Mke wangu hanipi unyumba...

Mke wangu hanipi unyumba...

Benjonathantz

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2014
Posts
237
Reaction score
52
Muda mwema utawale kwako!

Katika Maisha yangu nimekutana na mambo mbalimbali na hili likiwa moja wapo.

Kwa kufanya huduma za Injili maeneo mbalimbali hapa nchini. Imenipa fursa ya kuyajua matatizo mengi ya ajabu ajabu.

Moja ya mambo hayo ni wanawake wasiojisikia kuwapa unyumba waume zao kwa Muda mrefu. Kwa mtazamo wangu nilidhani ni jambo dogo tu lakini siku zinavyozidi kwenda. Nakutana na watu wengi wenye tatizo hilo.

»Siku moja nilikutana na Mwanamke mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa alikuwa hajisikii kumpa mumewe unyumba kabisa na alitufuata kwa ajili ya Ushauri.
Hatukutaka kumshauri chochote kabla ya kumsikia mumewe akikiri tatizo hilo.
Mumewe alikiri tatizo hilo akisema "MKE WANGU HANIPI UNYUMBA" .. Alitusihi tumpatie maombi na ushauri ili mkewe afunguliwe kutoka katika Tatizo hilo.

Basi bila kuchelewa tuliliita jina la Yesu na ghafla yule mwanamke akaangushwa na mapepo na yakaanza kutamka wazi wazi kuwa yamefunga ndoa na mwanamke yule na hakuna ataye ifunja ndoa hiyo. Hatukukata tamaa mana tulitambua ni kelele za shetani tu. Mungu alimponya mwanamke yule kutoka katika vifungo vya shetani.

Kuna watu wengi wana matatizo kama haya, Wengine Wanaota ndoto mbaya wakifanya mapenzi na wengine wanakosa hadi watoto katika kipindi cha ndoa.

Kama una tatizo kama hilo Dawa ni Damu Yesu Bila kukunja maneno!!
 
". . .Peaneni....msinyimane...." neno la MUNGU ktk kitabu cha 2 Korintho 7 linatanabaisha!.

Pepo la kunyimana lishindwe!!
 
Wengine hupona kwa damu za kuku na hushukuru na uponyaji huo.
 
Jina Yesu ni jina lililo na nguvu ya ajabu sana yaani ni ukitaja tu mapepo yanaanza kuondoka.."......Mwana wa Adamu alidhihirishwa ili azivunjevunje kazi za ibilisi"
 
Aombe talaka huyo mwanamke.

Sio kwamba anapenda hali hiyo bali ni Bahati mbaya tu anajikuta yupo katika hali hiyo... Hivyo dawa yake halali sio talaka. Dawa yake ni Maombi ya kutosha yatakayoleta uponyaji.
 
Nyani_ngabu umesema sahihi kbs
 
Last edited by a moderator:
Wewe kwa post zako,
Labda akuombee spidi gavana ya kupunguza unyumba
 
Sipati Picha gemu ya siku hio ilikuaje baada ya Madame kufunguliwa....nadhani watoto walisafirishwa kwa bibi yao.....hicho kitanda lazima kesho kiliitiwa fundi akitibu. Hongera kwa maombi, umeokoa ndoa

CC: MANI zumbemkuu


​@kyanakyomuhaya
 
Sipati Picha gemu ya siku hio ilikuaje baada ya Madame kufunguliwa....nadhani watoto walisafirishwa kwa bibi yao.....hicho kitanda lazima kesho kiliitiwa fundi akitibu. Hongera kwa maombi, umeokoa ndoa

CC: MANI zumbemkuu kyanokyomuhaya

Mpwa haya makubwa.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom