nitonye
JF-Expert Member
- Dec 18, 2011
- 7,349
- 3,904
Ndugu wanajamvi.
Ndoa yangu imekuwa na mtikisiko kidogo ambao kwa kiasi fulani unanipa shida hivyo nakuona kama vile mke wangu hanifai kwa sasa.
Anaonekana ana tatizo la kisaikolojia na hivyo kugeuza jambo lolote analoambiwa kuwa negative yaani kila jambo analiona kwa mtazamo hasi.
Mfano anaweza kuwa amekosea then nikamwambia mke wangu hapa umekosea basi yatatoka maneno kumi, yaani mimi namnyanyasa, na mengine mengi.
Mwanzoni nilikuwa nachukia mpaka nampiga lakini nilivyoona bado hajirekebishi nakaanza kutafuta nini chanzo hasa,
nikajaribu kuchunguza pengine ameanza kuchepuka hakuonekana hivyo.
Pengine marafiki zake wanamjaza ujinga nikagundua hapana. Nikajaribu kufuatilia historia yake vizuri jinsi alivyo zaliwa na jinsi alivyolelewa.
Nilichokigundua wazazi wake yaani mama baba walifariki akiwa mdogo sana na hivyo kuishi na shangazi yake, lakini shangazi yake akawa anatreat vibaya hata na ndugu wengine wakawa kama vile hawamthamini
Aliamua kutoka kwa shangazi yake kwa kukimbia na kwenda kuishi kwa mama yake mdogo.
Lakini nako kukawa hivyo hivyo.
Sasa amekuwa hivyo kwenye akili akajijengea kwamba yeye hakuna wa kumthamini, hata ni kimkosea anatoa maneno ya kukata tamaa hivyo lakini namuomba msamaha then anakuwa sawa.
Naombeni ushauri nini nifanye maana kumpeleka kwa wanasaikolojia nahisi ataona kama nimetoa mambo yake nje. Anasumbuliwa na kitu asichokijua yeye.
Ndoa yangu imekuwa na mtikisiko kidogo ambao kwa kiasi fulani unanipa shida hivyo nakuona kama vile mke wangu hanifai kwa sasa.
Anaonekana ana tatizo la kisaikolojia na hivyo kugeuza jambo lolote analoambiwa kuwa negative yaani kila jambo analiona kwa mtazamo hasi.
Mfano anaweza kuwa amekosea then nikamwambia mke wangu hapa umekosea basi yatatoka maneno kumi, yaani mimi namnyanyasa, na mengine mengi.
Mwanzoni nilikuwa nachukia mpaka nampiga lakini nilivyoona bado hajirekebishi nakaanza kutafuta nini chanzo hasa,
nikajaribu kuchunguza pengine ameanza kuchepuka hakuonekana hivyo.
Pengine marafiki zake wanamjaza ujinga nikagundua hapana. Nikajaribu kufuatilia historia yake vizuri jinsi alivyo zaliwa na jinsi alivyolelewa.
Nilichokigundua wazazi wake yaani mama baba walifariki akiwa mdogo sana na hivyo kuishi na shangazi yake, lakini shangazi yake akawa anatreat vibaya hata na ndugu wengine wakawa kama vile hawamthamini
Aliamua kutoka kwa shangazi yake kwa kukimbia na kwenda kuishi kwa mama yake mdogo.
Lakini nako kukawa hivyo hivyo.
Sasa amekuwa hivyo kwenye akili akajijengea kwamba yeye hakuna wa kumthamini, hata ni kimkosea anatoa maneno ya kukata tamaa hivyo lakini namuomba msamaha then anakuwa sawa.
Naombeni ushauri nini nifanye maana kumpeleka kwa wanasaikolojia nahisi ataona kama nimetoa mambo yake nje. Anasumbuliwa na kitu asichokijua yeye.