From Sir With Love
JF-Expert Member
- Sep 13, 2010
- 2,076
- 3,797
Narudia tena. Hii mada kama wanao hawasomi pale huwezi kuielewa.Kama hautakuwa na ujamaa na huyo mtuhumiwa, basi wewe utakuwa huyo mtuhumiwa.
Sisi wengine hatuna interest sana na hiyo feud inayoendelea baina yenu humo ndani, tuachotaka kujua ni kama David anazo sifa au hana?
Wewe ndiyo umeleta mada. Ungeuliza kwanza waliomwajiri kwa kuchukua taarifa za sehemu zote.Bora umenisaidia maana naona ananichosha tu
Anachanganya mada, ilitakiwa ajibu au aeleze kuwa mtu wake anasifa za kuongoza shule hizo
Mada huijui, ungeijua usingekuwa unauliza maswali ya kutafutiwa.Huyu anajaribu kutufanya vilaza kwa kubadili topic kijanja kwa matarajio kuwa tutaacha kufocus kwenye mada kuu.
Na subiri, watakuja tu.Nenda Kenya ukiwa Mtanzania, ushike nafasi ya kawaida sana huku ukiwa huna sifa halafu umiliki vimalimali kama alivyotaja Pdidy hapo juu uone kitakachokutokea. Usichukulie mambo kirahisi ukisweep conclusions kwa assumptions zisizo na uzito!
Swali la msingi ni kweli hana sifa.Tusibadishe goli,hayo mengine si yamesharekebishwa?Mleta mada, unaonekana una hasira sana baada ya kufukuzwa kazi hapo shuleni kwa sababu ya kula ada bila kupeleka ofisini.
St. Columba's ilikuwa ni shule bora za English medium, japo kwa sasa imedoda kwa sababu ya watu kama nyie.
Shule ni ya kanisa, lakini mlikuwa mnachukua rushwa kusajili watoto.
Mlikuwa mnachukua ada kutoka kwa wazazi kama cash na kuzila badala ya kumwambia mzazi apeleke bank. Mbaya zaidi mlikuwa mnatoa risiti fake.
Juzi tu wala rushwa wote wamefukuzwa kazi hapo shuleni, sasa mnalialia kwenye mtandao.
Maisha ni sehemu yoyote ile sio lazima hapo shuleni.
Binadamu bwana.
Akina nani..!? maana Mwenyekiti wa Bodi ya Shule Veronica Msinjili alipoulizwa alisema hajui na alipopigiwa Simu mwenyewe Wathiga hakupokea Simu.. huoni kuwa kuna kubebana hii issueWewe ndiyo umeleta mada. Ungeuliza kwanza waliomwajiri kwa kuchukua taarifa za sehemu zote.
Do your home work na uache porojo.
Huyo Mkenya anashikiliaje nafasi wakati hana sifa za kuishikilia? Hilo ndilo swala la msingi.Na subiri, watakuja tu.
Kama siasa mnaingiza kwenye elimu mnategemea nini?
Juzi tu hapa mlisema mwenye diploma kuingia chuo lazima awe na GPA ya 3.5 baadaye mlivyoona haiwezekani mkashusha mpaka 3.0.
Vigezo vya wenzetu wanajumuiya Africa mashariki vikoje?
Anakuja mtu hapa kutoka Uganda au Kenya ana degree yake ambayo ameipata kwa kupitia form 4, lakini kwa sababu huyu Mtanzania hakwenda form six sasa hivi mnasema haruhusiwi kwenda chuo kupitia form 4.
Baadaye mnakuja hapa kulalama vigezo vya kuajiriwa.
Kila siku matamko tu. Kila siku kulalama.
Hiyo hainifanyi kutokuelewa kuwa ajira ya mtu hulindwa na qualifications. Upo? Leta jingine la kuutetea huu upuuzi lakini siko blah blah ulizoandika hapo juu!Huelewi unachosema. Kama wanao hawasomi pale, huwezi kujua kinachoendelea hapo.
Nikawaulize nini? Kwamba kapewa nafasi kwa upendeleo au kaingizwa kwa qualifications za kufoji au kwanini hajatimuliwa mpaka sasa pamoja na watu kuhoji tayari?Narudia tena. Hii mada kama wanao hawasomi pale huwezi kuielewa.
Hayo maswali kawaulize waliomwajiri au mleta mada.
Wewe ndie unaepaswa kutupatia mwanga juu ya uwezekano wa mtu huyo kupewa nafasi akiwa hana sifa maana unaonekana unajua zaidi hili swala. Ukweli unabaki pale pale kuwa huyo jamaa hastahili kushika hiyo nafasi kama hana qualifications labda wewe ulete proof ambayo ni valid inayoopose hizi accusations, zaidi ya hapo ni kwamba hizi tuhuma ziko justified maana mtuhumiwa hajatoa utetezi wowote na hapokei simu.Mada huijui, ungeijua usingekuwa unauliza maswali ya kutafutiwa.
Katafute majibu mwenyewe. Sifa nikuambie mimi, mimi ndiyo nimemuajiri?
Wewe ndie unaepaswa kutupatia mwanga juu ya uwezekano wa mtu huyo kupewa nafasi akiwa hana sifa maana unaonekana unajua zaidi hili swala. Ukweli unabaki pale pale kuwa huyo jamaa hastahili kushika hiyo nafasi kama hana qualifications labda wewe ulete proof ambayo ni valid inayoopose hizi accusations, zaidi ya hapo ni kwamba hizi tuhuma ziko justified maana mtuhumiwa hajatoa utetezi wowote na hapokei simu.
Kha! Kuhusiana na ngono na dhuluma ni kweli maana ni vitu sensitive sana kama kuna ukweli na anaeviendekeza anastahili kuchukuliwa hatua haraka sana. Lakini tunarudi palepale, ni kwa vipi mtu asie na qualifications akashikilia nafasi asiyostahili? Achana na swala la propaganda, hilo nalo ni equally sensitive kama ilivyo tu ngono na dhuluma katika eneo la kazi.Hizi ni propaganda uchwara baada ya kazi kuota mabawa.
Hata kama aliishia la saba, kuwafanya wachache waliokuwa wanaharibu shule kuondoka ni bora mara mia kuliko kuwa na mzalendo academic ambaye anawaza ngono na dhuluma.
Kweli? Yaani haya mambo imefika wakati tuyatolee macho maana tulikaa kimya kwa muda mrefu mpaka tukageuzwa kuwa gunia la mazoezi ambalo kila asiejua kurusha ngumi anakuja kujifunzia. Matokeo yake tunaletewa vihiyo wa kila aina am,bao hawatusaidii lolote katika juhudi za kusonga mbele.Wabongo wakiona mtu anazungumza kiingilish wanapagawa wako wakenya wanapata ajira nzuri kwa njia hiyo .Kuna mkenya mmoja alijifanya mwalimu alikua na kazi ya kuvishika maziwa vitoto vya primary mpaka walipomng'amua wakamtoa nduki.
Mambo serious kama haya yanatokea halafu mtu anasema ni propaganda dhidi ya wageni,kweli? Inaudhi sana.Shule ya St. Columba's campus ya Upanga ni shida tupu. Mm watoto wangu watatu walikuwa wakisoma hapo, nimewahamisha kutokana na matatizo ya kiutendaji wa hiyo shule. Shule ina location nzuri ila hupati thamani ya pesa yako na madarasa utadhani ni mabanda ya kuku.
Huyo mkuu wa shule David Wathiga ndio source ya matatizo yote, uwezo wake wakuendesha shule na kusimamia walimu ni mdogo sana. Hata ukimpelekea malalamiko tena sensitive hupati feedback na pia halifanyiwi kazi anabaki kukuitikia tu vizuri.
Shule haina mabasi yake na anaetoa huduma ya usafiri ana mabasi mabovu kila siku spana mkononi.
Mabasi yanakuwa na watoto na dereva tu bila ya escort ya mwalimu au mtu responsible.
Walimu wana uwezo mdogo kwenye masomo wanaofundisha, wanawakosesha watoto kwenye mitihani ukiwasahihisha wanajenga chuki na mwanao mfano Teacher Hadija wa Grade one alimfinya mwanangu wa miaka sita karibu na sehemu zake za siri mpaka akatoka alama iliyodumu kwa zaidi ya wiki, Tr. Hadija nilipolalamika alijibu kuwa mwanangu atakuwa ameichoka shule na David Wathiga akiwa ni mwalimu mkuu hakichukuwa hatua yoyote.
Usimamizi wa watoto wanapokuwa shule ni mdogo sana hadi watoto wanabakana vyooni.
Walimu hawana wito, ukimpeleka mtoto na dawa kama yupo kwenye dose mtoto anaambiwa ungebaki kwenu, wakati watoto kila mara wanauguuwa UTI kutokana na vyoo vichafu havina maji yanayotiririka na hata sabuni yakunawia mikono chooni na kwenye dining room hamna.
Unalipia pesa ya swimming ya term, watoto wataenda ku swim hardly mara tano kwa term yote.
Chakula hakiridhishi, na kikibaki kinachanganywa na siku ya pili.
All in all hata performance ya shule kwenye mitihani ya taifa inaendelea kushuka mwaka hadi mwaka.
As a parent sikuwa naweza kurelax kabisa wakati wanangu walivyokuwa wakisoma kwenye hiyo shule. But now, i have found a good school, it's not perfect but it's a big step up from St. Columba's school.
Kwa hiyo shule inahitaji a change of leadership to begin with ndio mengine yatafuata.
Ni kweli inaudhi. Anaesema ni propaganda hajui uchungu wa mwana. Pata picha mwanao anabakwa na kundi la watoto wenzie akiwa shuleni.Mambo serious kama haya yanatokea halafu mtu anasema ni propaganda dhidi ya wageni,kweli? Inaudhi sana.
Kha! Unasubiri nini kushitaki? Imeniuma sana aisee, unaweza kupata kesi ya mauaji kimzahamzaha hivihivi!Ni kweli inaudhi. Anaesema ni propaganda hajui uchungu wa mwana. Pata picha mwanao anabakwa na kundi la watoto wenzie akiwa shuleni.
Note: kwenye results za 2016 kuna phrase inasema "kwenye kundi lake". Therefore mwaka huu kulikuwa na mgawanyo katika makundi madogo zaidi kutokana na idadi ya candidates, that is why inaonekana kama kupanda kidogo kulinganisha na 2015 and 2014. Na ndio maana kitaifa kwenye kundi laki idadi ya shule ni kwenye elfu 8 but shule kitaifa ni zaidi ya hizo.Wakuu,
Nimeweka screenshot za matokeo ya shule hii kwa miaka mitatu iliyopita.
Nadhani tuache hisia bila uhalisia...
Tafakari.