Mkoloni mtu hatare sana

Mto_Ngono

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
686
589
Nilipokumbuka ile hadithi ya kibanga kampiga mkoloni nikajiuliza kwa nini hakummaliza kabisa. Yapo mambo mengi katuletea au kuyafanya ambayo ukiyaangalia kwa nje ni mazuri kumbe yana ubaya sana hasa katika kutudhoofisha kimwili na kiakili. Nadhani tunamkumbuka sana mkoloni hadi kuona anafaa kuweka katika vitu mbalimbali ambavyo vinaweza kuwavuta watu karibu.

Suala moja tu ambalo najiuliza ni kwa nini katika project kubwa za ujenzi (haswa mall n.k) mabango mengi yanayoonesha picha ya jengo litakapokamilika hupambwa na wazungu!! picha katika mabango hayo huonesha watu kuingia na kutoka lakini watu hao wengi huwa ni rangi ya mkoloni. Hatuwezi kuweka watu kufanana na rangi zetu au hatujui thamani yetu na ya rangi yetu hadi tuwaweke wao ndani ya taifa letu!!

Please, wachora ramani badilikeni basi angalau tuone rangi zetu pale sio wakoloni tu. Wakoloni wabaya sana.
 
Nilipokumbuka ile hadithi ya kibanga kampiga mkoloni nikajiuliza kwa nini hakummaliza kabisa. Yapo mambo mengi katuletea au kuyafanya ambayo ukiyaangalia kwa nje ni mazuri kumbe yana ubaya sana hasa katika kutudhoofisha kimwili na kiakili. Nadhani tunamkumbuka sana mkoloni hadi kuona anafaa kuweka katika vitu mbalimbali ambavyo vinaweza kuwavuta watu karibu.

Suala moja tu ambalo najiuliza ni kwa nini katika project kubwa za ujenzi (haswa mall n.k) mabango mengi yanayoonesha picha ya jengo litakapokamilika hupambwa na wazungu!! picha katika mabango hayo huonesha watu kuingia na kutoka lakini watu hao wengi huwa ni rangi ya mkoloni. Hatuwezi kuweka watu kufanana na rangi zetu au hatujui thamani yetu na ya rangi yetu hadi tuwaweke wao ndani ya taifa letu!!

Please, wachora ramani badilikeni basi angalau tuone rangi zetu pale sio wakoloni tu. Wakoloni wabaya sana.
Kama unaongelea michoro ya kutumia software za archicard hakuna namna kwa urahisi unapoweka picha yoyote zinakuja zile zilizowekwa na wabunifu wa software hizo.
Wameweka picha za kizungu zaidi humo ndani, ukikerwa buni software yako uwauzie wachoraji
 
Hizo software kama Archcad na Autocad zote wametengeneza hao wakoloni kwahiyo hata picha za demo wanajiweka wao na watoto wao. Labda wewe Mto Ngono utusaidie kutengeneza tu software twakwetu ili kwenye picha uonekane wewe na ngozi yako
 
Tusipende kulia lia kama hatuna uwezo bali jikite kupambana ili uje na ubunifu wako
 
Kama unaongelea michoro ya kutumia software za archicard hakuna namna kwa urahisi unapoweka picha yoyote zinakuja zile zilizowekwa na wabunifu wa software hizo.
Wameweka picha za kizungu zaidi humo ndani, ukikerwa buni software yako uwauzie wachoraji

Duh! wameteka akili kabisa hata kutengeneza software zetu hatuwezi..
 
Mtu akiwa mkoloni anakuwa hana zuri hata moja, maana yeye anasababisha kitu, yeye anasaidia na yeye ndio mwenye kufaidika..!


Tuendelee kwenda na kasi ya ugunduzi wa Teknolojia mbali mbali. Ila hizi Teknolojia za mkoloni ipo siku itatufanya watumwa hasa Afrika,

Maana tumesahau misingi ya Waafrika wenzetu kama kina Mwl Nyerere, Gaddaf Bob Marley na wengine wengi, ambao walijitolea Kutuelimisha lakini hatukuelimika.

Pigo namba moja la Teknolojia ni ili laptop na kompyuta kuonyesha ni pigo la wote, Mapigo yanayo fata ni watu oheeehaee nahamanisha Afrika inatuhusu.

Mkoloni sio mtu mzuri kabisa, simpendi japo vitu vina rahisisha.
 
Labda mimi cjui, nikumbushe software moja iliyotengenezwa Tanzania/Africa na hajahusika mzungu

Mkuu ngoja waje wana sayansi wenda watatujuza hope wanaweza kuwa wanawafahamu wabongo waliounda software zao.
 
Mtu akiwa mkoloni anakuwa hana zuri hata moja, maana yeye anasababisha kitu, yeye anasaidia na yeye ndio mwenye kufaidika..!


Tuendelee kwenda na kasi ya ugunduzi wa Teknolojia mbali mbali. Ila hizi Teknolojia za mkoloni ipo siku itatufanya watumwa hasa Afrika,

Mana tumesahau misingi ya Waafrika wenzetu kama kina Mwl Nyerere, Gaddaf Bob Marley na wengine wengi, ambao walijitolea Kutuelimisha lakini hatukuelimika.

Pigo namba moja la Teknolojia ni ili laptop na kompyuta kuonyesha ni pigo la wote, Mapigo yanayo fata ni watu oheeehaee nahamanisha Afrika inatuhusu.

Mkoloni sio mtu mzuri kabisa, simpendi japo vitu vina rahisisha.
Ni kweli humpendi mkoloni lakini lifestyle yako ya leo ni ya kikoloni.
Walitukuta tukiwinda, hatuvai mavazi kama ya leo, hatukujua kusoma na kuandika.
Hivyo hata uwepo wa jf na wewe kujiunga ni matokeo ya ukoloni.
 
Mkuu ngoja waje wana sayansi wenda watatujuza hope wanaweza kuwa wanawafahamu wabongo waliounda software zao.
Kwa kifupi ulikuwa na nia njema lakini hukufanya utafiti na ukakimbilia kuwalaumu wabunifu wa majengo
 
fbb0c55591e63dae520b37f0f515b890.jpg
 
Back
Top Bottom