Mke wa mtu kaniletea msala

Mi bishoo tu

Senior Member
Jun 3, 2023
122
292
Habarini za weekend Watanganyika, mwaka Jana nilikutana na dada mmoja mmoja Wilayani Bunda ambaye mmewe ni mmiliki wa hiace zinazoenda bunda-kibara-kisorya. Baada ya kupeana mawasiliano tukaanza chats za hapa na pale. Baada ya kuwa tumezoeana sana akaanza kulalamika kwamba mmewe kapata chombo kipya dada Fulani mtumishi wa serikali mpaka yeye kamtelekeza kiaina na hata haki yake ya ndoa anaipata kwa shida hata mara moja moja kwa mwezi tena kwa malumbano.Baada ya kama miezi mitatu tukaanza mahusiano ya kimapenzi,ambapo huyo dada aliamua kuniachia Kila kitu kwenye mwili wake ambapo nilikula mpaka mtandao wetu pendwa kama mara nne hivi.

Muda mwingi tulikuwa tukitaka kuwasiliana nilikuwa namtafuta kupitia messenger na siyo kwenye text za kawaida kwa kuhofia mumewe kumkamata. Wakati mwingine kama haupo hewani nilikuwa namtuma family friend wao mmoja ambaye ni mkubwa kwake kiumri na ambaye pia kaolewa.

Sasa kuanzia March mpaka mwezi May mwaka huu mawasiliano yetu yakawa ya kusua sua, nikahisi pengine na masuala ya ubize kuingiliana maana kuna kipindi nilikimbia kwenda maeneo ya mgodi wa buhemba kuhangaika na utafutaji.

Sasa Jana nilimcheki messenger na pasipo kumuuliza chochote nikamrushia picha yangu nikiwa kitandani, nikajibiwa nice. Nikajiuliza mbona siyo kawaida yake kujibu kimkato hivyo. Ilikuwa mida ya saa 5:20 usiku, ilipofika mida ya saa 5:27 nikapigiwa simu kupitia fb messenger, sikujibu.

Nikaangalia profile aliyepiga ni mmewe. Nilimfahamu maana yule dada alikuwa tayari kashanitumia picha zake. Leo kuanzia asubuhi mpaka muda huu jioni kashanipigia mara 32 messenger na ninahisi aliichukua simu ya mkewe.

Sasa najiuliza kama kachukua simu ya mkewe na ikiwa atazama messenger kusoma text zote mke atakuwa kwenye hali gani maana mle kuna Kila aina ya uchafu kuanzia kutumiana picha chafu, video chafu kusifiana uchafu wetu wote.

Lktakini pia atakuwa kamfahamu family friend wao mmoja ambaye mbali ya kuwa wanasali kanisa moja hapa mjini pia ni mama anayejiheshimu sana kimuonekano na pia ndie tulikuwa tunamtumia kwa mambo yetu mfano mimi kumpa vizawadi na kupeleka kwa mchepuko wangu ambaye ni mke wa mtu. Nitawapa mrejesho itakavyojiri.

Wale tunaokula wake za watu tuwe makini sana sana sijui hili saga litaisha vipi...Kwa sasa nipo zangu Mukendo Musoma nisikilizie ndani ya siku mbili tatu


NB:Nimeficha code kwa zaidi ya 80% acheni kujifanya mnaelewa kuliko Mimi mhusika
 
Wewe jamaa mikasa yako huwaga ni story za eric shigongo., Mwenye kufikwa na shida hawezi kujianika kiasi hiki (code ziko open),maana lazima awe na hofu ya kuchotwa kama maji kwenye mtungi na kuhalalisha kuwa hii ni chai umetaja na sehemu ambayo upo kwa sasa wakti umeshaharibu., Itoshe kusema wewe ni mtunzi wa hadithi na hii si ya kwanza kuiona kutoka kwako.

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Wewe jamaa mikasa yako huwaga ni story za eric shigongo., Mwenye kufikwa na shida hawezi kujianika kiasi hiki (code ziko open),maana lazima awe na hofu ya kuchotwa kama maji kwenye mtungi na kuhalalisha kuwa hii ni chai umetaja na sehemu ambayo upo kwa sasa wakti umeshaharibu., Itoshe kusema wewe ni mtunzi wa hadithi na hii si ya kwanza kuiona kutoka kwako.

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
Inatakiwa tumreport kwa Moderators hata kama anafanya au anadanganya, hili la kutaja watu moja kwa moja ni baya sana kwani litasababisha kuvunja ndoa, mauaji na kashfa kwenye jamii. Unasema mmemfira mke wa mtu tena unaweka na code nyingi wazi hii sio sawa. Anachofanya sio sahihi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom