Mke wangu ana hoja au ni uoga wake tu?

Mke wangu ana hoja au ni uoga wake tu?

Yaleyale

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
1,797
Reaction score
2,410
Habari za weekend wanajamvi,

Nimepangiwa kusimamia kazi fulani njiani Arusha kwa muda wa miezi 10. Ili kupunguza gharama nimeona ni vyema nikapanga nyumba badala ya kuishi hotelini. Nimemwambia mke wangu kuwa nafikiria kutafuta msichana wa kazi kwa kuja mchana na kuondoka jioni. Kazi zake zitakuwa ni kupika na usafi.

Mke wangu hajahafiki kwa madai kuwa wasichana wengi wako desperate kupata wanaume na hasa ndoa hivyo nitakuwa nahatarisha ndoa yetu. Anadai mabinti wanaweza kufanya chochote na hasa kwenye chakula nikaja kujuta.Anadai nijipikilishe na kama siwezi nile hotelini. Kuhusu usafi wa ndani na kufua anadai nifanye tu mwenyewe.

Jambo ambalo naona ni gumu sana. Nimemwambia naweza kumtumia mchungaji wetu ambaye amehamia Arusha miezi kadhaa iliyopita anitafutie msichana anayejiheshimu ndani ya kanisa lakini bado hataki.
Mke wangu ana hoja au ni fear of the unknown?


Ushauri wenu wanajamvi
 
Mkeo ana hoja ya msingi. wanaume ni wadhaifu sana mbele ya mwanamke hata awe house girl hasa ikiwa mkewe yupo mbali kama ilivyo kwako. Kama upo serious na unataka kuepuka vishawishi na migogoro isyo ya lazima tafuta house boy au mlete mkeo huko arusha
 
Mkeo ana hoja ya msingi. wanaume ni wadhaifu sana mbele ya mwanamke hata awe house girl hasa ikiwa mkewe yupo mbali kama ilivyo kwako. Kama upo serious na unataka kuepuka vishawishi na migogoro isyo ya lazima tafuta house boy au mlete mkeo huko arusha

haswa kwa nn binti wa kike? mbn wa kiume pia wapo. huyo mkeo naungan naye kabisa ucthubut kufany hivo
 
Da! nimecheka tu, achana na msichana wa kazi, msikilize mkeo, aisee
 
samahani nipo nje ya mada hivi KUJIPIKILISHA ni kiswahili fasaha ?
 
Mkeo ana hoja ya msingi. wanaume ni wadhaifu sana mbele ya mwanamke hata awe house girl hasa ikiwa mkewe yupo mbali kama ilivyo kwako. Kama upo serious na unataka kuepuka vishawishi na migogoro isyo ya lazima tafuta house boy au mlete mkeo huko arusha

Mi mbona niliweza kuwa na mfanya kazi wa aina hiyo na hakuna kilichotokea? Ni kujiendekeza tu na tamaa za kijinga.
 
Insecurity in a wife is a nightmare. Ni wasaidizi wa ndani tu ndio wako desperate au ni wanawake kwa ujumla? Kwanza mnaishije wakati hakuna uaminifu?
 
Mi mbona niliweza kuwa na mfanya kazi wa aina hiyo na hakuna kilichotokea? Ni kujiendekeza tu na tamaa za kijinga.

binadamu hatufanani. Utakuwa umeoksea ukifikiri kwamba kila unaliloweza wewe basi kila mtu analiweza. Lakini pia mazingira ya kuishi na binti wa kazi hayafanani. Binti uliyekuwa naye wewe sio huyo atakayekuwa naye mleta mada. Mke wa mleta uzi sio sawa na mke wako ndio mleta uzi anasema mkewe ana hofu kuhusu jamaa kuajiri msichana wa kazi. Jiongeze
 
Mkeo ana hoja ya msingi. wanaume ni wadhaifu sana mbele ya mwanamke hata awe house girl hasa ikiwa mkewe yupo mbali kama ilivyo kwako. Kama upo serious na unataka kuepuka vishawishi na migogoro isyo ya lazima tafuta house boy au mlete mkeo huko arusha
Mkuu wife naye ana kibarua huko ninakotoka. So sio rahisi kuwa naye Arusha.
 
  • Thanks
Reactions: Kig
Muandiko wako tu,unaonesha kua unatafuta mke wa pili ila umeamua awe house girl
 
Kudeki na kufua nguo zako simple du mkuu, miezi 10 mbona kiduchu, na itakuwa sehemu ya mazoezi. Huna haja ya msichana wa kazi!
 
Mkeo ni mwanamke. Hivyo anawajua vizuri wenzie. Msikilize....tena vizuri sana.
 
Yaleyale

Chukua Kijana wa Kiume.....
Ukilazimisha utakuja na mrejesho House Girl ananitega.....
Mwisho Mzuri kuliko Mkeo,.......
Next:boxing:
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom