kuberwa
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 574
- 131
Wakuu, naomba ushauri katika mkwamo huu!Nilimpa mke wangu gari atumie kwa ajili ya shughuli zake za biashara ya duka la nguo. Kwa kwenda na kurudi nyumbani na kwa ajili ya kufuatilia mabo ya biashara yake. vile vile kwa shughuli za nyumbani kama kupeleka watoto hospitali n.k. Mimi pia nina usafiri wangu. Mwezi jana aliibiwa side mirror na taa moja ya mbele pale Kariakoo. Akaniarifu na baada ya kuona hana juhudi ya kurudishia huku akiendelea kuendesha gari "chongo" , niliamua kutumia pesa zangu kufanya replacement. Wiki mbili zilizopita nimekuta tena taa moja hakuna. Kumuuliza ikawa zogo. Anasema nisimuulize kitu yeye atarudishia. nikasubiri ikawa kama mwanzo. Baadaye nikaamua tena kununua taa nyingine na nikamwonya kuwa sitaweza kuwa nanunua taa naye anaendelea kutochukua tahadharina kuwa mwangalifu. Heeh! kumbe nimechafua hali ya hewa! Mwanamke wiki mbili hizi hatumii gari anakwenda kazini kwake kwa usafiri nisioujua. Juzi akanitumia sms akasema " sihitaji gari lako masimango yamezidi" Nishaurini wataalam,
Possible umemsimanga nalo acha alizire! Ingekuwa mimi ingekuwa mie ingeambatana nakugonga BAN YA 2 WEEKS, NO DUDU hadi unajiju!