Mke ana wivu sana

Mke ana wivu sana

Alvin Slain

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
6,375
Reaction score
3,665
Habari za huku.

Hongereni kwa uchaguzi ulioisha hivi karibuni.

Ndugu wanajamii nina mke ambae ana wivu na mimi mpaka nafikiri kumuacha maana hataki hata niongee na watu wa jinsia yangu.

Yeye kila siku analalamika kuwa nawapenda wazazi na marafiki kuliko yeye.

Muda wote anataka tukae wote tu hata kazi hakuna kufanya hivi ndio inakuwaga hivi au anataka kunianzishia isidingo?

Karibu.
 
Habari za huku.

Hongereni kwa uchaguzi ulioisha hivi karibuni.

Ndugu wanajamii nina mke ambae ana wivu na mimi mpaka nafikiri kumuacha maana hataki hata niongee na watu wa jinsia yangu.

Yeye kila siku analalamika kuwa nawapenda wazazi na marafiki kuliko yeye.

Muda wote anataka tukae wote tu hata kazi hakuna kufanya hivi ndio inakuwaga hivi au anataka kunianzishia isidingo?

Karibu.
kwa hiyo muda wote anataka uongee na yeye tu du!
 
Mpe mtoto atatulia

Hajakomaa mawazo huyo, hapo sijajua umri wake lkn kumpa mtoto pekee haitoshi. Wakati mwingine wanawake namna hii ni wale ambao wana wazo lkn kukuambia anshindwa badala yake anabaki kulalama kwa mfano alitaka umwezeshe ktk jambo kila hajakwambie then anaona unatuma pesa home, unawasaidia washkaj. Hyu ukikurupuka kumpa mtoto na hujamsoma atasumbua zaid badala ya kutulia na huenda akakuachia mtoto maana atachukulia umemzima asiendelee na mipango yake.
 
Mtafutie cha kufanya awe bize. Huo ni ubinafsi uliokithiri (egoism) ukiendekeza itakula kwako.
 
Mtafutie cha kufanya awe bize. Huo ni ubinafsi uliokithiri (egoism) ukiendekeza itakula kwako.

Nafikir kweli ni ubnafsi umemmjaa yaani anafikir nikiongea na watu wengine yeye kuna kitu anakosa
 
Siamini hayo mavitu na mtu kujiendekeza

ts nice kama umejua ni kujiendekeza,so stand as man maana inaonesha mkeo kakushika akili.Inamaana hauna kazi za kufanya hadi atake mkae wote siku nzima? labda unajishughulisha na kazi gani ebu tujulishe.
 
Anamiaka mingapi? wewe ndio mwanamme wake wa kwanza au alikuanao kabla yako? asikufuje na kukufanya kama kakuzaa yeye,huyo anatabia kama ya Binamu yangu mke hataki hata mume asalimie ndugu jamaa na marafiki ambao aliwakuta kabla yeye hajaolewa,ukipiga cm kaipokea yeye,ukifika kwake ndio anajitia anampenda mume mara kamfuta jasho,mara kamtia vijiti vya masikio,mara yani mpaka utachefukwa na roho,nyumba imejaa ndugu wa mke tele,sasa huyo atakufanya mpaka watu wako wa karibu ukosane nao...
 
Ndio muda wote anataka ukiamka ukae nae tu hata usitoke nje.
Na mimi sio mtu wa hivo sasa ninakua ktk hali ngumu
hebu jaribu kumwambia kuna rafiki zako unataka uonane nao .so muende wote (akikataa atakwambia nenda mwenyewe:redface🙂
 
ngoja apate wa kuwa nae mda mwingi, atakuruhusu kutoka ata kwa siku tatu.......
nyie wanaume wa sikuizi acheni kuwa bize sana na marafiki kuliko mke na watoto, kaa nae ujue yaliyo moyoni kwake na akilini kwake kwanza
 
Apolinary kumbe ulishaoa, mbona kimya kimya ulivokua mpweke ulitushirikisha ulivovuta jiko kimya duh
 
Mpe mtoto atatulia
umempa jibu zuri. Ukaribu wa mke na mume.unapungua mara mtoto anapopatikana. Attention ya mama kwa kiasi kikubwa inakuwa kwa mtoto. Hii sijui.inakuwaje maana hata kwa wanyama iko hivo. Hawana muda wa mapenzi kama mama ananyonyesha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom