Mke kazira kutumia gari: Ushauri please

Wakuu, naomba ushauri katika mkwamo huu!Nilimpa mke wangu gari atumie kwa ajili ya shughuli zake za biashara ya duka la nguo. Kwa kwenda na kurudi nyumbani na kwa ajili ya kufuatilia mabo ya biashara yake. vile vile kwa shughuli za nyumbani kama kupeleka watoto hospitali n.k. Mimi pia nina usafiri wangu. Mwezi jana aliibiwa side mirror na taa moja ya mbele pale Kariakoo. Akaniarifu na baada ya kuona hana juhudi ya kurudishia huku akiendelea kuendesha gari "chongo" , niliamua kutumia pesa zangu kufanya replacement. Wiki mbili zilizopita nimekuta tena taa moja hakuna. Kumuuliza ikawa zogo. Anasema nisimuulize kitu yeye atarudishia. nikasubiri ikawa kama mwanzo. Baadaye nikaamua tena kununua taa nyingine na nikamwonya kuwa sitaweza kuwa nanunua taa naye anaendelea kutochukua tahadharina kuwa mwangalifu. Heeh! kumbe nimechafua hali ya hewa! Mwanamke wiki mbili hizi hatumii gari anakwenda kazini kwake kwa usafiri nisioujua. Juzi akanitumia sms akasema " sihitaji gari lako masimango yamezidi" Nishaurini wataalam,

Possible umemsimanga nalo acha alizire! Ingekuwa mimi ingekuwa mie ingeambatana nakugonga BAN YA 2 WEEKS, NO DUDU hadi unajiju!
 
mkuu,hiki kisa chako kimenifundisha kitu,
nilikuwa na mpango wa kumnunulia wife usafiri(baiskeli ya gia) awe anaendea kazini nahc ataleta dharau kama hizi,ishamkost,ndo hapati tena kitu,na hta akinunua mwenyewe nauza!
 
kama shughuli zake ziko kariakoo mwekee alarm sababu kule watu wako na shughuli mbalimbali, wengine wanawaaga wake zao wanaenda kazini, kazi zenyewe ndio hizo za kuiba, wakipata upenyo wanaiba, pia tafuta njia nzuri ya kumwambia mkeo asione unamsimanga, kwani gari si yake na ww una yako?
 
Unless uwe haujatueleza yote,kama ulimwambia hivyo mara moja tu au ulikuwa unarudiarudia maneno hayohayo,kurudiarudia ndiyo kusimanga vinginevyo huyo ni Mwanamke mwenye Kisarani "bad tempered",yaani katika makuzi yake amefundishwa "kutokukosolewa",Arrogant,"always right"

Pole sana Mkubwa,ukiwa na rafiki/mke mwenye Haiba hiyo inabidi umkabili kwa Upole sana,ni "handle-with care type"

Kwanza mwache kwa muda angalau wa Wiki mbili ahenye,halafu siku kaa naye Mweleze kwa Upole "Mke wangu Mpenzi,embu niambie,ukiwa unakosea au una tabia isiyofaa,Mimi mume wako natakiwa nifanye nini?",mwache ajibu hilo swali!!

Kama ni mwanamke ambaye anakupenda,swali hilo litamchoma na atakuomba radhi!!!! Otherwise,mpotezee mpaka mwenyewe atambue kwamba anakosea!!!

WEll said hapo kwenye RED. Watu ambao huwa wakikosolewa wanasema wanaonewa (wanatumia maneno kama unanidharau, unanisimanga, unajisikia sana nk) wanasumbuliwa na a low self esteem; makuuzi yao hayakuwajengea kujiamini na kujithamini; mara nyingi wanakuwa paranoid...kila wakati wanahisi kuonewa na mara nyingi ni wepesi kuanzisha ugomvi wa maneno...Nyani mzee, naamini hili si tukio pekee...lakini nakushauri kwa kuwa ni wife you need to understand her; ni weakness ambayo ina mizizi mirefu so learn to live with her.
 
Kina mama ndio walivyo ndugu yangu, kuna kipindi inabidi unajishusha tu hata kama yeye ndio mwenye kosa, kuna siku niliwahi kusema hapa we ukitaka kuishi kwa amani usifuatilie kabisa 'mambo madogo madogo' kama bajeti za nyumbani, matumizi ya magari (hata kama umenunua wewe) au sijui nyumbani panaendaje, wewe cha msingi tafuta hela mkabidhi aamue yeye vyote vya kufanya, apange matumizi na kila kitu kinachohusu hapo nyumbani na wewe ridhika tu au laa umpe ushauri akikataa basi ila wewe fuatilia 'mambo makubwa' tu kama kwanini Gaddafi kafa, CCM mwisho wake lini? Kwanini shilingi yetu inazidi tu kushuka thamani, Obama atashinda next election? Vipi Congo itakuwaje baada ya uchaguzi ujao November? Alafu utaona kama kutakuwa na shida na mpenzi mkeo
Sokwe bana, umenifurahisha sana, ila unachosema ni kweli mkuu!
 
shukuru Mungu hawajamvamia kuchukua gari lote na kumpiga yeye, wewe mtengenezee tu sio kulalama, wanawake ndivo tulivo
 
shukuru Mungu hawajamvamia kuchukua gari lote na kumpiga yeye, wewe mtengenezee tu sio kulalama, wanawake ndivo tulivo
Mwanamke katokana na ubavu wa kushoto wa mwanaume na sifa ya ubavu
ni kuwa umepinda, kwa hiyo mwanamke AMEPINDA.
 
Wakuu, naomba ushauri katika mkwamo huu!Nilimpa mke wangu gari atumie kwa ajili ya shughuli zake za biashara ya duka la nguo. Kwa kwenda na kurudi nyumbani na kwa ajili ya kufuatilia mabo ya biashara yake. vile vile kwa shughuli za nyumbani kama kupeleka watoto hospitali n.k. Mimi pia nina usafiri wangu. Mwezi jana aliibiwa side mirror na taa moja ya mbele pale Kariakoo. Akaniarifu na baada ya kuona hana juhudi ya kurudishia huku akiendelea kuendesha gari "chongo" , niliamua kutumia pesa zangu kufanya replacement. Wiki mbili zilizopita nimekuta tena taa moja hakuna. Kumuuliza ikawa zogo. Anasema nisimuulize kitu yeye atarudishia. nikasubiri ikawa kama mwanzo. Baadaye nikaamua tena kununua taa nyingine na nikamwonya kuwa sitaweza kuwa nanunua taa naye anaendelea kutochukua tahadharina kuwa mwangalifu. Heeh! kumbe nimechafua hali ya hewa! Mwanamke wiki mbili hizi hatumii gari anakwenda kazini kwake kwa usafiri nisioujua. Juzi akanitumia sms akasema " sihitaji gari lako masimango yamezidi" Nishaurini wataalam,

huyo ana yake..... kama unabisha weka magari ndani na usimpe ikifika wiki utajua kila kitu
 
huyo ana yake..... kama unabisha weka magari ndani na usimpe ikifika wiki utajua kila kitu
Solution si kuweka ndani, hiyo gari amkabidhi HOUSE GIRL ili apime
vizuri kina cha maji!
 
Ndugu yangu Nyani Mzee,

Wake zetu hawa ndo hivyo, ni handle with great care. Yaani hiyo situation yako nimeshakumbana nayo mara kibao! Solution ya leo haitafanya kazi kesho. Ila kama wengi wanavyosema hapa mwanamke anakuwa na ile feeling kwamba na yeye ni bosi hivyo hatakiwi kusemwa semwa. Lakini vile vile mwanamke mwenye udhaifu fulani kama kutojali mali, usahaulifu sana, kukosea kitu fulani anajenga defence mechanism.

Wanawake wengi kutokana na aina ya malezi yanayopata utotoni, wanakuwa wakubwa huku wakiwa na vitabia vingi vya kitoto. Hiki kitabia ni mojawapo. Yaani amefanya makosa, hataki akosolewe, akikosolewa yule anayemkosoa ndo anamuona mbaya wake. Halafu hapo lazima kuna watu wa nje (hasa mashosti zake) anawasimulia wanampa ya kumpa.

Mie msimamo wangu ni kuwa ulichofanya ni sahihi. Lazima umuoneshe kama anachofanya ni makosa na inatakiwa awe mwangalifu. Alichotakiwa kufanya ni kukuomba umpe ushauri afanyeje asiwe anaibiwa na ajaribu mbinu utakazompa. Lakini kwa mwanamke kukubali mbele ya mme wake kuwa amekosea; hasa kosa lenyewe likiwa hili la kujirudia rudia, anaona ni udhaifu. Sababu kubwa ni kuwa wanawake mara nyingi huwa wanaongea sana na marafiki zao mambo yao ya ndani mno na mara nyingi wanashuliwa vibaya.

Najua atalalmika kuwa una mnyanyasa, una gubu, n.k. Lakini usipofanya hivyo itakuwa mbaya zaidi. Ni afadhali aone unamnyanyasa kwa muda mfupi hatimaye atagundua tu kuwa kosa ni la kwake.

Mwanamke hata siku moja hatakubali kujishusha kwa mme wake (reality). Na mwanamke hana ujasiri wa kuomba msamaha kwa mme (reality).

Kurudisha hali ya hewa, mwache kama wiki moja au mbili, then mwombe msamaha kwa jinsi ulivyoufikisha ujumbe. Halafu mwache tena. Baada ikipita kama miezi miwili au mitatu mwambie kama hataki tena kuitumia hiyo gari unaigawa kwa mtu mwingine (hasa ndugu wa upande wako) au unafikiria kuiuza.

Kwa mwanamke subira yavuta heri. Mwache kwa muda. Ila onesha concern kuwa kitendo chake hicho hakikufurahishi! Atajirudi tu!
 
Kuna vitu vingine siyo vya kuleta hapa JF. kuna vitu ambavyo vipo ndani ya control ya mwanaume ndani ya nyumba. Hiki ni kimojawapo.
Ok..sikulaumu lakini, labda ulitaka kutuonyesha idadi ya magari uliyonayo. Tumekupata mkuu

Rejao, hoja yangu si idadi ya magari. Gari si fahari kama zamani ni kitendea kazi tu. Hoja ni hiyo tabia ya kuzira anapokosolewa. Umekuwa too subjective. Nashukuru nimekuelewa.
 
Ndugu yangu Nyani Mzee,

Wake zetu hawa ndo hivyo, ni handle with great care. Yaani hiyo situation yako nimeshakumbana nayo mara kibao! Solution ya leo haitafanya kazi kesho. Ila kama wengi wanavyosema hapa mwanamke anakuwa na ile feeling kwamba na yeye ni bosi hivyo hatakiwi kusemwa semwa. Lakini vile vile mwanamke mwenye udhaifu fulani kama kutojali mali, usahaulifu sana, kukosea kitu fulani anajenga defence mechanism.

Wanawake wengi kutokana na aina ya malezi yanayopata utotoni, wanakuwa wakubwa huku wakiwa na vitabia vingi vya kitoto. Hiki kitabia ni mojawapo. Yaani amefanya makosa, hataki akosolewe, akikosolewa yule anayemkosoa ndo anamuona mbaya wake. Halafu hapo lazima kuna watu wa nje (hasa mashosti zake) anawasimulia wanampa ya kumpa.

Mie msimamo wangu ni kuwa ulichofanya ni sahihi. Lazima umuoneshe kama anachofanya ni makosa na inatakiwa awe mwangalifu. Alichotakiwa kufanya ni kukuomba umpe ushauri afanyeje asiwe anaibiwa na ajaribu mbinu utakazompa. Lakini kwa mwanamke kukubali mbele ya mme wake kuwa amekosea; hasa kosa lenyewe likiwa hili la kujirudia rudia, anaona ni udhaifu. Sababu kubwa ni kuwa wanawake mara nyingi huwa wanaongea sana na marafiki zao mambo yao ya ndani mno na mara nyingi wanashuliwa vibaya.

Najua atalalmika kuwa una mnyanyasa, una gubu, n.k. Lakini usipofanya hivyo itakuwa mbaya zaidi. Ni afadhali aone unamnyanyasa kwa muda mfupi hatimaye atagundua tu kuwa kosa ni la kwake.

Mwanamke hata siku moja hatakubali kujishusha kwa mme wake (reality). Na mwanamke hana ujasiri wa kuomba msamaha kwa mme (reality).

Kurudisha hali ya hewa, mwache kama wiki moja au mbili, then mwombe msamaha kwa jinsi ulivyoufikisha ujumbe. Halafu mwache tena. Baada ikipita kama miezi miwili au mitatu mwambie kama hataki tena kuitumia hiyo gari unaigawa kwa mtu mwingine (hasa ndugu wa upande wako) au unafikiria kuiuza.

Kwa mwanamke subira yavuta heri. Mwache kwa muda. Ila onesha concern kuwa kitendo chake hicho hakikufurahishi! Atajirudi tu!

Nimeipenda hii. Mizizi ya tabia kama hii wakati mwingine ni malezi na kuwa too defensive. Nadhani nahitaji ku concentrate ktk vitu muhimu na kumwacha azire mpaka achoke. Mie nasonga mbele na mapambano ya maisha.
 
inaonyesha mkeo ana hasira sana
kwann mpaka atume sms kwani nyumbani harudi (kaonyesha dharau kwako)
ss we usimuulize kaa kimya mpaka hasira zitakapoisha.
 
Unajua kuna wanawake wana shida sana; hata akipata mzinga (ajali) cha kwanza kuwazia ni matusi ya husband; lol; badilikeni bwana mwanamke si mtoto wako ni partner. yaani was treated that way home na kwa mume nipate same treatment.

But if you treat your wife like a child she will behave like one.

wakati mwingine mtu anakua mzembe mzembe inabidi kumtreat kama toto dogo...mtu akiwa straight na makini na mambo yake utaanzaje kumcontrol?
 
Huyo ili kumridhisha afurahi fungua taa zako site mirror ukiweza na kioo cha dirishan viweke kwenye buti then mwambie mke wang na mie leo wameniibia utaona atakavofunguka kwa furah si nilikwambia we unasema mie mzembe.
 
Wakuu, naomba ushauri katika mkwamo huu!Nilimpa mke wangu gari atumie kwa ajili ya shughuli zake za biashara ya duka la nguo. Kwa kwenda na kurudi nyumbani na kwa ajili ya kufuatilia mabo ya biashara yake. vile vile kwa shughuli za nyumbani kama kupeleka watoto hospitali n.k. Mimi pia nina usafiri wangu. Mwezi jana aliibiwa side mirror na taa moja ya mbele pale Kariakoo. Akaniarifu na baada ya kuona hana juhudi ya kurudishia huku akiendelea kuendesha gari "chongo" , niliamua kutumia pesa zangu kufanya replacement. Wiki mbili zilizopita nimekuta tena taa moja hakuna. Kumuuliza ikawa zogo. Anasema nisimuulize kitu yeye atarudishia. nikasubiri ikawa kama mwanzo. Baadaye nikaamua tena kununua taa nyingine na nikamwonya kuwa sitaweza kuwa nanunua taa naye anaendelea kutochukua tahadharina kuwa mwangalifu. Heeh! kumbe nimechafua hali ya hewa! Mwanamke wiki mbili hizi hatumii gari anakwenda kazini kwake kwa usafiri nisioujua. Juzi akanitumia sms akasema " sihitaji gari lako masimango yamezidi" Nishaurini wataalam,

Tayari vijana wa Kariakoo wanakumegea huyo mke we fatilia utagundua tu au unipe kazi hiyo mm nikuchunguzie kiintelejinsia.
Na jamaa zangu k.koo wengi kwenye maduka ya nguo na simu wabaya sana kwa wake za watu wanao fanyabiashara madukani.
Mzazi hapo lazima unakandamiziwa, funga biashara mwambie akae home akipika na kupakua.
 
mkuu wazazi wenu wote wana magari?hilo gari litengeneze vizuri uwapelekee kijijini mzee naye aienjoy.hawa viumbe wanaumiza kichwa sana.usitake kupigishana naye kelele.Muache aongee mwenyewe atachoka coz ukijifanya kumjibu mwisho wake utampiga makofi.chunguza mienendo yake.mke akianza dharau kua nae makini.wajue marafiki zake na vijiwe vyake.hawa viumbe hawapendi kukosolewa ndo maana anasema unamsimanga.pole sana.mia
 
Kuna wanaume wanajua kuwasimanga wake zao, hadi huruma

Yeah wakati mwingine unaweza kuwa ulisema ukapitiliza inatutokea; nami ni shahidi bahati nzuri kuna muda wa kujirudi maisha yanaenda.....kupishana kupo ndani ya nyumba usichukulie kiviiile!
 
Back
Top Bottom