Bro skia nikwambiee
Achana na huyo mwanamke atakutesa sana
Usijdanganye kuwa atabadilika,that will never happen
Usiendelee kuwa nae kwa sababu eti unaonea watoto huruma,watoto watakua tu
Nimekulia kwenye familia yenye migogoro tangu nipo chekechea nashuhudia wazazi wangu wanagombana mara kwa mara mpaka Leo hii ni ugomvi kila kukicha na chanzo cha ugomvi ni bimkubwa wangu
So mzee akawa na point kama yako eti wakiachana mimi nitapata tabu kukua bila wazazi wawili
Hilo ni bonge La mistake alilofanya mzee wangu kuendelea na bimkubwa wangu ili tu mimi nipate malezi ya baba na mama
Matokeo yake sasa
Mpaka leo hii ni ugomvi kwenda mbele hamna amani
Kama ningekua na uwezo ningewatenganisha lakini ndoa yao Mimi hainihusu nadeal na mambo yangu
Nina uhakika hata hao watoto wako wangekua na ufahamu na kujua unachopitia wangekuruhusu uachane na huyo mwanamke
Kama unapenda watoto wako wasiathirike kisaikolojia kutokana na ugomvi wa wazazi ni bora ukaachana na huyo mwanamke wako mapema kuliko waendelee kushuhudia ugomvi wa wazazi kila kukicha lazima wata athirika kisaikolojia
Mimi ni mhanga wa migogoro ya wazazi naelewa ninachokisema
Kazi ni kwako bro