wadau hop mko poa,
naomba nielimishwe jamani kama kuna maisha ya aina hii au ni kiini macho ndo naona.kuna jamaa yangu ambaye ni swahiba wangu tangu kitambo sana ameoa na ana watoto 3.kinachonishangaza ni tabia ya mke wake,yaani amekuwa akigawa uroda hovyo,si kwa watoto anaowazidi umri wala kwa wakubwa.yaani kwa ufupi naweza kusema nanii yake iko mkononi,ukiipiga tu inaanguka unaondoka nayo.kitu kinachoniacha hoi ni huyu swahiba wangu,yaani japokuwa anajua fika kuwa mke wake anafanya uchafu huo yeye kapiga kimya.yaani haongei hata kidogo,yupo kama vile hamna kinachoendelea.kuna wakati alisafiri nje ya nchi kwa wiki mbili akaniachia familia yake niiangalie,so nikawa naenda kuicheki,kuna siku niko siting room namsubir shemeji yangu huyo atoke tusalimiane mara kinatoka kidume kimoja hivi kimejifunga kanga yake,nikamsalimia kama kawaida kisha shemeji yangu akaja tukasalimiana nikasepa.siku nyingine niko sehem napata soda,shem wangu huyo kanipita tena na kijamaa kimoja hivi,tena bila aibu akanisalimia halafu haooo wakazama kwa chumba.yaani mwanamke anafanya kama vile sio mke wa mtu eti.jamaa aliporudi nilimueleza ukweli kuhusu wyf wake but mshikaji kabaki kucheka cheka na maisha yakaendelea kama kawaida.kwa sasa hali ni mbaya mno lakini jamaa kama vile kipofu flani hivi.kuna kipindi nilifikia hatua ya kumuuliza kama amepoteza nguvu zake ili nimshauri akaonane na wataalam wamsaidie but jamaa anasema yuko poa.sasa kwanini asimkemee mkewe?hana jibu.imefikia hatua hata vichalii vinavyojifunza kuduu hapa mtaani vinamzoa kiholela holela tu,yaani hata watoto wake hasa aliye std 7 mwaka huu hana raha kabisa,yaani mtoto mdogo but anafeel aibu kwa anayoyafanya mama yake.nashindwa kujua tatizo liko wapi ili niweze kumsaidia swahiba wangu coz cjui tatizo ni yeye au ni mke?
NINA FEEL VIBAYA NA NINGEPENDA KUONA AIBU HII INAONDOKA KWA RAFIKI YANGU LAKINI CJUI NIANZIE WAPI.