Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Kauli kama hii hutoka vinywani mwa wanaume wengi. Lakini, je, unajua ni kwa kiasi gani kauli hii huwa haina ukweli hata chembe? Huenda hujui kabisa, au inawezekana pia nawe ni mmoja kati ya wale wanaowalalamikia wenza wao kuwa hawawaelewi.
Wanaume mara nyingi sana ndio mashujaa wa kudai kwamba wake zao au wapenzi wao hawawaelewi na hivyo kuwatupia mzigo pale uhusiano unapovunjika. Lakini ukweli ni kwamba wanaume ndio ambao huwa hawawaelewi wanawake kwenye uhusiano.Mara nyingi wanaume wanakuwa tayari wameweka kichwani dhana kwamba wanawake ni tatizo-hawaaminiki, wanasumbua, wana wivu wanapenda kukalia wanaume wakipewa nafasi na mengine ya aina hiyo. Dhana hizo zinakuwa zimejijenga kutokea utotoni katika malezi na katika mazingira anamokulia. Kumbuka mfumo-dume ndiyo unaoongoza duniani.
Kwa hiyo mwanamke anaposema ‘A' mwanaume kutokana na kuwa tayari ameshamhukumu mwanamke, huwa anasikia ‘B' na hivyo hujibu ‘C' na hapo ndipo matatizo ya mawasiliano yanapoanzia. Mwanamke anaweza kujaribu tena kutaka kufikisha ujumbe anaotaka kuufikisha kwa mumewe, lakini safari hii atakuwa na hasira. Mumewe naye atapandisha hasira kwa sababu hajui ni kwa nini aambiwe jambo kwa hasira, na hapo ndipo kisirani kinapoanzia.
Ni wazi wengi wetu tumeshawahi kusikia wanawake wanaolalamika, ‘ndugu yangu mimi sijui nifanyeje, kitu kidogo mtagombana wee hadi unajiona huna maana…..' Lakini miongoni mwetu wanawake wanaweza pia kuwa mashahidi wa hali hii, kwamba, wanapojitahidi kuelezea hisia zao kwa upendo, wanaume wanakuwa wakali bila sababu hadi wanafikia mahali ambapo kila siku kuna malumbano ndani ya nyumba. Haya ni matokeo ya wanaume kushindwa kujua namna ya kuwasliana na wake au wapenzi wao.
Kuna haja ya wanaume kujua kwamba, kuwasikiliza wake zao kwa umakini na kuwaelewa ni sehemu muhimu sana katika kukamilsha uanaume wao. Tatizo la wanaume wengi ni kushindwa kwao kutofautisha kati ya kuwasikiliza wake au wapenzi wao na kuwakubalia. Wanadhani wakiwasikiliza kwa makini itakuwa ni sawa na kuwakubalia, hivyo wanapoona wanaongea jambo ambalo wao hawakubaliani nalo huacha kuwasikiliza, kuwakatisha au kuwaponda kwa njia ya kebehi na dharau. Wanachoshindwa kujua ni kwamba, mara zote wanawake huhitaji kusikiliizwa na siyo kukubaliwa mawazo yao au hisia zao.
Wanaume mara nyingi sana ndio mashujaa wa kudai kwamba wake zao au wapenzi wao hawawaelewi na hivyo kuwatupia mzigo pale uhusiano unapovunjika. Lakini ukweli ni kwamba wanaume ndio ambao huwa hawawaelewi wanawake kwenye uhusiano.Mara nyingi wanaume wanakuwa tayari wameweka kichwani dhana kwamba wanawake ni tatizo-hawaaminiki, wanasumbua, wana wivu wanapenda kukalia wanaume wakipewa nafasi na mengine ya aina hiyo. Dhana hizo zinakuwa zimejijenga kutokea utotoni katika malezi na katika mazingira anamokulia. Kumbuka mfumo-dume ndiyo unaoongoza duniani.
Kwa hiyo mwanamke anaposema ‘A' mwanaume kutokana na kuwa tayari ameshamhukumu mwanamke, huwa anasikia ‘B' na hivyo hujibu ‘C' na hapo ndipo matatizo ya mawasiliano yanapoanzia. Mwanamke anaweza kujaribu tena kutaka kufikisha ujumbe anaotaka kuufikisha kwa mumewe, lakini safari hii atakuwa na hasira. Mumewe naye atapandisha hasira kwa sababu hajui ni kwa nini aambiwe jambo kwa hasira, na hapo ndipo kisirani kinapoanzia.
Ni wazi wengi wetu tumeshawahi kusikia wanawake wanaolalamika, ‘ndugu yangu mimi sijui nifanyeje, kitu kidogo mtagombana wee hadi unajiona huna maana…..' Lakini miongoni mwetu wanawake wanaweza pia kuwa mashahidi wa hali hii, kwamba, wanapojitahidi kuelezea hisia zao kwa upendo, wanaume wanakuwa wakali bila sababu hadi wanafikia mahali ambapo kila siku kuna malumbano ndani ya nyumba. Haya ni matokeo ya wanaume kushindwa kujua namna ya kuwasliana na wake au wapenzi wao.
Kuna haja ya wanaume kujua kwamba, kuwasikiliza wake zao kwa umakini na kuwaelewa ni sehemu muhimu sana katika kukamilsha uanaume wao. Tatizo la wanaume wengi ni kushindwa kwao kutofautisha kati ya kuwasikiliza wake au wapenzi wao na kuwakubalia. Wanadhani wakiwasikiliza kwa makini itakuwa ni sawa na kuwakubalia, hivyo wanapoona wanaongea jambo ambalo wao hawakubaliani nalo huacha kuwasikiliza, kuwakatisha au kuwaponda kwa njia ya kebehi na dharau. Wanachoshindwa kujua ni kwamba, mara zote wanawake huhitaji kusikiliizwa na siyo kukubaliwa mawazo yao au hisia zao.