Mke wa balozi Daraja auawa; Mfanyakazi wa nyumbani atafutwa

Kocha Wenger...mbona umemkomalia sana huyo msaidizi? Yaani huoni uwezekano wa wengine....unaanza kunikumbusha yale ya akina Malvo na mwenzake maana jamaa walikomalia na profile za ma serial killer huku wakiwaacha jamaa waendelee kufanya uhalifu wao...
 
kama ni vitasa vya namna hiyo ilikuwaje balozi na dereva wake washindwe kufungua toka nje?
mie naona balozi pia angetaja mda kamili (late evening) angeweza kusaidia kidogo kutoka na hali halisi ya pirika za mtaani zinavyoendelea lazima majirani wangeona matukio ambayo sio ya kawaida yanendelea kwa muheshimiwa sana sana swala la ujambazi.
 
alikimbiaje halafu akafunga mlango kwa ndani?
Uwezekano ni kwamba huyo jamaa aliruka ukuta. hata hivyo mbona mama alikutwa amefungiwa katika garage? Je huyo mama alijifungiaje humo? Hapa kuna walakini mkubwa sana!
 
Pole sana kwa wafiwa na mwenyezi mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu.

Jasusi.. that is the story we have been told; but in a situation like this there is a story behind the story. Ngoja nioneshe matundu machache kwenye stori ilivyo sasa.

a. The Story:


Kwa hiyo.. timeline yetu ni kuwa lolote lililotokea lilitokea siku ya Jumamosi kati ya mchana na jioni. Halikutokea usiku. Kama lilikuwa ni tukio la ujambazi na matumizi ya nguvu kiasi hicho hao majambazi watakuwa ni watu wa karibu sana kiasi cha kutokusababisha shuku toka kwa majirani mchana kweupe; na hiyo ina maana wapo mashahidi walioona kilichotokea, gari, watu n.k

Balozi alilala salama usiku ule bila kutoa taarifa polisi, kwa ndugu, jamaa na marafiki huku akiwa hana mawasiliano na mke wake na hajasema kama alijaribu kuwasiliana na msaidizi huyo wa nyumbani. (this is important to keep in mind)

b. The Story:


Sasa tunajua kuwa Balozi alilala salama usiku wote ule na hakufanya juhudi ya kupiga simu nyumbani siku ya pili wala kutoa taarifa kwa mtu mwingine yeyote. Muda huo unatoa nafasi ya mtu yeyote kutoweka na kuchelewesha uchunguzi.

Lakini pia tunaona jambo jingine muhimu kwa upelelezi. Malango ya nyumba ya Balozi yalikuwa yamefungwa kwa ndani. Sasa hapa hatuna budi kujiuliza huyo msaidizi wa nyumbani alitokaje na vitu vya kuiba halafu akafunga mlango kwa ndani kiasi kwamba mtu aliye nje anashindwa kuufungua?

La pili ni kuwa Balozi hana ufunguo wa mlango wa nyumba yake akiwa nje?

c. The Story:


Hapa kuna tatizo kidogo. Kwenye upelelezi tunaweza kusema ni kutokubaliana kwa eneo la tukio (inconsinstence of crime area). Viatu vya mhanga na mabegi yake yamekutwa karibu na geti. Vilifikaje hapo? Je mhanga aliuawa nje, aliwafukuza wahusika, hapa ni clue nzuri.. kulikuwa na damu karibu na geti?

d. The story:


So far.. tunachosikia hapa ni kwamba ndani ya nyumba na eneo zima hakukuwa na ushahidi wa foul play! Ina maana huyo mama hakuuawa ndani ya nyumba au nje ya nyumba kwani kama kungekuwa na damu au aina yoyote ya ushahidi kuwa amedhurika wangeita polisi mara moja. Kama walikuta ushahidi wa kitendo kibaya walipoingia ndani (hasa baada ya kukuta viatu vyake nje na mabegi) walitakiwa kutoa taarifa polisi mara moja, itakuwaje kama wabaya walikuwa bado wako ndani wanasubiri? especially baada ya kujua kuwa geti lilifungwa kwa ndani?

d. The story:
[Just when he was about to give up, he remembered to look inside his garage and…there she was, laying on the floor with a knife sticking out on her chest.

"We unlocked the garage which was padlocked from outside but she was already dead. We reported the matter to the police and they are investigating," he whispered, tears streaming down his face. [/QUOTE]

Hapa kuna mambo ya kutugusa fikra zetu kidogo. Baada ya kumkosa huko kwingine kote akaamua kuangalia kwenye gereji na wakaona mwili wa marehemu ukiwa na kisu kifuani. Wakafungua hilo lango la gereji (na hivyo kupoteza kwa kiasi kikubwa ushahidi wa nani aliufunga!) na siwezi kushangaa walipofika ndani mmoja wao akakichomoa kile kisu, na hivyo kufuta ushahidi wa nani alikichomeka (I hope thats not the case).

e. The story:


Tunaambiwa kuwa hili halikuwa tukio la ujambazi kwani hakuna kitu cha thamani kilichoibiwa, kuna kitu hawa watu walikuwa wanatafuta au kulikuwa na sababu binafsi ya kufanya tukio hilo zaidi ya kuiba. kama hao jamaa walikuwa wanatafuta fedha na ndani ya nyumba kuna vitu vya thamani why not take the valuables and liquidate them later?

So.. in short ni kuwa it is not what it seems..

Wacha we... .... MM Mwanakijiji mimi naona nisiseme maana kama wale walio ughaibuni wanaangalia FBI Files documentaries hapo iko kazi.

Bandugu angalieni hizo programmes ni muhimu sana kwa wale wanaoweza hasa walio USA, UK na popote pale ambako zinatolewa na hata askari polisi wetu ili kujua mbinu na mienendo ya uhalifu na jinsi ya kupata evidence etc.
 
Mh balozi aliwapigia simu watu gani siku hiyo ya tukio! conspiracy nyingine huenda aliwasiliana na wauwaji....mkewe alimpigia kuhakikisha job well done!
 
Kocha Wenger...mbona umemkomalia sana huyo msaidizi? Yaani huoni uwezekano wa wengine....unaanza kunikumbusha yale ya akina Malvo na mwenzake maana jamaa walikomalia na profile za ma serial killer huku wakiwaacha jamaa waendelee kufanya uhalifu wao...
kinacho nifanya nimkomalie msaidizi kwa vile inaonekana ni wao wawili tu ndio waliokuwa kwenye nyumba.na yeye ndio anaweza kutoa ufumbuzi zaidi wa hii kesi la sivyo hapa hii issue haitopatiwa jibu.

sijamng'ang'ania kwa kumuhukumu lakini kama kuna mchezo mchafu wowote umefanyika ambao sio ujambazi yeye ndio mwenye jibu kamili na hawa wasaidiz mara nyingi hawana power kabisa na labda kaogopa hata akisema ukweli anaona kesi atatupiwa yeye.
 
Mh balozi aliwapigia simu watu gani siku hiyo ya tukio! conspiracy nyingine huenda aliwasiliana na wauwaji....mkewe alimpigia kuhakikisha job well done!
Jamani, this is NOT fair! Unauhakika gani?
 
Binafsi sitaki kumshuku mtu yeyote wakati huu wa msiba; ninachojaribu kuonesha ni kuwa simulizi lilivyo sasa (aidha kwa bahati mbaya au makusudi) lina matundu mengi kuliko pakacha. Ni matumaini matundu hayo yatazibwa ili tuweze kupata picha kamili kwa sababu..

Kama nimempigia mke wangu simu na baadaye nikajaribu sana kumpata siwezi.. nisingelala huko nilikokuwa hasa ukizingatia ni mtu mzima.. hata kama ingekuwa si ujambazi ingekuwaje kama ameanguka bafuni na hakuna mtu wa kumsaidia?
 
Tatizo media za bongo nazo haziaminiki kivile.Najaribu kujiuliza kuwa walimwona kuwa yumo garage wakiwa nje au baada ya kufungua mlango wa garage?Maana habari inaelekeza kuwa ni walimwona kabla ya kufungua mlango.Either pana dirisha hapo garage(huwa sio kawaida) au walichungulia chini ya mlango(inategemea na mlango ulivyo).Pia kama main gate ni la kufunga hata kwa nje then possibly muuaji alipita hapohapo na akafunga akiwa nje.Je simu ya mkononi ya marehemu imepatikana?Sijaona ikiongelewa kwani wanasema ni hizo tsh 2 mil(how accurate is this figure??).
 
Ni kifo cha kusikitisha sana, but naungana na yule ambaye ametaka tusitoe hukumu kwa houseboy, tusubiri kazi ya polisi. Poleni sana wafiwa.
 
.....
Kama nimempigia mke wangu simu na baadaye nikajaribu sana kumpata siwezi.. nisingelala huko nilikokuwa hasa ukizingatia ni mtu mzima.. hata kama ingekuwa si ujambazi ingekuwaje kama ameanguka bafuni na hakuna mtu wa kumsaidia?


Ki bongo bongo mbona kawa tu kumkosa mtu kwenye simu na ukalala usingizi. Labda huyo mpigiwaji awe mgonjwa mwenye kuhitaji uangalizi wa karibu. Vinginevyo watu kibao walala usingizi mnono wanapowapigia wake zao simu bila kuwapata.

Labda niulize, je simu ya marehemu ipo? Hiyo simu inaweza kutoa clue ya timeline ya tukio au kama kulikuwa na mawasialino yanayohusiana na tukio.

Pili, what if huyo mama balozi alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na msaidizi wa nyumbani, ikapelekea kukorofishana na hata kufikia kumuua?

What if mama balozi alikuwa katili sana kwa msaidizi kiasi kufikia kijana kutaka kumkomoa dizaini ya wa wanavyofanya watu wa Mara?
 
what a sad day, for the family of the Daraja. Our prayers and grief are with you, as you go through this tough time. We will always remember you, as one of the respectable and warm hearted ladies during your time here in DC. May u rest in peace.
 
Polisi wa Tanzania sina imani nao ni wazembe sana utakuta tayari hata evidence nyingi zimekuwa tempered au hawakuchukua vitu ambavyo viko obvious. Utakuta wako more political aligned kuliko kufanya kazi zao kwa uadilifu.
 
Ki bongo bongo mbona kawa tu kumkosa mtu kwenye simu na ukalala usingizi. Labda huyo mpigiwaji awe mgonjwa mwenye kuhitaji uangalizi wa karibu. Vinginevyo watu kibao walala usingizi mnono wanapowapigia wake zao simu bila kuwapata.
kwa mke wako ni vigumu sana kupuuzia na kwenda kulala kama hajawapokea simu unless ni kawaida yenu kwamba mmoja wenu asipopekea simu nikawaida tu.kitu ambacho nakataa kuwa hivyo kwa mke wako lazima utakuwa na wasi wasi na kufanya juhudi zakujua kama yuko salama au hapana wakati huo huo.


maswali mengine ya nyongeza hapa,katika maongezi yao ya mchana je mke wake alikuwa nyumbani au alikuwa katoka? na kama alikuwa nyumbani je alikuwa na mpango wa kwenda popote? najua lazima mke na mume lazima wapeane ratiba.nauliza maswali haya kutoka na hivyo viatu na hand bag kukutwa karibu na geti je mama wa nyumba alikuwa anarudi nyumbani au alikuwa anatoka na kama kulikuwa na safari labda mume wake alimwambia katika maongezi yake.tukijua hapo sasa tunaweza kujaribu ku-connect dots kutoka hapo alipokuwepo mwanzo au alipokuwa anataka kwenda je watu waliomtegemea kuja baada kuona kimya wali-react vipi ?


kitu kingine kuna simu ya ndani? kama hipo mume wake alivyomkosa kwenye simu ya mkononi alijaribu simu ya ndani ? je mfanya kazi wa ndani alikuwa na cell phone? kama alikuwa nayo mume wake alijaribu kumpigia hili kujua kama kila kitu salama au kama mama wa nyumba yupo? nimeuliza hivi kutokana na watu wengi wana cell phone siku hizi kama hakuwa nayo hili swlai sio muhimu.
 
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na awape nguvu na faraja wafiwa katika kipindi hiki kigumu kwao~AMEN. Huyu mfanyakazi si ajabu kashirikiana na Majambazi na kuna vitu ambavyo si ajabu vimeibiwa katika nyumba hiyo.
 
what if huyo mfanyakazi wa ndani naye ameuawa na kuburuzwa sehemu nyingine, au ametekwa n.k
 
what if huyo mfanyakazi wa ndani naye ameuawa na kuburuzwa sehemu nyingine, au ametekwa n.k

That is possible too Mkuu, wakati polisi wakiendelea kumtafuta mfanyakazi wa ndani majambazi ndiyo wanazidi kutokomea na kuharibu ushahidi.
 
Back
Top Bottom