Mkoa gani ni nafuu kuishi kwa Tanzania?

Vladmir Putini

JF-Expert Member
Mar 22, 2022
777
1,442
Wakuu habarini za muda huu,
poleni kwa majukumu. Maisha yana changamoto espicially kwa vijana ila tusikate tamaa tuendelee kupambana.

Wakuu kama mada inavyojieleza, nilikuwa naomba ushauri wenu mnijuze ni mkoa/mji gani hapa Tanzania nikienda kuishi gharama zake za maisha walau zina afadhali/ziko chini tofauti na mikoa mingine?!

Nimekuja humu kwa sababu naamini kuna watu kutoka sehemu mbali mbali za Tanzania hii na wengine wameishi sehemu mbalimbali pia wana experience hiyo tayari.

Binafsi sijaishi sehemu nyingi sana Tanzania, nimeishi mikoa ya Singida (nilikozaliwa na kukulia), Arusha, Mwanza, na Zanzibar(Unguja) nilipo kwa sasa.

Sasa kwa hizi sehemu chache nilizo bahatika kuishi kuna baadhi ya sehemu hasa Arusha na Unguja gharama za maisha ziko juu mno, kuanzia room za kulipa kodi ili uishi, bidhaa za vyakula, mavazi yani ziko juu mno.

Mfano, room za kuishi kwa zanzibar chumba kawaida tu chenye umeme ni elfu mpaka 50 per month alafu ni cha kawaida sana na kidogo tu, chumba cha master (self contained room) ni mpaka elf 70+ mpaka laki moja per month.

Sasa kwa uchumi wangu kwa kweli haya maisha kwa huku naona kama magumu sana.


Sasa kama nilivyosema kwa sasa nipo Zanzibar(Unguja) ila nataka nikimbie nitoke huku kabisa, nna mtaji kama wa million 3 hivi nilikuwa naomba wadau mnishauri ni mkoa gani hapa Tanzania naweza ishi ambapo gharama za maisha zitakuwa za chini kidogo ambapo naweza kuanza maisha kwa hizo million 3.

Sehemu ambayo naweza fanya bishara ndogo ndogo, hata kama ni kilimo cha msingi maisha yaende tu.

NB: Nna 28 years, sijaoa kwa hiyo kuhama kwangu toka sehemu moja kwenda nyingine ni rahisi sana.

81fb935bb05a42249858cd0526fa1470_1.jpg
 
Moro (Sio jiji)
Mbeya
Tanga
Mkuu asante kwa ushauri wako.

Kuna mtu nilikuwa naongea nae mambo hayo hayo juzi hapa, alinambia kama ulivyo nambia wewe kwamba MBEYA na MOROGORO maisha ni cheap, bidhaa especially za vyakula ni cheap sana na kikubwa zaidi kanambia ardhi za hiyo mikoa miwili zina rutuba sana kama nawaza kujishughulisha na kilimo huko kunanifaa ndivyo alivyo nishauri.

Na kwa upande wangu, hiyo sehemu nnayotaka mimi siyo lazima iwe mjini sana, hata kama ni wilayani ila cha msingi ninachotaka taka miundo mbinu ya msingi iwepo (bara bara ya lami, minara ya simu kwa ajili ya mawasiliano,umeme pia) hivyo tu vitu vya msingi wangu.

Na pia kwa upande wa room vp kodi zake kwa mwezi wastani ani (overall)
 
1. Moro

nilipata ishi hapo tena mjini, chakula rahisi sana hali ya hewa ni nzuri mno, napapenda Moro

2000. Dodoma
ni pakicenge, chakula ghali labda kwakua ni jangwa
Moro town, wastani room ya master ni sh ngapi kwa mwezi mkuu
 
Sehemu rahisi pa kuishi Tanzania hii ambapo kila kitu ni nafuu ni Mwanza pekee.
Mwanza-nyama unapata hadi ya kufungiwa ya 100,dagaa,samaki,ndizi,maharage ,Michele vyote bure kabisa.
Gharama za kupanga chumba& nyumba zote zipo chini.Nguo,usafiri vyote simple.
Yeah ni kweli, nimewahi kuishi MWANZA kati ya 2015 to 2019.

Na niliipenda sana mwanza na mpaka leo naipenda especially manthari yake ya miamba, upepo mwanana wa ziwa Victoria, kwa kweli naipenda mwanza mpaka leo na sikuwahi kutegemea kama nitaihama mwanza ila kuna kibarua nilipata mahali nje ya mwanza ndiyo ikanifanya niimimbie mwanza.


Sehemu ambayo niliishi ni MALIMBE (mitaa ya chuo cha SAUT ), Nyamalango, NGANZA.

Na kule room nilikuwa nalipia elfu 50 kwa mwezi ila ilikuwa ni master room ya ukweli na unakuta imewekwa na kitanda cha 5 kwa 6 na godoro lake ndani we ukifika unahamia tu.

Na huko nilikokuwa naishi naambiwa ilikuwa ni mitaa ya chuo kwa hiyo room zilikuwa ghali, ila naskia mitaa kama nyegezi kona, mkolani, mkuyuni kule bado room naskia ulikuwa unaweza pata mpaka kwa elf 20 per month.

Lakini hofu niliyonayo ya kurudi mwanza sasahivi ni kwamba naona mtaji wangu ni mdogo sana kwa ule mji .

Japo mimi hata kama lucheche naweza ishi ila cha msingi tu eccessibility ya kufika town iwe rahisi.
 
Dsm ni cheap zaidi mana dsm in maeneo ya masikini wakutupwa na matajiri sana..niwewe tu na uwezo wako dsm manzese unapata chumba cha buki 20..msosi kama kawa miguu ya kuku na utumbo ugari wa jero maisha yanasonga.

#MaendeleoHayanaChama
 
Dsm ni cheap zaidi mana dsm in maeneo ya masikini wakutupwa na matajiri sana..niwewe tu na uwezo wako dsm manzese unapata chumba cha buki 20..msosi kama kawa miguu ya kuku na utumbo ugari wa jero maisha yanasonga.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Naheshimu mawazo yako ila DAR hapana mkuu.

Dar ni jiji ambalo lishakuwa kubwa sana na lina mambo mengine sana, kifupi sipendelei kuishi sehemu yenye population kama ya dar.

Na kikubwa zaidi mimi nataka sehemu/mkoa ambao baadae nikifanikiwa kwa mtaji wangu mdogo baada ya miaka 5 au 6 ikifika hata milion 15 au 20 niweze kujenga hata kijumba changu cha room 4 au 5 simple tu maisha yakaenda.

Maana naamini kuna baadhi ya mikoa hapa tanzania bado unaweza kupata kiwanja kwa milion 2 mpak 5 tofauti dar ambapo hiyo pesa si chochote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom