Evelyn Salt
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 77,105
- 165,328
Hahahaaaa... sio ndio maana huwa mnatuonea sana linapokuja lile swala la Papuchi?
Kwa maana wanaume wanaonekana wapo deperate sana na hio kitu mwanamke anamringia.
Fundi ujenzi mmoja alikua anatupa kisa chake na mkewe akasema alioa mke kule kijijini akamleta mjini. mkewe akabana bana hela ya matumizi na nyingine nyingine akacheza kamchezo gani sijui unaitwa kibati na majirani zake.. ilipofika zamu yake akapokea laki NNE na nusu... kilichofuatia akamwambia mumewe ''sikutaki tena narudi nyumbani' Mume akajua kiburi ni hako kahela maana alikua hajawahi kushika hela nyingi ivo... akamwambia nenda mama. wapi na wapi baada ya wiki mbili kaja kumlilia mumewe? maana vile vihela alienda kujidai kuweka jina kijijini fasta zimeshakauka. kwa kuwa mumewe alikua keshajua ni ulimbukeni wa hela unamsumbua.. akampokea mkewe bahati mbaya jamaa amefariki mwaka jana.
Wanawake hamtabiriki aisee.
Hatueleweki kama hizi nanii zetu kwakweli.....