Mke wa pacha wangu anataka nizae nae

JembePoli

JF-Expert Member
Jul 14, 2015
1,324
994
Habari zenu wana MMU bila shaka hamjambo,

Mimi ni mume wa mke mmoja lakini pia sisi tulizaliwa wawili (pacha) wote wakiume, baada ya kutokea matatizo ya kufiwa na wazazi wetu tukiwa na miaka 14 tu ilibidi ndugu watuchukue mimi nilienda kwa baba mkubwa Mbeya mwenzangu alienda kwa mjomba Mwanza tukawa tumetengana kwa namna hiyo,tulitembeleana mara moja kwa mwaka kutokana na ratiba za masomo.

Nilipokuwa kidato cha tatu mzee hakulizishwa na mwenendo mzima wa masomo yangu ukilinganisha na pacha wangu wa Mwanza hivyo akaniamishia shule nyingine pale pale Mbeya.Pale ndio nilijuana na binti mmoja matata sana nikafanya bidii akawa rafiki yangu huku nikitafuta siku kumfanya awe mpenzi wangu (maana ulikuwa urafiki wa kaka na dada) sikufanikiwa maana miezi kadhaa mbele nae alihama maisha yakaendelea.

Tukaja kuonana tukiwa wakubwa tena akiwa ni mchumba wa pacha mwenzangu walifunga ndoa miaka 4 iliyopita hawajabahatika kupata mtoto kwa muda wote wa ndoa yao na madaktari wanasema hawana tatizo lolote.
Mimi kama nilivyosema ni mume wa mke mmoja na ndoa yangu inamwaka mmoja tu mpaka sasa bado sijabahatika kupata mtoto japo naamini MUNGU atatujalia tutapata.Kwa sasa tunaishi mkoa mmoja japo wilaya tofauti wote tukiwa na familia.

Jumapili nilikutana na shemeji yangu mke wa pacha akanieleza jinsi ambavyo mumewe amekuwa akitamani mtoto kiasi hata akiwabebea zawadi watoto wa majirani zao yeye kama mwanamke imemuuma akafikilia aje aniombe nitembee nae siku ya hatari ili tu ashike mimba kwa kuwa sisi ni damu moja.

Nikamjibu haitawezekana (mimi na pacha hatufanani labda uwe makini sana) kwanza yule ni ndugu yangu siwezi mfanyia hivyo,alichonambia na kusisitiza ni anaomba kwani inawezekana damu zao haziendani na madaktari wanawasibitishia hawana tatizo na yeye hataki kuona mumewe anahamanika japo anasema hajawahi kuona hata siku moja mmewe akionyesha kuchukizwa na hali ya wao kutokuwa na mtoto kwani huwa akimwambia upo wakati nae ataitwa baba japo anahisi mumewe ipo siku atachoka hali hiyo na atabadilika hivyo ananiomba sana.

Nimefikiria sana;

1~Hata nikiendelea na msimamo wangu wa kukataa si ataenda kwa mwanaume mwingine na kumbambikia ndugu yangu,hata kama nikiingilia si nitaonekana mwehu.

2~Anajua kuwa ninampenda lakini ilikuwa zamani (japo ni mzuri na ni mara 2 ya mwanzo) sasa ninamke sitapenda kumsaliti,japo hawezi kujua ila tu dhamila yangu inanihukumu.

3~Vipi akijua pacha si ndio undugu utakuwa hakuna tena/japo hata mimi napenda kuitwa baba na kwa vyovyote mtoto wao ataniita baba.Kuna msemo unasema ukiwaza sana utaona yote ni majibu sahihi naombeni mnisaidie ki mtazamo wenu.

Tafadhari japo ni ndefu soma kwa umakini na ikumbukwe hatujafanya lolote na shemeji yangu na kuna baadhi ya majina na shule nimeficha kwani inaweza kuleta shida kwani inawezekana nae/nao wanapita pita humu.
 
ivi umejiuliza na hili swali??? je' ukilala nae na kuisaliti ndoa yako alafu shemeji yako bado asishike mimba kamwe itakuwaje??????????? acha huruma za kijinga wakat pacha wako hawazi saana swala hlo we ndo uweweseke ati nikifanya itakuw vile nisipofany itakuwa hiv acha kuzunguka ukuta wakati eneo ni hilo hilO jenga familia yako na yangoswe mwachie ngoswe.
 
ivi umejiuliza na hili swali??? je' ukilala nae na kuisaliti ndoa yako alafu shemeji yako bado asishike mimba kamwe itakuwaje??????????? acha huruma za kijinga wakat pacha wako hawazi saana swala hlo we ndo uweweseke ati nikifanya itakuw vile nisipofany itakuwa hiv acha kuzunguka ukuta wakati eneo ni hilo hilO jenga familia yako na yangoswe mwachie ngoswe.
 
ivi umejiuliza na hili swali??? je' ukilala nae na kuisaliti ndoa yako alafu shemeji yako bado asishike mimba kamwe itakuwaje??????????? acha huruma za kijinga wakat pacha wako hawazi saana swala hlo we ndo uweweseke ati nikifanya itakuw vile nisipofany itakuwa hiv acha kuzunguka ukuta wakati eneo ni hilo hilO jenga familia yako na yangoswe mwachie ngoswe.
 
Mnapofika duniani Kila mtu Na lake.Mshauri pacha wako aende kwa wataalamu wa uzazi Ili ajue la kufanya.ila usimwambie khs mke wake.

Double impact ya Van dame.Hahahaa
 
kazi ya uumbaji ni ya Mungu mwenyewe, yeye ndie mwenyekujua nani azaliwe naazaliwe na nani. sauti inayokuambia usifanye hivyo ni sauti ya Mungu hivyo itii.

Kweli mkuu lakini lazima kuwe na usababishaji.
Ahsante kwa ushauri
 
ivi umejiuliza na hili swali??? je' ukilala nae na kuisaliti ndoa yako alafu shemeji yako bado asishike mimba kamwe itakuwaje??????????? acha huruma za kijinga wakat pacha wako hawazi saana swala hlo we ndo uweweseke ati nikifanya itakuw vile nisipofany itakuwa hiv acha kuzunguka ukuta wakati eneo ni hilo hilO jenga familia yako na yangoswe mwachie ngoswe.

Mkuu kuna kitu umeongea ambacho hata mimi nimegundua "huruma" hicho tu ndio kinachonifanya niwe na mambo mengi wakati muhusika analilux tu huko.
Ahsante umeniweka sawa.
 
Mnapofika duniani Kila mtu Na lake.Mshauri pacha wako aende kwa wataalamu wa uzazi Ili ajue la kufanya.ila usimwambie khs mke wake.

Double impact ya Van dame.Hahahaa

Mkuu hayo yote wameshafanya tena kwa madaktari bingwa lakini jibu ni lile lile wote mko vizuri.
Labda niwashauri watafute miti shamba
 
Anatakaje sasa umpe mimba wakati nawe bado hujapata mtoto anajuaje wewe utampa hiyo mimba??

Ongea na shemeji ako ukiwa serious kabisa na sura ya kazi, mwambie mtoto ni maajiwa ya Mungu ukifika wakati atapata (kuna dada kajifungua juzi watoto mapacha wa kike, kaishi ndoani miaka 14 nae ana miaka 41)

Mwambie kama hitaji lake kubwa ni mtoto na yupo tayari kumpata kwa mtu yoyote atoke kwenye hiyo ndoa akatafute mtoto kuliko kumbambikizia mme wake mtoto wa mtu mwingine.
Mwambie akiendelea na hayo mawazo utamwambia ndugu yako
 
Du huyu shemeji yako siyo mvumilivu katika ndoa ukifanya hilo kosa na mkeo akajua itakuwa mgogoro mkubwa sana katika familia yenu bora umshauri tu avumilie atampata tu mtoto km mungu akiamua cha msingi mfariji mshauri kwa maneno ya hekima. Inaonyesha anatatizo la kisaikolojia,pia kumbuka ukijaribu mara ya kwanza hamuwez kuacha atakuja tena na maneno mengine ya kukushawishi muendelee kufanya.Acha kabisa hyo ni dhambi na ni laana kubwa mbele ya Mungu.
 
Du huyu shemeji yako siyo mvumilivu katika ndoa ukifanya hilo kosa na mkeo akajua itakuwa mgogoro mkubwa sana katika familia yenu bora umshauri tu avumilie atampata tu mtoto km mungu akiamua cha msingi mfariji mshauri kwa maneno ya hekima. Inaonyesha anatatizo la kisaikolojia,pia kumbuka ukijaribu mara ya kwanza hamuwez kuacha atakuja tena na maneno mengine ya kukushawishi muendelee kufanya.Acha kabisa hyo ni dhambi na ni laana kubwa mbele ya Mungu.

Ahsante mkuu ndio maana nikaona nililete hapa angalau mnanipa mwanga wa kutoka kwenye hili
 
Habari zenu wana MMU bila shaka hamjambo,

Mimi ni mume wa mke mmoja lakini pia sisi tulizaliwa wawili (pacha) wote wakiume, baada ya kutokea matatizo ya kufiwa na wazazi wetu tukiwa na miaka 14 tu ilibidi ndugu watuchukue mimi nilienda kwa baba mkubwa Mbeya mwenzangu alienda kwa mjomba Mwanza tukawa tumetengana kwa namna hiyo,tulitembeleana mara moja kwa mwaka kutokana na ratiba za masomo.

Nilipokuwa kidato cha tatu mzee hakulizishwa na mwenendo mzima wa masomo yangu ukilinganisha na pacha wangu wa Mwanza hivyo akaniamishia shule nyingine pale pale Mbeya.Pale ndio nilijuana na binti mmoja matata sana nikafanya bidii akawa rafiki yangu huku nikitafuta siku kumfanya awe mpenzi wangu (maana ulikuwa urafiki wa kaka na dada) sikufanikiwa maana miezi kadhaa mbele nae alihama maisha yakaendelea.

Tukaja kuonana tukiwa wakubwa tena akiwa ni mchumba wa pacha mwenzangu walifunga ndoa miaka 4 iliyopita hawajabahatika kupata mtoto kwa muda wote wa ndoa yao na madaktari wanasema hawana tatizo lolote.
Mimi kama nilivyosema ni mume wa mke mmoja na ndoa yangu inamwaka mmoja tu mpaka sasa bado sijabahatika kupata mtoto japo naamini MUNGU atatujalia tutapata.Kwa sasa tunaishi mkoa mmoja japo wilaya tofauti wote tukiwa na familia.

Jumapili nilikutana na shemeji yangu mke wa pacha akanieleza jinsi ambavyo mumewe amekuwa akitamani mtoto kiasi hata akiwabebea zawadi watoto wa majirani zao yeye kama mwanamke imemuuma akafikilia aje aniombe nitembee nae siku ya hatari ili tu ashike mimba kwa kuwa sisi ni damu moja.

Nikamjibu haitawezekana (mimi na pacha hatufanani labda uwe makini sana) kwanza yule ni ndugu yangu siwezi mfanyia hivyo,alichonambia na kusisitiza ni anaomba kwani inawezekana damu zao haziendani na madaktari wanawasibitishia hawana tatizo na yeye hataki kuona mumewe anahamanika japo anasema hajawahi kuona hata siku moja mmewe akionyesha kuchukizwa na hali ya wao kutokuwa na mtoto kwani huwa akimwambia upo wakati nae ataitwa baba japo anahisi mumewe ipo siku atachoka hali hiyo na atabadilika hivyo ananiomba sana.

Nimefikiria sana;

1~Hata nikiendelea na msimamo wangu wa kukataa si ataenda kwa mwanaume mwingine na kumbambikia ndugu yangu,hata kama nikiingilia si nitaonekana mwehu.

2~Anajua kuwa ninampenda lakini ilikuwa zamani (japo ni mzuri na ni mara 2 ya mwanzo) sasa ninamke sitapenda kumsaliti,japo hawezi kujua ila tu dhamila yangu inanihukumu.

3~Vipi akijua pacha si ndio undugu utakuwa hakuna tena/japo hata mimi napenda kuitwa baba na kwa vyovyote mtoto wao ataniita baba.Kuna msemo unasema ukiwaza sana utaona yote ni majibu sahihi naombeni mnisaidie ki mtazamo wenu.

Tafadhari japo ni ndefu soma kwa umakini na ikumbukwe hatujafanya lolote na shemeji yangu na kuna baadhi ya majina na shule nimeficha kwani inaweza kuleta shida kwani inawezekana nae/nao wanapita pita humu.
mmmh acheni uzinifu jamani
 
Je ni ile familia iliyopotea kwenye ajali arusha? Pole kwa kupoteza wazazi.
 
Habari zenu wana MMU bila shaka hamjambo,

Mimi ni mume wa mke mmoja lakini pia sisi tulizaliwa wawili (pacha) wote wakiume, baada ya kutokea matatizo ya kufiwa na wazazi wetu tukiwa na miaka 14 tu ilibidi ndugu watuchukue mimi nilienda kwa baba mkubwa Mbeya mwenzangu alienda kwa mjomba Mwanza tukawa tumetengana kwa namna hiyo,tulitembeleana mara moja kwa mwaka kutokana na ratiba za masomo.

Nilipokuwa kidato cha tatu mzee hakulizishwa na mwenendo mzima wa masomo yangu ukilinganisha na pacha wangu wa Mwanza hivyo akaniamishia shule nyingine pale pale Mbeya.Pale ndio nilijuana na binti mmoja matata sana nikafanya bidii akawa rafiki yangu huku nikitafuta siku kumfanya awe mpenzi wangu (maana ulikuwa urafiki wa kaka na dada) sikufanikiwa maana miezi kadhaa mbele nae alihama maisha yakaendelea.

Tukaja kuonana tukiwa wakubwa tena akiwa ni mchumba wa pacha mwenzangu walifunga ndoa miaka 4 iliyopita hawajabahatika kupata mtoto kwa muda wote wa ndoa yao na madaktari wanasema hawana tatizo lolote.
Mimi kama nilivyosema ni mume wa mke mmoja na ndoa yangu inamwaka mmoja tu mpaka sasa bado sijabahatika kupata mtoto japo naamini MUNGU atatujalia tutapata.Kwa sasa tunaishi mkoa mmoja japo wilaya tofauti wote tukiwa na familia.

Jumapili nilikutana na shemeji yangu mke wa pacha akanieleza jinsi ambavyo mumewe amekuwa akitamani mtoto kiasi hata akiwabebea zawadi watoto wa majirani zao yeye kama mwanamke imemuuma akafikilia aje aniombe nitembee nae siku ya hatari ili tu ashike mimba kwa kuwa sisi ni damu moja.

Nikamjibu haitawezekana (mimi na pacha hatufanani labda uwe makini sana) kwanza yule ni ndugu yangu siwezi mfanyia hivyo,alichonambia na kusisitiza ni anaomba kwani inawezekana damu zao haziendani na madaktari wanawasibitishia hawana tatizo na yeye hataki kuona mumewe anahamanika japo anasema hajawahi kuona hata siku moja mmewe akionyesha kuchukizwa na hali ya wao kutokuwa na mtoto kwani huwa akimwambia upo wakati nae ataitwa baba japo anahisi mumewe ipo siku atachoka hali hiyo na atabadilika hivyo ananiomba sana.

Nimefikiria sana;

1~Hata nikiendelea na msimamo wangu wa kukataa si ataenda kwa mwanaume mwingine na kumbambikia ndugu yangu,hata kama nikiingilia si nitaonekana mwehu.

2~Anajua kuwa ninampenda lakini ilikuwa zamani (japo ni mzuri na ni mara 2 ya mwanzo) sasa ninamke sitapenda kumsaliti,japo hawezi kujua ila tu dhamila yangu inanihukumu.

3~Vipi akijua pacha si ndio undugu utakuwa hakuna tena/japo hata mimi napenda kuitwa baba na kwa vyovyote mtoto wao ataniita baba.Kuna msemo unasema ukiwaza sana utaona yote ni majibu sahihi naombeni mnisaidie ki mtazamo wenu.

Tafadhari japo ni ndefu soma kwa umakini na ikumbukwe hatujafanya lolote na shemeji yangu na kuna baadhi ya majina na shule nimeficha kwani inaweza kuleta shida kwani inawezekana nae/nao wanapita pita humu.


MAANDIKO MATAKATIFU YANASEMA IKIMBIENI ZINAA.

NDUGU KAA MBALI NA DHAMBI HII NI TAMU KWA MUDA MFUPI SANA ILA IN MACHUNGU YASIYOFUTIKA

NA PIA KAA MBALI NA MKE WA NDUGU YAKO HATA KAMA ANAKUSHAWISHI WW KATAA
 
mmmmmm huyo Dada anamuomba maiti Sanda? kakuona na watoto wangapi mpaka anataka mbegu? awache uchangu wake na ukimvua nguo ndio umeshauchamba upupu............
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom