Kuna mpenzi wa rafiki yangu anakunywa Safari 12 akibadili anakunywa chupa mbili za konyagi bila maji na huwezi kujuwa kalewa demu ana kichwaa cha pombe balaa.
Halafu kiumbo ni mdogo hata kwenye mkono hatoshi.Huyo unahaki umshangae , maana si kawaida mwanamke anywe nusu chupa asione dunia inazunguka kushoto kulia, chini juu, bala tupu.
kama nyie mnakunywa na mnalewa mpaka wengine kumwaga radhi hadharani kwanini kwetu iwe tatizo!!tatueni pande zote mbili bwana...sio kila kitu mnakandamizia kwetu zaidi!!!:disapointed:
Kuna wanaume wakinywa bia 2-3 tu anaanza ugomvi/kutukana kwahiyo tatizo lipo pande zote.lakini inavyo onyesha wanawake, wanalewa haraka kuliko wanaume. Hatukatai kulewa kwa wanaume , lakini ebu tuangalie kwanini mnapata kizunguzungu just kuonja tuu. Halafu mwanamke akilewa na kuanza kuleta vituko ni kitu ambacho si kuzuri kutokana na heshima mnayompewa katika jamii.
lakini inavyo onyesha wanawake, wanalewa haraka kuliko wanaume. Hatukatai kulewa kwa wanaume , lakini ebu tuangalie kwanini mnapata kizunguzungu just kuonja tuu. Halafu mwanamke akilewa na kuanza kuleta vituko ni kitu ambacho si kuzuri kutokana na heshima mnayompewa katika jamii.
Kwasababu hatujazoea ulevi....ila wapo wanawake wanaoweza kuzihimili...pia kina baba wanaopepesuka baada ya mbili tatu!!!
Kuhusu heshima kwani ya baba sio muhimu????Embu kaba kote kote!!
Sasa lizzy tunaenda pamoja, ila nikuulize swali. Unajua vichochoro vyetu vya hapa bongo. Ukikuta mwanaume amelala njiani na giza, na mwanamke amelala naye gizani saa nne usiku amelewa, Ivi yupi atakuwa katika mazingira yahatari??. Mie naona mwanamke ndoo ataadhirika zaidi, si unanipata hapo kipenzi??
Kwa jinsi dunia ilivyoharibika????Hata baba anakua hatarini sana tu aisee....
Haya, tuzungumzie hivi (samahani lakini lizzy): Ubakaji.
Lakini lizzy, hivi kipi rahisi. mwanaume kumbaka mwanamke, au mwanaume kumbaka mwanaume mwenzake??