rwamkoma.
Mkono amesema; "Kila mara nazungumzia Buhemba kuwa dhahabu imechukuliwa, majengo na mitambo vimeibwa kwa usimamizi wa polisi na maofisa wa serikali. Kyarano imekufa. Vitu vya Mwalimu vimeharibiwa, nina faida gani?"
Mbunge huyo amekwenda mbali zaidi kwa kusema huenda ikawa kweli kwamba Mwalimu aliuawa kama alivyodai Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere, kwa sababu mambo mengi aliyoyasimamia Mwalimu yameachwa yafe.
"Nawaeleza hawaendi Buhemba, hawaendi Kyarano, maji Butiama hakuna, hawaendi…ndiyo kauli yangu hiyo kwamba kama wanataka kunifukuza, basi wanifukuze. Mimi ni mbunge, nimeyazungumza haya mara zote kama mbunge na si kama mhuni. Huo ndiyo msimamo wangu na sijawahi kuyumba. Kama wanataka kunifukuza, sawa!" amesema.
Kauli ya Nape kuhusu Mkono
Kauli ya Mkono ya kutamka wazi kwamba yupo tayari kufukuzwa kutoka CCM imemshitua Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye.
Alipoulizwa kama chama hicho kipo tayari kumpoteza mwanachama na mfadhili mahiri kama Mkono, Nape alianza kwa kukosoa taarifa zilizoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema zinalenga kuibua mjadala usiokuwapo.
"Nani kasema watahojiwa? Hoja hii ni kweli iliibuliwa kwenye kikao cha NEC kwa baadhi ya wajumbe kuhoji kwamba ilikuwaje wabunge wa CCM wakasaini kumng'oa madarakani Waziri Mkuu! Lakini tukaona kuwa hii ni hoja ya bungeni, na huko kuna party caucus. Uongozi wa Kamati ya Wabunge wa CCM upo, na haujatupatia taarifa rasmi kama kuna watu wamevunja kanuni.
"Tukasema kama wanaona kuna uvunjaji kanuni watujulishe. Nasema hii hoja inatengenezwa makusudi. Kama kulikuwa na tatizo, basi party caucus watatujulisha, lakini hadi sasa hatujapata taarifa rasmi. Wale wana kanuni zao za wabunge, kama wanaona kuna jambo linahitaji kufikishwa ngazi za juu wanalileta," amesema.
Alipoulizwa kama chama kinaweza kumwadhibu Mkono na wenzake, alisema, "Sipendi kuzungumzia mtu, hapa tunajadili kanuni na sheria. Tunaendesha chama kwa kanuni, sheria na taratibu, kama sheria zinasema Nape kakosea pamoja na umuhimu wake, sheria zitafuatwa. Nakuhakikishia katika hili hatujapata taarifa."
Nape: Maige si saizi yangu
Katika siku za karibuni, Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige (CCM), amenukuliwa akisema kwamba Nape ni gamba ndani ya CCM na anapaswa kuwajibishwa. Kwa upande wake, Nape amejibu mapigo kwa kusema, "Maige si saizi yangu, ni mbunge, atajibiwa na (CCM) wilaya yake. Nadhani wameshaanza kumjibu."
Filikunjombe: Wabunge hawafai
Kwa upande wake, Filikunjombe alipowasiliana na JAMHURI alisema yeye yuko tayari kufukuzwa kutoka CCM kama chama hicho kitamhukumu kuwa alifanya kosa kwa kutia saini azimio la kumg'oa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ila akasema uamuzi wa aina hiyo utamshangaza mno na unathibitisha unafiki wa wabunge wa CCM.
"Nimesikia walijadili suala hili kwenye NEC na Rais Kikwete akasema vikao vipo vingi, suala hili lipelekeni kwenye vikao husika kama party caucus bungeni.
"Mimi nasema sijutii uamuzi wangu. Tena nasema kama wapo wa kufukuzwa kutoka CCM ni wale waliokataa kusaini ndiyo waadhibiwe, kwa sababu huo ndiyo uliokuwa msimamo wa chama. Asilimia 90 au 95 ya wabunge walikuwa wanalalamika na tukakubaliana hivyo.
"Ajabu; ilipofika wakati wa kusaini daftari wengine wakawa wanalipita kama hawalioni. Wabunge wengi ni wanafiki sana. Ndiyo; tunapaswa kuwa na nidhamu lakini nidhamu ya woga haifai. Dhamira yangu iko safi kabisa, kwa hili nipo tayari kufukuzwa katika chama.
"Pamoja na kwamba ninaheshimu uamuzi wa vikao, ukweli utabaki pale pale kwamba nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.
"Hawa waliokataa kusaini ndiyo wa kufukuzwa maana walikuwa wanataka chama kianguke na serikali yake. Sasa itakuwa ajabu sisi tulioitetea serikali isiangushwe - tena serikali ya chama chetu - ndiyo tufukuzwe sitaelewa ila nipo tayari hata leo," amesema Filikunjombe.
Wabunge hao watatu waliungana na wabunge wa vyama vya upinzani vya Chadema, CUF, TLP na UDP kusaini azimio la kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, lililoandaliwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
Baada ya hatua hiyo, Serikali ililazimika kufanya mabadiliko makubwa kwenye Baraza la Mawaziri na mawaziri wanane na manaibu wawili kutupwa nje ya ulingo.
Mkono akubali kufukuzwa CCM
*Apata wasiwasi kuwa Nyerere aliuawa wakubwa waharibu mambo
*Filikunjombe asema wabunge ni wanafiki, yuko tayari kufukuzwa
*Nape asema vikao vipo, NEC yawatwisha mzigo wabunge wa CCM
Na Waandishi Wetu
Hali ya mambo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inazidi kuwa mbaya, baada ya mmoja wa makada na wafadhili wake maarufu, Nimrod Mkono, kusema yupo tayari kufukuzwa uanachama.
Hatua hiyo ya Mkono imekuja baada ya kuwapo tetesi kwamba wabunge watatu wa CCM - Mkono (Musoma Vijijini), Deo Filikunjombe (Ludewa) na Alphaxard Lugola (Mwibara), kuweka saini kwenye fomu yenye kusudio la kutaka kumng'oa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Mkono ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, ameiambia JAMHURI kwamba yupo tayari kwa lolote, ikiwa ni pamoja na kuvuliwa gamba kama itaonekana kuwa uamuzi wake wa kusaini ulikiuka misingi.
"Siwezi kubadili msimamo, heri nife kuliko kuunga mkono Serikali inayoiba, maana pale katika Mgodi wa Buhemba iliyoiba ni Serikali… imeondoa kila kitu na kuacha mashimo," alisema kwa hisia kali na kuongeza:
"Kwangu mimi haina faida kuwa mbunge kama kuna mambo ya kuwaumiza wananchi. Mimi ni mbunge wa wananchi wa Musoma Vijijini, natetea masilahi yao, sasa kama wanataka kunifukuza kwa kuwatetea wananchi, wanifukuze, nipo tayari. Chochote waamue, nipo tayari kabisa."
Amesema yeye na wabunge wenzake waliosaini fomu ya kumng'oa Waziri Mkuu walifanya hivyo kwa nia njema ya kuleta uwajibikaji serikalini, na kwamba huo ndiyo uliokuwa msimamo wa wabunge wengi kwenye kikao cha Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (party caucus).
"Watuvue magamba, mimi nipo tayari kuvuliwa gamba, hatuwezi kwenda hivyo. Katika party caucus tulikubaliana tuiwajibishe serikali. Mimi kila mahali naongea Buhemba, Buhemba, Buhemba. Kwenye vikao vya chama nazungumzia Buhemba, Kyarano, lakini hawasikii. Sasa kama hawanisaidii kumaliza hizi kero za wananchi, nikae kwenye chama kinisaidie nini?" Amehoji.
Kyarano ni bwawa lililochimbwa kwa maelekezo ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwanzoni mwa miaka ya 1980 kwa ajili ya shughuli za kilimo cha umwagiliaji. Lipo katika mpaka wa vijiji vya Butiama, Bisarye na Rwamkoma.
Mkono amesema; "Kila mara nazungumzia Buhemba kuwa dhahabu imechukuliwa, majengo na mitambo vimeibwa kwa usimamizi wa polisi na maofisa wa serikali. Kyarano imekufa. Vitu vya Mwalimu vimeharibiwa, nina faida gani?"
Mbunge huyo amekwenda mbali zaidi kwa kusema huenda ikawa kweli kwamba Mwalimu aliuawa kama alivyodai Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere, kwa sababu mambo mengi aliyoyasimamia Mwalimu yameachwa yafe.
"Nawaeleza hawaendi Buhemba, hawaendi Kyarano, maji Butiama hakuna, hawaendi…ndiyo kauli yangu hiyo kwamba kama wanataka kunifukuza, basi wanifukuze. Mimi ni mbunge, nimeyazungumza haya mara zote kama mbunge na si kama mhuni. Huo ndiyo msimamo wangu na sijawahi kuyumba. Kama wanataka kunifukuza, sawa!" amesema.
Kauli ya Nape kuhusu Mkono
Kauli ya Mkono ya kutamka wazi kwamba yupo tayari kufukuzwa kutoka CCM imemshitua Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye.
Alipoulizwa kama chama hicho kipo tayari kumpoteza mwanachama na mfadhili mahiri kama Mkono, Nape alianza kwa kukosoa taarifa zilizoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema zinalenga kuibua mjadala usiokuwapo.
"Nani kasema watahojiwa? Hoja hii ni kweli iliibuliwa kwenye kikao cha NEC kwa baadhi ya wajumbe kuhoji kwamba ilikuwaje wabunge wa CCM wakasaini kumng'oa madarakani Waziri Mkuu! Lakini tukaona kuwa hii ni hoja ya bungeni, na huko kuna party caucus. Uongozi wa Kamati ya Wabunge wa CCM upo, na haujatupatia taarifa rasmi kama kuna watu wamevunja kanuni.
"Tukasema kama wanaona kuna uvunjaji kanuni watujulishe. Nasema hii hoja inatengenezwa makusudi. Kama kulikuwa na tatizo, basi party caucus watatujulisha, lakini hadi sasa hatujapata taarifa rasmi. Wale wana kanuni zao za wabunge, kama wanaona kuna jambo linahitaji kufikishwa ngazi za juu wanalileta," amesema.
Alipoulizwa kama chama kinaweza kumwadhibu Mkono na wenzake, alisema, "Sipendi kuzungumzia mtu, hapa tunajadili kanuni na sheria. Tunaendesha chama kwa kanuni, sheria na taratibu, kama sheria zinasema Nape kakosea pamoja na umuhimu wake, sheria zitafuatwa. Nakuhakikishia katika hili hatujapata taarifa."
Nape: Maige si saizi yangu
Katika siku za karibuni, Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige (CCM), amenukuliwa akisema kwamba Nape ni gamba ndani ya CCM na anapaswa kuwajibishwa. Kwa upande wake, Nape amejibu mapigo kwa kusema, "Maige si saizi yangu, ni mbunge, atajibiwa na (CCM) wilaya yake. Nadhani wameshaanza kumjibu."
Filikunjombe: Wabunge hawafai
Kwa upande wake, Filikunjombe alipowasiliana na JAMHURI alisema yeye yuko tayari kufukuzwa kutoka CCM kama chama hicho kitamhukumu kuwa alifanya kosa kwa kutia saini azimio la kumg'oa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ila akasema uamuzi wa aina hiyo utamshangaza mno na unathibitisha unafiki wa wabunge wa CCM.
"Nimesikia walijadili suala hili kwenye NEC na Rais Kikwete akasema vikao vipo vingi, suala hili lipelekeni kwenye vikao husika kama party caucus bungeni.
"Mimi nasema sijutii uamuzi wangu. Tena nasema kama wapo wa kufukuzwa kutoka CCM ni wale waliokataa kusaini ndiyo waadhibiwe, kwa sababu huo ndiyo uliokuwa msimamo wa chama. Asilimia 90 au 95 ya wabunge walikuwa wanalalamika na tukakubaliana hivyo.
"Ajabu; ilipofika wakati wa kusaini daftari wengine wakawa wanalipita kama hawalioni. Wabunge wengi ni wanafiki sana. Ndiyo; tunapaswa kuwa na nidhamu lakini nidhamu ya woga haifai. Dhamira yangu iko safi kabisa, kwa hili nipo tayari kufukuzwa katika chama.
"Pamoja na kwamba ninaheshimu uamuzi wa vikao, ukweli utabaki pale pale kwamba nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.
"Hawa waliokataa kusaini ndiyo wa kufukuzwa maana walikuwa wanataka chama kianguke na serikali yake. Sasa itakuwa ajabu sisi tulioitetea serikali isiangushwe - tena serikali ya chama chetu - ndiyo tufukuzwe sitaelewa ila nipo tayari hata leo," amesema Filikunjombe.
Wabunge hao watatu waliungana na wabunge wa vyama vya upinzani vya Chadema, CUF, TLP na UDP kusaini azimio la kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, lililoandaliwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
Baada ya hatua hiyo, Serikali ililazimika kufanya mabadiliko makubwa kwenye Baraza la Mawaziri na mawaziri wanane na manaibu wawili kutupwa nje ya ulingo.