Mke wangu hana nidhamu?

Mke wangu hana nidhamu?

Snipper

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
1,336
Reaction score
2,173
Mimi nina mke na tuna mtoto mmoja. Lakini tangu nimemuoa huyu mwanamke maka mitatu iliyopita hajawahi hata siku moja kunikaribisha kwenda kuoga maji bafuni kwa adabu ambazo mimi nimekuwa nikiziona katika maeneo mengine. Kwa mfano anaweza kuandaa maji bafuni na kuniambia...nyanyuka ukaoge maji yako bafuni...hivi ina maana anshindwa kusema maneno kama karibu mme wangu ukaoge maji yako tayari bafuni? Hata kwa chakua hali ni hiyohiyo.
Kutokana na hili pamoja na mengine nimekuwa nikimchukulia kuwa hana adabu kwa mme wake au nakosea wadau?
Naombeni msaad wenu nifanye ninikumfanya anitendee ninavyopenda kutendewa maana nikimwambia kuwa sifurahii jinsi anavyonifanyia anaonekana kunishangaa tu na kuishia kunilaumu eti labda nina visa vingine tofauti na hilo!
ifanye nini ndugu zangu? naomba mnishauri tafadhali!
 
Kumbe mimi nina bahati sana, nakaribishwa mpaka raha.
 
Tafuta nyumba ndogo chai utanywea bafuni utaogeshwa utasuguliwa utapakwa mafuta itachanwa nywele kila huduma unayokosa kwa mkeo hapo utaipata Mara Tatu yake
 
Mkuu umeoa kabila gani? kuna baadhi ya makabila wanawake wao hawana hali ya unyenyekevu kabisa.
nimeoa mtu wa manyara....mbulu, mbona dada zake wanaonekana wana heshima? hata kama hayupo wao wakinitengea maji bafuni utasikia wanasema..''shem kaibu maji bafuni'' lakini yeye mwenye mali utasikia anafyatuka ''nyanyuka ukaoge wengine wanataka kuoga utawachelewesha'' basi mi namwangalia simumalizi!
 
Mawasiliano madogomadogo ndani ya nyumba yanaweza kuvunja ndoa au yasivunje,kukawepo na usaliti au usiwepo.Mfano unaomba chakula, unanyooshewa mguu "kile pale"halafu upate nyumba ndogo anaejua majukumu,atasoma namba na kubaki kulaumu.
 
Tafuta nyumba ndogo chai utanywea bafuni utaogeshwa utasuguliwa utapakwa mafuta itachanwa nywele kila huduma unayokosa kwa mkeo hapo utaipata Mara Tatu yake
nilishampa hiyo tahadhali akasema labda nitakuwa nimeamua tu maana hiyo siyo sababu ya kuweza kunipeleka huko!...nashindwa kumuelewa kabisa!
 
dah! ngoja tu nitumie sehem ndogo ya hekima yangu manake ningegeuza side B pasingetosha.

jibu jepesi ni kwamba mkeo hajazoea hayo unayoyataka kufanyiwa, hivyo kumlazimisha inakuwa kero kwake. nakushauri kama unapenda hayo uliyoyasema basi mwonyeshe mfano siku moja chukua maji tia wenye ndoo mwambie mke wangu mpenzi karibu tukaoge, najua atakwenda kuoga lazima mkisha maliza una mwambia basi mwenzio ukinifanyia hivi nitafurahije?? napenda kubembelezwa mm na kutamkiwa maneno ya ukarimu namna hii. siku hiyo hiyo ataanza kukuambia.

alternatively weka maji ya shower bafuni kwako, hutohitaj kuwekewa maji ni kiasi cha wewe kuingia na kufungua bomba tu.
 
Kama ishu ni maji ya kuoga tu, si uweke mabomba bafuni?

Na akikucheat si utamla alive?

Culture, culture, culture!
hapa tunapoishi tumepanga chumba na sebule na hakuna namna ya kuweka bomba bafuni...kuhusu kucheat..kwangu hilo ni kosa ambalo halisameheki maana hata mimi njitahidi kuliepuka!
 
Kaka makabila ya kaskazini Tanzania, kanda ya kati na hata ya Pwani kidogo inabidi mwanaume uwe mvumilivu haswa kama watokea mikoa kinyume na hiyo.
Mathalani, kabila kama la Kingoni kawaida mwanamke hujinyenyekeza kwa mwanaume kwa kupiga magoti wakati wa salamu, ukaribisho wa chakula n.k lakini hilo ni kinyume kwa makabila ya kaskazini. Kukaribishwa mezani wakati mwingine huwa Kijeshi jeshi.
Sasa "mbwa uliyemzoea ndiye unayeweza kuishi naye". Yakupasa umzoee mkeo kwa kadiri na namna alivyo huku ukitambua kuwa makabila ya huko hayana baadhi ya gestures kama yalivyo makabila mengine.

nimeoa mtu wa manyara....mbulu, mbona dada zake wanaonekana wana heshima? hata kama hayupo wao wakinitengea maji bafuni utasikia wanasema..''shem kaibu maji bafuni'' lakini yeye mwenye mali utasikia anafyatuka ''nyanyuka ukaoge wengine wanataka kuoga utawachelewesha'' basi mi namwangalia simumalizi!
 
naomba pia ugeuze na side B tafadhali gfsonwin. hiyo njia uliyonishauri naona kama inaweza kusaidia mno!
dah! ngoja tu nitumie sehem ndogo ya hekima yangu manake ningegeuza side B pasingetosha.

jibu jepesi ni kwamba mkeo hajazoea hayo unayoyataka kufanyiwa, hivyo kumlazimisha inakuwa kero kwake. nakushauri kama unapenda hayo uliyoyasema basi mwonyeshe mfano siku moja chukua maji tia wenye ndoo mwambie mke wangu mpenzi karibu tukaoge, najua atakwenda kuoga lazima mkisha maliza una mwambia basi mwenzio ukinifanyia hivi nitafurahije?? napenda kubembelezwa mm na kutamkiwa maneno ya ukarimu namna hii. siku hiyo hiyo ataanza kukuambia.

alternatively weka maji ya shower bafuni kwako, hutohitaj kuwekewa maji ni kiasi cha wewe kuingia na kufungua bomba tu.
 
Last edited by a moderator:
wanaume bwana mnaboajeeee
utajijuuuu and u wil keri uaself we huwezi kuweka??kama ameshindwa kukwambia jiambie mwenyewe kimoyomoyo
 
asante sana kwa kunishauri ndugu yangu maana nahisi kama sitendewi haki!
Kaka makabila ya kaskazini Tanzania, kanda ya kati na hata ya Pwani kidogo inabidi mwanaume uwe mvumilivu haswa kama watokea mikoa kinyume na hiyo.
Mathalani, kabila kama la Kingoni kawaida mwanamke hujinyenyekeza kwa mwanaume kwa kupiga magoti wakati wa salamu, ukaribisho wa chakula n.k lakini hilo ni kinyume kwa makabila ya kaskazini. Kukaribishwa mezani wakati mwingine huwa Kijeshi jeshi.
Sasa "mbwa uliyemzoea ndiye unayeweza kuishi naye". Yakupasa umzoee mkeo kwa kadiri na namna alivyo huku ukitambua kuwa makabila ya huko hayana baadhi ya gestures kama yalivyo makabila mengine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom