Mke anasomeshwa tuache Ujinga

Mke anasomeshwa tuache Ujinga

rikiboy

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
22,170
Reaction score
43,975
Jamani Jf imekuwa sehemu ya kujifunza mambo mengi sana lakini pia ukikaa vibaya unaweza toka na mawazo ya Ajabu sana na ukawa na imani za Ovyoo tu hasa Kuhusu wanawake zetu na mambo ya mapenzi.. Leo kuna uzi jamaa anaomba ushauri kuhusu mke wake aliemsomesha kumtenda lakini watu wanamshambulia sana kwa kitendo cha kumsomesha na kumlaumu lakini huyu bwana me sijaona kosa lake kama Yeye alizaaa na huyo mwanamke na Baada ya kumsomesha kama mke ambae wamezaa watoto wawili kabisa hakika Huyu Jamaa hana kosa kabisa lakini Mwenye akili mbovu na za Ovyoo ni Huyu mwanamke aisee yani kawakimbia na wanae wawili Hakika imeniumiza sana...!

Ukweli ni kuwa Mchumba hasomeshwi lakini Mke anaweza someshwa kwa mazingira haya.

1. Kwanza kama ukimsomesha mke wako akipata kazi atakuzidi kipato maana ya Mshahara kwa mbali bhasi USIMSOMESHE.

2. Kama ukimsomesha mkeo atakuwa anaenda mbali kimasomo i mean anaenda mkoa mwingine na sio ile ya kwenda chuo na kurudi nyumbani bhasi USIMSOMESHE.

3.Kama ukimsomesha mkeo bhasi atakuzidi Elimu hakika USIMSOMESHE.

Tuishi nao kwa akili sana maana Hatujui siku ile pale Bustani ya Eden shetani aliongea nini na Mwanamke..![emoji24][emoji24][emoji24][emoji2089]
IMG-20190615-WA0007.jpeg
 
Mtusomeshe jamani si mnajua hatuna ada...mwanamke akiwa na elimu na kipato familia imepona..mtapataga zawadi na maout kama yote jamani mweeh..
 
Kasomeshe uone matokeo yake,kuna mtu kapandisha uzi sio mda mrefu yamemtokea puani mambo yakusomesha mke.
 
Nashukuru nilisomeshwa na wazaz wangu sijala ada ya mwanaume na ninakula mshahara wangu tuheshimiane jaman .

Huyo mwanamke ana pepo siyo mzmaaa
 
Somesha tu hakuna aliyekukataza bro ila marufuku baadae kulia kuwa umekimbiwa.
 
mnatafuta nini kwenye kusoma soma mijitu mizima mshkutana bado unataka umrudshe mkeo darsani akatoke na walimu..si umfungulie biashara afanye mmeambiwa kila kitu kipo darsani kwani?

Mke anasomeshwa sawa ila kama elimu unayompa ina vikwazo hivyo hapo juu BORA ABAKI anakaanga mihogo inatosha.
 
Sasa mkuu napomsomesha nitajuaje kama atakuja kunizidi kipato? Hizo point mbili zamwisho nadhani nizamaana sana wewe unakadiploma Kako uchwala eti unamsomesha wife degree.... Wakupime akili sio bureee
 
Hiyo sababu ya kwanza hiyo ina walakini. ..afu ukiogopa na kuwaza kupitwa na mtu wako asilimia kubwa inakua hvyo hvyo.
 
kikao tulichokaa mwezi uliopita pale masai club wanaume wote tulitoka na azimio moja tu mchumba asomeshwi ila mke tutamsomesha kwa level ambayo haitamzidi mmeo bhasi ndio hivyo
 
Bora kumfungulia mtaji wa million 100 kuliku kusomesha mtoto wa MTU na ukute anayo sura ya mvuto usijaribu huo moto
 
Kusoma sana uoga wa maisha,kwan mafanikio yapo kwenye kusoma tu..anayesomesha ana roho ngumu sana yaan unapelekea mke wanaume wenzako kireja reja"et mke anasoma arusha ww upo dar una akili ww"?
 
Jamani Jf imekuwa sehemu ya kujifunza mambo mengi sana lakini pia ukikaa vibaya unaweza toka na mawazo ya Ajabu sana na ukawa na imani za Ovyoo tu hasa Kuhusu wanawake zetu na mambo ya mapenzi.. Leo kuna uzi jamaa anaomba ushauri kuhusu mke wake aliemsomesha kumtenda lakini watu wanamshambulia sana kwa kitendo cha kumsomesha na kumlaumu lakini huyu bwana me sijaona kosa lake kama Yeye alizaaa na huyo mwanamke na Baada ya kumsomesha kama mke ambae wamezaa watoto wawili kabisa hakika Huyu Jamaa hana kosa kabisa lakini Mwenye akili mbovu na za Ovyoo ni Huyu mwanamke aisee yani kawakimbia na wanae wawili Hakika imeniumiza sana...!

Ukweli ni kuwa Mchumba hasomeshwi lakini Mke anaweza someshwa kwa mazingira haya.

1. Kwanza kama ukimsomesha mke wako akipata kazi atakuzidi kipato maana ya Mshahara kwa mbali bhasi USIMSOMESHE.

2. Kama ukimsomesha mkeo atakuwa anaenda mbali kimasomo i mean anaenda mkoa mwingine na sio ile ya kwenda chuo na kurudi nyumbani bhasi USIMSOMESHE.

3.Kama ukimsomesha mkeo bhasi atakuzidi Elimu hakika USIMSOMESHE.

Tuishi nao kwa akili sana maana Hatujui siku ile pale Bustani ya Eden shetani aliongea nini na Mwanamke..![emoji24][emoji24][emoji24][emoji2089]View attachment 1138855
Nakumbuka mada flani huko nyuma hukuwa hivi, sijui umebadilika lini?

USITUPANGE!!!!!!
 
Back
Top Bottom